Gamba halisi la nyoka hili hapa by Prof Euphrase Kezilahabi

KAMBOTA

Senior Member
Mar 21, 2011
176
103
gamba la nyoka.jpg
Nasikia huko mtaani kitabu hiki cha Professor Euphrase Kezilahabi kinasakwa kama almasi kila mtu anataka kukisoma yaelekea humu ndo kuna gamba halisi la nyoka eeeh.....!

 
Sahihisho: Prof. Euphrase Kezilahabi bado yuko hai na yuko kikazi Botswana. tafadhali sahihisha hili.
 
Mzee sahihisha hapo kama ulivyoshauriwa. Au mod tafadhari saidia!! Prof. Bado yuko hai kama alivyokwambia jamaa hapo juu. Yuko Gaborone, Botswana tangu mwaka 95. Kwa kuwa humsikii nchini haina maana ametutoka!!!
 
Asanteni sana wadau na samahani kwa kutoa taarifa isiyo sahihi kwakweli nashukuru sana kwa kunikosoa pia naomba mtu mmwenye kufahamu mawasiliano ya huyu mwanataaluma anipe hata anwani ya barua pepe, sanduku la posta, website/blog au namba za simu , naomba anitumie kwenda novakambota@gmail.com
 
Naomba moderator sahihisha hicho kichwa cha thread toa hilo neno the late
 
Hiki kitabu, kilinikuza kifikra na kutokana na kitabu hiki ndiyo maana nikaamua kujiita Gamba La Nyoka!, kusema kweli muandishi alifanya kazi nzuri sana kwenye hiki kitabu.
Katika hiki kitabu kuna mzee mmoja anaitwa Mzee Chilongo, yeye anapinga juhudi za maendeleo kwa hoja za ajabu ajabu kwa kudai eti " kuna haja gani ya kujenga vyoo wakati kijiji kimezungukwa na mapori?".hahah.
Katika hicho kitabu kuna vijana wamemaliza chuo kikuu, wanataka kuleta theory walizofundishwa darasani katika maisha ya kawaida ya kila siku, wanakuja kukuta kumbe hali halisi ni tofauti kabisa!
Ni kitabu kizuri kwelikweli, kama wewe ni greatthinker anayetaka kuelewa jamii ya Kitanzania imetoka wapi, ni vyema ukakisoma kitabu hiki, Mwandishi pia aliandika kitabu kinachoitwa "Dunia Uwanja wa Fujo".
 
Baadhi ya kazi zake ni hizi hapa
 

Attachments

  • 1451234626952.jpg
    1451234626952.jpg
    53.3 KB · Views: 503
Profesa Kezilahabi ni Mwanafalsafa makini.
Miongoni mwa kazi zake nyingine ni.
1) Mzingile
2) Nagona
3) Rosa Mistika
4) Dunia uwanja wa fujo
 
Hiki kitabu, kilinikuza kifikra na kutokana na kitabu hiki ndiyo maana nikaamua kujiita Gamba La Nyoka!, kusema kweli muandishi alifanya kazi nzuri sana kwenye hiki kitabu.
Katika hiki kitabu kuna mzee mmoja anaitwa Mzee Chilongo, yeye anapinga juhudi za maendeleo kwa hoja za ajabu ajabu kwa kudai eti " kuna haja gani ya kujenga vyoo wakati kijiji kimezungukwa na mapori?".hahah.
Katika hicho kitabu kuna vijana wamemaliza chuo kikuu, wanataka kuleta theory walizofundishwa darasani katika maisha ya kawaida ya kila siku, wanakuja kukuta kumbe hali halisi ni tofauti kabisa!
Ni kitabu kizuri kwelikweli, kama wewe ni greatthinker anayetaka kuelewa jamii ya Kitanzania imetoka wapi, ni vyema ukakisoma kitabu hiki, Mwandishi pia aliandika kitabu kinachoitwa "Dunia Uwanja wa Fujo".

Pia Aliandika Kitabu Kingine Maarufu, Rosamistica
 
mwandishi ungesema jaman kuna kitabu hiki....... nunueni msome but si kufanya promo ya kizaman kama hii. hakuna mtu anayekizungumzia mtaani. watu hawavijui vitabu hivi isipokuwa sisi wachache. so ungesema tu kuna kitabu kinaitwa .............
 
Back
Top Bottom