Galileo Galilei: Mwanasayansi aliyeukana ukweli aliouamini

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,425
BANNER-PAGE-2-825x510.jpg

Galileo alizaliwa 1564 na baba aliyekuwa mwanamziki,alisomea maswala ya tiba chuo kikuu,ila baadaye aliacha na kusomea fizikia na hesabu,jambo lililo mfanya arudi nyumbani bila cheti chochote cha masomo.Ila bado licha ya hayo alikuja kuwa mwanahesabu enzi hizo alikuwa akifundisha chuo kikuu.Hakika alikuwa anavipaji vingi alikuwa mnajimu, mwanafizikia na mhandisi.

Kupia uchunguzi na uvumbuzi na uboreshaji wa vifaa mbalimbali(aliboresha hadubini ijapo hakuivumbua) kulimfanya ajikute akiamini nadharia ya Coperician mwishoni mwa karne ya 16.Nadharia hiyo inasema dunia inaizunguka jua.Galileo alisadiki amethibitisha nadharia ya coprician.

Katka kipindi hiki nadharia hii ilipigwa marufuku na kuitwa ni yakizushi na ya kumkufuru Mungu pia kukana maandiko matakatifu ya Biblia(Yoshuo10:12);hivyo mtu alie amini au kutetea nadharia hiyo aliitwa mwasi na mzushi na hukumu yake ilikuwa ni kifo au kifungo cha maisha...

Galileo alishishindwakujizuia juu ya uvumbuzi wake ungeo weza kuthibisha ukweli huu uliopgwa na kanisa na kupigwa marufuku:alitaka kuwathibitishia watu kuwa nadharia ya copriacian niya kweli na hivyo marufuku hiyo inapaswa kuondolewa...

Ilimlazimu kufika Ruma 1611 ili kukutana na uongozi wa kanisa,apate kuwa sadikisha ukweli huu kuwa dunia inaizunguka jua..alipo fika Roma alikutana na mwanateolojia maarufu na mashuhuri wakati huo aliyekuwa anamwamini sana Ballerimire Robit .Galileo aliamini akimsadikisha huyo ukweli wake utapokelewa kwa kuwa ndie aliyekuwa mashuhuri wa kupinga waasi.Balleriamine alijulikana kama *Kiboko cha waasi*Alikuwa mjenga hoja kupitia maandiko yenye ushawishi kuwa jua inaizukuka dunia,hujongea kutoka masharki kwenda magharibi.

Licha ya Galileo kumshawishi Balkermine kwa kutumia vifaa na kwa busara.Ballerimine alimwambia Galileo akome kuendeleza kutangaza nadharia hiyo kwani inapingana na Mungu.

Licha ya kukatazwa kuendeleza kutangaza ukweli huo ulioitwa uzushi ila bado kwa busara aliendeleza kuutangaza ukweli huu alio uamini.Baada ya miaka 17 hii ilikuwa mwaka 1632 alifunguliwa mashitaka ya uasi. Mwaka huo aliitwa afike ktk mahaka ya kuwa hukumu waasi akiwa ni mzee wa miaka 70,alishidwa kufika kwa kuwa alikuwa mgojwa.Hata hivyo alipewa vitisho na Papa Urban wa nne kuwa asioofika atateswa na kufikisha kwa nguvu.

Alifika 1633 mwaka mmoja baadaye na kuambia akane uasi huo,akambia aandike kitabu kuunga mkono nadharia kuwa dunia haizunguki bali jua.Aliandika kitabu kilicho itwa "Diologue concerning two chief wold system"kilicho unga mkono nadharia ya copernician.

Jun 22/1633 alihukumiwa ktk mahakama ya waasi kwa kosa la kuamini fundisho la uongo kinyume na mafundisho matakatifu yasemayo jua hujongea hutoka masharik had mashariki na dunia iko ktk ya ulimwengu.

Galileo hakutaka kufa kwa ukweli alio uamini na kuusadiki;kwa kuhofu kuuwawa ilimlazm kuukana ukweli alio usadiki na kuwasadikisha wengine kuwa dunia ndio inaizunguka jua.

Kutokana na utaratibu wa kanisa katoliki wakati huo chini ya papa Urabn wa nne alivikwa mavazi ya toba na kisha kutamka maneno haya,mbele ya umati wawatu ambao walikuwa wameanza kuamini wengine ukweli huu akasema

"...ninakana,ninalaani na ninachukia makosa yaliyotajwa na copreciani kuwa dunia ndio inazunguka jua,na makosa yote kwa ujumla ikiwemo kutangaza,uasi na chochote kinacho pinga kanisa takatifu"

Licha ya kutubu hakimu alimhukumu kifungo cha cha maisha gerezani,ila kutokana na uzee alifungwa kifungo cha maisha nyumbani. Alipo kuwa akikaa kwa upweke na majuto ya kuukana ukweli aliouamini. Jambo hli lilimsononesha hadi kufaa..

Wanafunzi wake walio mwamini aliwaambia
"...ijapo Maandiko hayawez kukosea ila wahubiri na wafasiri wanaweza kukokea kwa njia nying kuyaeleza maandiko matakatifu;maranyingi hukosea sana wanapo fasiri neno kwa neno..."
Baadaye kanisa la Romani katolik liliomba msamaha kwa kudai kesi ya Galileo hukumu yake haikuwa sawa,Papa Yohana wa pili asisema Kesi ya Galileo ilikuwa kama ya Yesu,wanatheorojia wakati ule walishidwa kufasir maandiko vizuri kwani Galileo alikuwa sahihi kusema DUNIA INAIZUNGUKA JUA!!

Nakumbuka msemo wake mmoja alipoambiwa nadharia alio iamini inapingana na Mungu alisema

"God is known by nature in his work and by doctrine in his reveled word"

Alipenda sana kujifunza kwa kilq mtu bila kujali elimu wala wadhifa wake aliwahi sema

"I have never met a man so ignorant that ihve could'nt learn somthing frome him"

JE SISI TUNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWAKE?

1-Maadiko matakatifu hayakosei ila wafasiri nawanateorojia huweza kuya fasir isivyo na kupoteza maana halisi na ukweli wa nene

2-Sayansi haipingani na Mungu,ila teolojia na uelewq ndio unaoweza kukufanyq uone hivyo

3-Papa anaweza kukosea,si kweli hakosei kamavyo sadiki weng kama angelikuwa hakosei asinge ruhusu Galileo kuhukumiwa kwa ukweli

4-Ni bora kufa kwa ukweli unaoamini na ulio usadiki kuliko kuishi kwa kuukana ukweli na kujirazimisha kuusadiki uongo.

5 Ukweli unaousadiki leo ambao wengne hawauoni usiukatee na kuamini uongo kwa kuwa hauungwi mkono na watu wengi

6 Kusomea usicho kipende ni kuamua kuishi maisha ya kusononeka,na kuzika ndoto zako pia karama ukiyo nayo

6 Mungu hujifunua kwa wanadamu kupitia vitu vya asili,kazi yake na kupitia maandiko yako..hivyo waalimu wazuri juu ya Mungu ni VITU VYA ASIRI,KAZI YAKE NA KUPITIA MAANDIKO YAKE MATAKATIFU.
 
Kanisa katoliki lilimtesa Galileo bila sababu inatakiwa kwenye sala zao wamuombee Sana , pia wasiache kutubu Kama Kanisa walifanya mengi kuwanyanyasa wengine...
Papa did confess for such crime and Pope ndo kanisa katoliki lenyewe.

I loved Galileo in my studies!
 
Uzi mzuri lakini ninashindwa kukuelewa pale unaposema" ukweli aliouamini".

Mkuu ukishajua kitu, hiyo sio imani tena, imani ni kutokuwa na hakika na jambo.

Galileo alijua kuwa jua halizunguki, hakuamini kuwa jua halizunguki.
 
Baada ya Galileo Galilei wamezaliwa wafia dini wengne ambao hutumia hayo hayo maandiko kupotosha ukweli. Wengne wakaibuka miaka hiyo hiyo ya Galileo huko uarabuni na kuungana na wenzao kuifanya dunia uwanja wa fujo
 
Kwakweli Kanisa limeua mtu asiye na hatia na kuuchelewesha ulimwengu kupata ukweli kwa wakati uliopaswa,Inabidi watubu
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom