johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 82,754
- 139,571
Mkuu wa wilaya ya Gairo amemtuhumu mwenyekiti wa CCM wa wilaya kwamba amehongwa gari na mbunge Ahmed Shabiby ili wambebe kwenye uchaguzi. Mkuu wa wilaya amewataka Takukuru wamshughulikie mwenyekiti huyo.
Naye mwenyekiti wa CCM amesema gari hilo hajahongwa na Shabiby kama inavyodaiwa bali amenunuliwa na waziri wa Katiba na sheria Dr Mwigullu Nchemba. Mwenyekiti amesema yeye pia ni msaidizi wa Dkt. Mwigulu jimboni Iramba akisimamia mahusiano ya mbunge na Waislamu hivyo amenunuliwa gari hiyo kama kitendea kazi.
Kuhusu kuchunguzwa mwenyekiti amesema ni kweli aliitwa Takukuru wilayani na wakamwambia tuhuma hizo ni za kisiasa hivyo jalada limepelekwa Dodoma ambako alihojiwa Ijumaa iliyopita na sasa anasubiri majibu.
Mwisho mwenyekiti amebainisha kuwa mkuu wa wilaya ni mtu mkorofi na kwamba anataka kugombea ubunge wa jimbo hilo na kila wakati amekuwa anawatisha kwamba yeye ana ulinzi wa kigogo aliye juu.
Chanzo: Clouds 360
Maendeleo hayana vyama!
Naye mwenyekiti wa CCM amesema gari hilo hajahongwa na Shabiby kama inavyodaiwa bali amenunuliwa na waziri wa Katiba na sheria Dr Mwigullu Nchemba. Mwenyekiti amesema yeye pia ni msaidizi wa Dkt. Mwigulu jimboni Iramba akisimamia mahusiano ya mbunge na Waislamu hivyo amenunuliwa gari hiyo kama kitendea kazi.
Kuhusu kuchunguzwa mwenyekiti amesema ni kweli aliitwa Takukuru wilayani na wakamwambia tuhuma hizo ni za kisiasa hivyo jalada limepelekwa Dodoma ambako alihojiwa Ijumaa iliyopita na sasa anasubiri majibu.
Mwisho mwenyekiti amebainisha kuwa mkuu wa wilaya ni mtu mkorofi na kwamba anataka kugombea ubunge wa jimbo hilo na kila wakati amekuwa anawatisha kwamba yeye ana ulinzi wa kigogo aliye juu.
Chanzo: Clouds 360
Maendeleo hayana vyama!