Gaddafi na mkewe chupuchupu, mtoto na wajukuu wake waangamizwa
Seiful Arabi mtoto wa dikteta Muammar Gaddafi kiongozi wa Libya pamoja na wajukuu wake watatu wameuawa kwenye mashambulizi ya ndege za Nato huko Tripoli, mji mkuu wa Libya. Taarifa zinasema kuwa, Kanali Muammar Gaddafi ameponea chupuchupu kwenye shambulio hilo. Vikosi vitiifu kwa Gaddafi vimeeleza kuwa, mashambulio hayo yamepelekea kuharibiwa vibaya kituo kimoja cha watoto mjini Tripoli. Taarifa hiyo imeendelea kueleza kuwa, kwa akali watu 15 akiwemo mtoto mwenye umri wa miaka tisa wameuawa, baada ya ndege za Nato kushambulia mji wa Misratah. Gaddafi amesikika akisema jana kwamba, hatong'atuka madarakani, amma yuko tayari kufanya mazungumzo iwapo vikosi vya Nato vitasimamisha mashambulizi yao. Hata hivyo majeshi ya Nato na hali kadhalika wanamapinduzi nchini humo wametupilia mbali pendekezo hilo la Gaddafi, na kusisitiza juu ya kung'olewa madarakani dikteta huyo.
Kwa hisani ya Idhaa ya Kiswahili ya Redio Tehran, Iran
Kwa hisani ya Idhaa ya Kiswahili ya Redio Tehran, Iran