Fursa za ujasiriamali Zanzibar

HatibuZ

Member
Dec 27, 2013
20
15
Habari zenu wakuu,
Nategemea mnaendelea vizuri na pirikapirika za kujitafutia kipato.
Nashkuru kuifahamu jf, kwa kweli ni sehemu muafaka ya kuzidisha maarifa binafsi ya fani fulani na ya maisha kwa ujumla, kiasi ya kwamba imesheheni taarifa,mawazo huru,miongozo na kubwa zaidi inatoa nafasi ya fikra endelevu.

Kwahivyo nami nimeonelea niwasilishe dukuduku langu ili nipate kutoka kwenu ushauri na maelekezo yatayoweza kunisaidia kupata rizki na kuinuka kimaisha.

Kwa kua ugumu wa maisha unazidi kila kukicha huku fursa za ajira zikiwa chache kulinganisha na idadi ya wahitimu kila mwaka, nimeamua kujiingiza ktk ujasiriamali, hivyo napanga napangua, nafanya upembuzi wa biashara husika/namna ya kujiajiri.

Maelezo binafsi:-
ELIMU: Mimi ni mhitimu wa shahada ya kwanza ktk fani ya usimamizi wa fedha ( finance ).
UZOEFU: niliwahi kujishughulisha na masuala ya utalii zanzibar; kubook malazi, kuandaa tours,kuwaunganishia watalii usafiri n.k ila siku hizi kwa mtu binafsi(na hata kwa kampuni ndogo) imekua ngumu sana.
SEHEMU KUSUDIWA: Zanzibar, mjini unguja.
MTAJI WA FEDHA: milioni 1.
MTAJI WA WAZO: bado haupo sawa - najaribu kujiepusha na kucopy na kupesti bila mpango maalumu.

Kutokana na maelezo hayo, naomba ushauri wenu:
1- nifanye nini?
2- Biashara gani inaweza kunitoa na ujanja+skills zipi zinahitajika kwayo?
3-Fursa gani zilizopo Unguja na vipi naweza kuzichangamkia?

Mawazo na michango yenu naithamini.

Hatibu Golo
Jang'ombe - ZnZ
 
Mkuu hongera sana kwa post nzuri. Haya ndo aina ya mawazo kijana wa kizanzibar anatakiwa awe nayo na sio issue za kulaumu au kuweka imani kwa wanasiasa wachumia matumbo (CUF+CCM).

Back to the topic, ushauri wangu jaribu kujifanyia SWOT analysis. Yaani pambanua Strengths ulizonazo (ile area ambayo naturally upo vizuri), weakness zako (yaani madhaifu uliyonayo), Opportunities ( fursa zilizo kuzunguka) afu umalizie na Threats ( Vikwazo vilivyopo) . Cha muhimu wazo zuri la biashara linatakiwa kutoka kwako na liendane na strengths ulizonazo. Watalaamu wanashauri ni vema watu wafanye kile kitu wanapenda kutoka mioyoni mwao kwani watafanya kwa kujituma na kwa ustadi wa hali ya juu!
Habari zenu wakuu,
Nategemea mnaendelea vizuri na pirikapirika za kujitafutia kipato.
Nashkuru kuifahamu jf, kwa kweli ni sehemu muafaka ya kuzidisha maarifa binafsi ya fani fulani na ya maisha kwa ujumla, kiasi ya kwamba imesheheni taarifa,mawazo huru,miongozo na kubwa zaidi inatoa nafasi ya fikra endelevu.

Kwahivyo nami nimeonelea niwasilishe dukuduku langu ili nipate kutoka kwenu ushauri na maelekezo yatayoweza kunisaidia kupata rizki na kuinuka kimaisha.

Kwa kua ugumu wa maisha unazidi kila kukicha huku fursa za ajira zikiwa chache kulinganisha na idadi ya wahitimu kila mwaka, nimeamua kujiingiza ktk ujasiriamali, hivyo napanga napangua, nafanya upembuzi wa biashara husika/namna ya kujiajiri.

Maelezo binafsi:-
ELIMU: Mimi ni mhitimu wa shahada ya kwanza ktk fani ya usimamizi wa fedha ( finance ).
UZOEFU: niliwahi kujishughulisha na masuala ya utalii zanzibar; kubook malazi, kuandaa tours,kuwaunganishia watalii usafiri n.k ila siku hizi kwa mtu binafsi(na hata kwa kampuni ndogo) imekua ngumu sana.
SEHEMU KUSUDIWA: Zanzibar, mjini unguja.
MTAJI WA FEDHA: milioni 1.
MTAJI WA WAZO: bado haupo sawa - najaribu kujiepusha na kucopy na kupesti bila mpango maalumu.

Kutokana na maelezo hayo, naomba ushauri wenu:
1- nifanye nini?
2- Biashara gani inaweza kunitoa na ujanja+skills zipi zinahitajika kwayo?
3-Fursa gani zilizopo Unguja na vipi naweza kuzichangamkia?

Mawazo na michango yenu naithamini.

Hatibu Golo
Jang'ombe - ZnZ
 
Asante mkuu INVESTAtz,
Ushauri wako naendelea kuufanyia kazi.

Kuhusu siasa, nashkuru nazielewa kiasi siasa za tanzania hasa zenji, hivyo nimejieka mbali na ushabiki wa kufuata mkumbo, nabakia kua mfuatiliaji tu wa yanayojiri na kutumia haki zangu km raia.

Ama kuhusu upembuzi binafsi, naweza kuufupisha kwa hii; mixed personal-business related swot analysis:-

Uimara na fursa:
naweza fanya vizuri ktk ufundishaji; lugha mbili tatu na hata ktk fani yng for beginners.
Udhaifu na vikwazo:
imani ndogo kwa watu walionizunguka ktk kushirikiana kujikwamua (due to the history - mawazo ya miradi mengi yamefeli kabla + baada tu ya kuanza ) so inawia vigumu kuchagua washirika sahihi.
 
Back
Top Bottom