Fursa ya biashara ndani ya visiwa vya Comoro

Duh .....mimi nakusanya sana iriki milima ya usambara ila nauzia mombasa na uganda
Sasa tunafanyaje?maana mimi ni mzee wa kubadili Gia angani
Any way nishafikaga visiwa vya moheli lkn nkitokea mafia
Namba ya sim nshakupa fanya hivyo tuyajenge

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee mwenzangu vipi!? Ulifanikiwa!?
 
Duh .....mimi nakusanya sana iriki milima ya usambara ila nauzia mombasa na uganda
Sasa tunafanyaje?maana mimi ni mzee wa kubadili Gia angani
Any way nishafikaga visiwa vya moheli lkn nkitokea mafia
Namba ya sim nshakupa fanya hivyo tuyajenge

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi ulifanikiwa kwenda Comoro?
Mimi naelekea huko hivi karibuni
 
Mimi ni mfanyabiashara Tanzania na Comoro. Nilianza mwaka jana lakini mafaniko ni makubwa kwan kuna fursa nyingi sana sababu visiwa vya Comoro 96% wanategemea vitu pamoja na chakula kutoka nje.

Hivyo hupelekea kuwa na mahitaji kubwa ya hasa vyakula lakini changamoto hasa inayopelekea biashara ya Comoro kusua sua ni usafirishaji lakini fursa ni nyingi sana pia changamoto nyingne ni mmoja hasa kwa Watanzania hamna umoja kabisa wa kibiashara kwan hata kwenye upende wa usafirishaji Wacomoro ndio wanakodi meli tena hapa Tanzania na kijipatia pesa nzuri sana

Wakati tunauwezo wa kujikusanya wafanya biashara na kukodi chombo tutafanya supply kwa wakati sababu kuna kipindi Comoro nzima haina kitunguu ama vinywaj kama juice sababu tu hamna meli za kwenda lakini fursa ni nyingi sana

Herr muller
Chakula cha aina gani? Hata matoke ya Bukoba wanayahitaji? Au ubwabwa tu?
 
Ukiwa hapa Mtwara mitaa ya Chikongola utashuhudia lundo la Wacomoro wakija kufata bidhaa Tanzania.
Kwenye mtaa huu kuanzia guest house za Chilindima kuja hadi huku inapoishia Tiffany hotel kote wanajaa hawa jamaa. Ila guest yao pendwa ni Obrigado au Chalinze maana hapo ndio wanaona ni sehemu salama kuweka vitu vyao.
Wakifika Mtwara hapa wanaanza kupanga mipango ya safari ya kuja Dar, wana jamaa yao ambaye ni Mcomoro pia lakini anaishi Dar. Huyu jamaa huwa wanamtumia katika mizunguko yao hasa wakishaingia Tanzania, wanamlipia hela anakuja Mtwara anatafuta usafiri wa kuja Dar, wakifika huko anawatembeza kununua bidhaa na kurudi nazo Mtwara.
Hawa jamaa huku Tanzania wanakuja na meli yao wakiwa wameikodi, wananunua bidhaa nyingi sana yani ni kila kitu kilichopo mbele yao wananunua.
Leo wameondoka na nimeongea nao wanapanga kurudi tena mwezi wa sita kuhemea tena.
Comoro sijafika ila kwa mizigo walonunua hawa jamaa inaonyeaha dhahiri kuwa pesa ipo kama utapata mwenyeji kule.
 
Ukiwa hapa Mtwara mitaa ya Chikongola utashuhudia lundo la Wacomoro wakija kufata bidhaa Tanzania.
Kwenye mtaa huu kuanzia guest house za Chilindima kuja hadi huku inapoishia Tiffany hotel kote wanajaa hawa jamaa. Ila guest yao pendwa ni Obrigado au Chalinze maana hapo ndio wanaona ni sehemu salama kuweka vitu vyao.
Wakifika Mtwara hapa wanaanza kupanga mipango ya safari ya kuja Dar, wana jamaa yao ambaye ni Mcomoro pia lakini anaishi Dar. Huyu jamaa huwa wanamtumia katika mizunguko yao hasa wakishaingia Tanzania, wanamlipia hela anakuja Mtwara anatafuta usafiri wa kuja Dar, wakifika huko anawatembeza kununua bidhaa na kurudi nazo Mtwara.
Hawa jamaa huku Tanzania wanakuja na meli yao wakiwa wameikodi, wananunua bidhaa nyingi sana yani ni kila kitu kilichopo mbele yao wananunua.
Leo wameondoka na nimeongea nao wanapanga kurudi tena mwezi wa sita kuhemea tena.
Comoro sijafika ila kwa mizigo walonunua hawa jamaa inaonyeaha dhahiri kuwa pesa ipo kama utapata mwenyeji kule.
Dah.. yaan natamani sana kupata connection nao.. chukua number zahuyu jamaa yao wa Tz ili niongee naye
 
Alichoongea mtoa mada ni kweli kabisa kuhusu fursa za biashara Comoro, nakumbuka mwaka 2018 tuliungana watu kadhaa tukajichanga ili tukodi meli ya kupeleka bidhaa Comoro na biashara tuliyoikusudia ilikuwa mbuzi. Tulifanikiwa kweli kukodi hiyo meli kwa mmiliki kutoka Zanzibar kwa milioni 46.

Baada ya kukamilisha process zote za vibali mbuzi walichelewa kidogo kupatikana kutokana na idadi tuliyokusudia so ikabidi tupeleke kwanza mizigo ya wafanyabiashara wengine then meli ikirudi ndo tuanze biashara yetu ya mbuzi kama kawaida. Tulimchagua mwenzetu mmoja aende na meli na kupokea malipo yote ila baada ya kuondoka na ile meli na kupata malipo akatokomea.

Tulifuatilia sana hadi kwenda mahamani ila ndo hivyo tena haikuwezekana ikabidi kila mtu ashike njia yake maana wengi walikuwa very disappointed, mpaka leo plan nzima ya biashara ipo kwenye pc yangu huwa naiangalia tu but I know oneday hii biashara nitaifanya tu sijakata tamaa.
 
Mwenye uzi kaweka bayana kuwa fursa ni nyingi na soko ni la uhakika ukitoa changamoto ndogo ndogo kama kodi,viza n.k ambazo haziwezi kumkwamisha mfanyabiashara mwenye malengo..,So Changamoto kubwa aliyoianisha hapa ni USAFIRI.., wapo Wafanyabiashara wa Tanzania wenye nia ya dhati(seriously) tuunganishe nguvu yetu kwa pamoja tuweze kodi meli na kupeleka bidhaa..,binafsi natoka Njombe nadili na uuzaji wa mbao.Nna tafuta sana soko la mbao,ambao niliona uzi mmoja humu unasema soko kule ni kubwa..,

Hivyo kama tupo tayari tujadili ni kwa namna gani tuungane na kukodi meli ya kutufikisha sokoni
Ndugu soko la mbao kule ni changamoto asikudanganye mtu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom