Fursa Congo: Sasa tuboreshe Tazara kuwa SGR, njia nne Mbeya -Songwe na tujenge Barabara na reli ya Kisasa hadi bandari ya Kalemi, Katavi

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,227
26,048
Baada ya DRC kuingia rasmi EAC , mataifa makubwa katika Jumuiya hii Uganda Kenya na Tanzania,yanaendelea kupambana kukamata fursa ili kushika soko la nchi hii yenye watu zaidi ya Milioni 100

Wakati Uganda akijenga Barabara kuingia majimbo ya kaskazini mwa Congo, Kenya anafungua Ofisi Mombasa Kwa ajili ya Wafanyabiashara wa Congo kuweka kituo chao ili kupitisha mizigo yao kupitia Bandari ya Mombasa na kuingia Congo kupitia Uganda . Kenya pia sasa anafungua viwanda na uwekezaji Congo.

Kwetu Tanzania tumefungua tawi la crdb ili kukamata mitaji ya wakongo na tunajenga Bandari ya Kalema ili kurahisisha mizigo kuingia mashariki mwa Congo kupitia Bandari ya Kalemii iliyopo Tanganyika upande wa Congo.

Zaidi Tanzania pia kupitia Wizara ya Kilimo na Bandari tumefungua Ofisi Congo kurahisisha usafirishaji wa Mazao na Mizigo bila kusahau SGR nyingine ambayo itafika Congo kupitia Kigoma- Burundi.


Sasa Congo nao wanaifanyia maboresho makubwa bandari yao ya kalemii ili kuendana na kasi hizi za maendeleo na tangu mwaka jana mchina ameshasaini mkataba kuanza ujenzi

Ili kukamata vizuri soko la Congo hasa Kwa upande wa mashariki na kusini, hatuna budi Tanzania tuanze kufanya haya;

1. Tujenge kwa Kiwango cha rami na zege, Barabara kutoka Tanganyika hadi bandari ya Kalemi kwa Mkoa wa katavi

2. Tuboreshe na kujenga reli kwa Kiwango cha kisasa kutoka Mpanda hadi Bandari ya Kalemi

3. Tuboreshe Tazara Kwa Kiwango cha SGR mpaka Zambia na tushirikiane na Zambia kuiboresha pia reli kutoka Zambia hadi Lubumbashi, kusini mwa DRC kwa Kiwango cha SGR hata Kwa kukopa

4. Tuite sekta binafsi wajenge meli kubwa za mizigo za kisasa katika Ziwa Tanganyika. Kama hata Kwa ubia na Serikali ni sawa tu

5. Tuboreshe kwa kiwango cha kisasa barabara kutoka Mbeya hadi Songwe kwa Kiwango cha kuhimili mizigo mikubwa Hasa malori . Barabara hii itanuliwe hadi njia nne ili kuwe na njia 1 Kwa ajiri ya Malori tu hadi mpaka wa Tunduma.

Muwe na jumapili njema

Kutoka Manyara
Lord Denning
 
Theoretically your correct,lakini bila kuonyesha financial plan hakuna kitu.
Hiyo pesa ya ujenzi ni pesa ya ndani au mikopo.
Makampuni kutoka France yamepiga hodi kwa kishindo labda tuanzie hapo kwani France agependa kuimarisha miundo mbinu kwenye Francophone states zilizotuzunguka kupitia Tanzania
 
Mleta mada anaandika kama vile congo haijawahi kuwa majirani zetu.

Hao wapo kila siku tatizo ni kupata viongozi wenye uthubutu wa kufanya mambo kama hayo.

Tumeshampoteza mmoja tusubiri Mungu alete mwingine.

Ila kwa awamu hii mambo kama haya ni sahau.
 
Mleta mada anaandika kama vile congo haijawahi kuwa majirani zetu.

Hao wapo kila siku tatizo ni kupata viongozi wenye uthubutu wa kufanya mambo kama hayo.

Tumeshampoteza mmoja tusubiri Mungu alete mwingine.

Ila kwa awamu hii mambo kama haya ni sahau.
Wewe jamaa vipi, hujasikia/kuona 'vi-oligarchy' tunavyoviwezesha kufanya mambo hayo?
Awamu hii zungumza lugha hiyo utaeleweka vizuri sana.

Nikuhakikishie, siku si nyingi utasikia wakihimizwa kufanya kweli.

Sijasema ni vibaya, lakini ukiniuliza nieleze maoni yangu juu ya fursa hii nitakueleza zaidi ya kutegemea hao jamaa ndio watufanyie kila kitu, tena kwa gharama zetu sisi wenyewe.

Tuna mwambao mrefu sana kwenye ziwa letu hili tunalopakana na DRC, kama wewe ni ka-'oligarchy' kama yule jamaa aliyekuwa anasaini mikataba hivi karibuni wakati wa 'Royal Tour' nenda pale mwambaoni ukajichukulie sehemu ya kujenga bandari yako mwenyewe ya kuvushia mizigo kwenda kwa majirani zetu hao
Tunamsubiri Mo na yeye afanye vitu vyake karibuni, kama hajaanza kimya kimya. Na yule Azam?.

Tega sikio.
 
Mleta mada anaandika kama vile congo haijawahi kuwa majirani zetu.

Hao wapo kila siku tatizo ni kupata viongozi wenye uthubutu wa kufanya mambo kama hayo.

Tumeshampoteza mmoja tusubiri Mungu alete mwingine.

Ila kwa awamu hii mambo kama haya ni sahau.
Tuliempoteza ni yupi. Labda lile likurupukaji liuaji litekaji na livunja katiba? Ndio unamaanisha? Hakuwa na akili hiyo. Aliuwa wenye akili akina Mawazo Ben saanane nk
 
Mleta mada anaandika kama vile congo haijawahi kuwa majirani zetu.

Hao wapo kila siku tatizo ni kupata viongozi wenye uthubutu wa kufanya mambo kama hayo.

Tumeshampoteza mmoja tusubiri Mungu alete mwingine.

Ila kwa awamu hii mambo kama haya ni sahau.
Kaa utulie uone Samia anavyofanya zaidi
 
Baada ya DRC kuingia rasmi EAC , mataifa makubwa katika Jumuiya hii Uganda Kenya na Tanzania,yanaendelea kupambana kukamata fursa ili kushika soko la nchi hii yenye watu zaidi ya Milioni 100

Wakati Uganda akijenga Barabara kuingia majimbo ya kaskazini mwa Congo, Kenya anafungua Ofisi Mombasa Kwa ajili ya Wafanyabiashara wa Congo kuweka kituo chao ili kupitisha mizigo yao kupitia Bandari ya Mombasa na kuingia Congo kupitia Uganda . Kenya pia sasa anafungua viwanda na uwekezaji Congo.

Kwetu Tanzania tumefungua tawi la crdb ili kukamata mitaji ya wakongo na tunajenga Bandari ya Kalema ili kurahisisha mizigo kuingia mashariki mwa Congo kupitia Bandari ya Kalemii iliyopo Tanganyika upande wa Congo.

Zaidi Tanzania pia kupitia Wizara ya Kilimo na Bandari tumefungua Ofisi Congo kurahisisha usafirishaji wa Mazao na Mizigo bila kusahau SGR nyingine ambayo itafika Congo kupitia Kigoma- Burundi.


Sasa Congo nao wanaifanyia maboresho makubwa bandari yao ya kalemii ili kuendana na kasi hizi za maendeleo na tangu mwaka jana mchina ameshasaini mkataba kuanza ujenzi

Ili kukamata vizuri soko la Congo hasa Kwa upande wa mashariki na kusini, hatuna budi Tanzania tuanze kufanya haya;

1. Tujenge kwa Kiwango cha rami na zege, Barabara kutoka Tanganyika hadi bandari ya Kalemi kwa Mkoa wa katavi

2. Tuboreshe na kujenga reli kwa Kiwango cha kisasa kutoka Mpanda hadi Bandari ya Kalemi

3. Tuboreshe Tazara Kwa Kiwango cha SGR mpaka Zambia na tushirikiane na Zambia kuiboresha pia reli kutoka Zambia hadi Lubumbashi, kusini mwa DRC kwa Kiwango cha SGR hata Kwa kukopa

4. Tuite sekta binafsi wajenge meli kubwa za mizigo za kisasa katika Ziwa Tanganyika. Kama hata Kwa ubia na Serikali ni sawa tu

5. Tuboreshe kwa kiwango cha kisasa barabara kutoka Mbeya hadi Songwe kwa Kiwango cha kuhimili mizigo mikubwa Hasa malori . Barabara hii itanuliwe hadi njia nne ili kuwe na njia 1 Kwa ajiri ya Malori tu hadi mpaka wa Tunduma.

Muwe na jumapili njema

Kutoka Manyara
Lord Denning
Points nzuri sana.
I wish viongozi wangekuwa wanafikiria namna hii.
 
Lord denning ,

..Tazara haihitaji kuwekewa mataruma mapya ya Stamdard Gauge Rail.

..Mataruma yaliyopo ya Cape Gauge Rail yanatosha kwa shughuli zote za reli hiyo.

..Reli za nchi zote wanachama wa SADC ni za kiwango cha Cape Gauge Rail hivyo it makes more sense kwa Tazara kutumia kiwango hicho badala ya Standard Gauge.
 
Tazara ndugu kwanza ni kusolve problem zilizoifanya idumaee sio kifanya iwe SGRwakati nchi zote za SADC zinatumia Cape Gauge.Tatizo ni menejiment hasa upande wa Zambia ni kama wametususia Tazara hawawekezi kama Tanzania.
 
Baada ya DRC kuingia rasmi EAC , mataifa makubwa katika Jumuiya hii Uganda Kenya na Tanzania,yanaendelea kupambana kukamata fursa ili kushika soko la nchi hii yenye watu zaidi ya Milioni 100

Wakati Uganda akijenga Barabara kuingia majimbo ya kaskazini mwa Congo, Kenya anafungua Ofisi Mombasa Kwa ajili ya Wafanyabiashara wa Congo kuweka kituo chao ili kupitisha mizigo yao kupitia Bandari ya Mombasa na kuingia Congo kupitia Uganda . Kenya pia sasa anafungua viwanda na uwekezaji Congo.

Kwetu Tanzania tumefungua tawi la crdb ili kukamata mitaji ya wakongo na tunajenga Bandari ya Kalema ili kurahisisha mizigo kuingia mashariki mwa Congo kupitia Bandari ya Kalemii iliyopo Tanganyika upande wa Congo.

Zaidi Tanzania pia kupitia Wizara ya Kilimo na Bandari tumefungua Ofisi Congo kurahisisha usafirishaji wa Mazao na Mizigo bila kusahau SGR nyingine ambayo itafika Congo kupitia Kigoma- Burundi.


Sasa Congo nao wanaifanyia maboresho makubwa bandari yao ya kalemii ili kuendana na kasi hizi za maendeleo na tangu mwaka jana mchina ameshasaini mkataba kuanza ujenzi

Ili kukamata vizuri soko la Congo hasa Kwa upande wa mashariki na kusini, hatuna budi Tanzania tuanze kufanya haya;

1. Tujenge kwa Kiwango cha rami na zege, Barabara kutoka Tanganyika hadi bandari ya Kalemi kwa Mkoa wa katavi

2. Tuboreshe na kujenga reli kwa Kiwango cha kisasa kutoka Mpanda hadi Bandari ya Kalemi

3. Tuboreshe Tazara Kwa Kiwango cha SGR mpaka Zambia na tushirikiane na Zambia kuiboresha pia reli kutoka Zambia hadi Lubumbashi, kusini mwa DRC kwa Kiwango cha SGR hata Kwa kukopa

4. Tuite sekta binafsi wajenge meli kubwa za mizigo za kisasa katika Ziwa Tanganyika. Kama hata Kwa ubia na Serikali ni sawa tu

5. Tuboreshe kwa kiwango cha kisasa barabara kutoka Mbeya hadi Songwe kwa Kiwango cha kuhimili mizigo mikubwa Hasa malori . Barabara hii itanuliwe hadi njia nne ili kuwe na njia 1 Kwa ajiri ya Malori tu hadi mpaka wa Tunduma.

Muwe na jumapili njema

Kutoka Manyara
Lord Denning
Boss huna kitu chochote cha kiuchumi unachoweza kuripoti kutoka Manyara hadi uongelee ya Katavi ukiwa Manyara?
 
Back
Top Bottom