Funzo kwa wewe mwenye michepuko

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,551
Kabla mahusiano yao hayajakolea
jamaa akamkalisha chini huyu mdada na kumpa misimamo yake.

"Mpaka tumekuwa kwenye mahusiano maana yake nimekupenda
Nilikwambia tangu awali nina mke na watoto.
Nampenda mke wangu ndio maana nilifunga nae ndoa.....

Sitamani hata siku moja aje kuumia eti kwasababu yako

Sina malengo yoyote na wewe hususani ya kindoa maana tayari niko na ndoa.....nakuheshimu pia kwa nafasi yako lakini kuwa na nidhamu kwenye ndoa yangu......kukupenda wewe haina maana kwamba mke wangu simpendi no,ni udhaifu wa wanaume tulionao

Sitaki uwasiliane na mke wangu hata mara moja
Sitaki ajue nina hawara nje,mke wangu anasali anamuomba Mungu.

Hata mahusiano yetu najua ataonyeshwa kwenye ndoto tu!
Ni afadhari akawa ana hisia tu lakini sio ajue.

Aisha akajibu " ina maana huna malengo kabisa na Mimi
Ko una mpango wa kunichezea tu?

"Kwani ulitaka nini ziada kutoka kwangu?jamaa akamuuliza.
Nataka unizalie watoto namimi nataka ndoa hata mke wa pili

Haa eti nini!?kama ni hivyo tuishie hapa ,dini yetu hairuhusu kawatafute wakina mzee Yusufu sihitaji stress ndio maana nimekwambia mapema misimamo yangu kama utaiweza,huiwezi tuishie hapa....

Haya nimekuelewa ntafuata huu utaratibu kwasababu nakupenda.alijibu dada.....poa una amani lakini?aliuliza jamaa
Yes usijari......

Naomba ninapokuwa nyumbani usinitext wala nisiione call yako ni mpaka iwe ninapokuwa kazini tu.....

He sasa si uweke password kama hutaki mkeo asione simu yako?
Hapana sitaki kuonekana kutokuaminiwa na wife...na usichati na Mimi kwa msg za kawaida au Whatsap wala messenger,tutumiane email tu.

Aisha akajibu "sawa"

Uhusiano wao uliendelea lakini Aisha hakuwahi kuwa na amani kwa mapenzi yenye mashart kama yale ,ilikuwa inamuuma akikumbuka maneno ya jamaa na vile anavyo mheshimu mkewe na si yeye.....alivumilia tu kwakuwa jamaa ana hela,chochote alichotaka alipewa.

Alitumia kila mbinu ili kumvutia jamaa,alijaribu kumuuliza kitu anachokipenda huyo buana ili amfanyie mfano chakula anachopenda,lakini jamaa hakuwa muwazi Sana kwake.

Alitamani sana kumjua huyo mke wa jamaa lakini hakuweza
Alijaribu kutafuta hakufanikiwa,ila mara kadhaa alimskia jamaa akiongea nae kwenye simu anamuita Magdalena.....au mama Francisco.

Siku moja akiwa saluni kwake aliyofunguliwa na jamaa akiwa na msichana wake wa kazi
Akaanza kupitia Facebook akaingia kwenye profile ya jamaa aone marafiki zake ,

Akasearch jina la Magdalene akalipata,akafungua profile yake akakuta ni kweli ni mkewe jamaa,kwanza alimuweka mumewe Picha yake ya wasifu.

Akamuomba urafiki,muda huo huo mag akaacept......akamshukuru kwa kumkubalia urafiki mag akamwambia "karibu my"
Akajibu asante....

Wakachat sana siku ile.....huyu Aisha akajisemesha "nimemmaliza tayari.....usiku ule hakulala usingizi akimtafakari yule mwanamke....amfanyie nini maana ndio kikwazo kikubwa chake.

Kulipokucha mchana akiwa nyumbani kwake akamtext msichana wake
" nimeongea na huyu mshamba nimemkaribisha saluni nimemwambia tunampa ofa aje,sasa naomba akija hapo wewe endelea kumfumua hizo nywere zake Mimi nitamnunulia soda ntamuwekea na pilipili atajuta kunifahamu"!

Dada pilipili!!?aliuliza huyo binti
Wewe nawe baki na hilo ilo ,namaanisha sumu!alijibu Aisha
Anhaà hapo sawa,ko nisimuwahishe niende nae taratibu?

No wewe Fanya kawaida Mimi dakika chache ntakuwa hapo...alijibu aisha

Mag dakika 20 akawa amefika na gari yake
Akamjulisha Aisha akampa maelekezo msichana wake akawa amemwona akampokea.....wakaanza kazi

Dakika 10 mbele Aisha akawa amefika ,story zikaendelea
Magdalene hamjui Aisha, Aisha anamjua Magdalena.

Baada ya kumsuka nywere akiwa karibu na kumaliza Aisha akamwambia ngoja nikununulie na soda japo ukanywe hata nyumbani,soda gani vile?

"Yoyote nichukulie my dear nashkur sana"alijibu mag

Aisha akazuga kama anaenda dukani lkn alikuwa kazunguka nyuma ya saluni yake akatoa chupa ya take away kwenye pochi yake, na akapita dukani akaagiza zingine mbili za kwao na binti yake.

Akampa Magdalena soda aina ya pepsi,akashukuru akawasha gari akaondoka.....akionyesha kufurahishwa na Huduma zao na upendo au ukarimu wao asijue mtego wa muwindaji.

Huku nyuma walianza kupongezana wakiamini zoezi lao limefanikiwa walijua kwa vyovyote vile angekunywa njiani
Na iwapo angekunywa tu asingefika mbali kutokana na ujazo wa paketi aliyomimina kwenye chupa......

"sikutaka kumpa mapema halafu afie hapa sitaki mizoga ya watu hapa akafie mbele huko pumbavu kabisa" alijisemesha Aisha.

Kumbe Magdalena ile soda hakunywa kwenye gari.

Akawa amefika nayo mpka home.....

na kwasababu ilikuwa imepoa akaingia nayo ndani akaiweka kwenye friji akazichanganya na zingine.

Ikawa imelala kwenye friji.

Mchana wa kesho yake jamaa akarudi nyumbani kula chakula
Alipokuwa anaondoka kurudi ofisini,akamwomba mkewe ampe soda,na soda yake kubwa ni pepsi akampa ile ya kina Aisha pasipo kujua .

Patamu hapo......

Akiwa anaondoka akaona kuna email imeingia ,kucheki anakutana na text ya Aisha "uko wapi my?"

Natoka nyumbani naenda ofisini, OK basi nipitie saluni Nina shida kidogo..........

Anataka amuulize maendeleo ya familia yake ,ana wasiwasi je soda ilinyweka?au ile sio sumu kadanganywa?

Jamaa alipofika Aisha akaingia kwenye gari akamkiss jamaa
Wakaondoka wote kuelekea ofisini kwa jamaa.

Aisha akalalamika njaa ikabidi ampitishe mahali akala akamsubiri.
walipokuwa wakiondoka akiwa kwenye gari akaona soda akamwomba anywe,jamaa bila ajizi yoyote akampa....kumbe ni ile yenye pilipili!

Na kwakuwa alikuwa kakaukiwa akaanza nayo hapo hapo!
akakata kama nusu hivi

Huku wakipiga story........

Dakika tano peke zilikuwa ni nyingi akaanza kuskia maumivu makali hamna mfano,moja kwa moja akajua ni ile soda.....ha! Akajishika tumbo akatoa macho akamuuliza "hii umeitoa wapi?jamaa akajibu" nyumbani kwenye friji langu"

Ooooooh my god mkeo ameniua jamani! Mkeo ameniua niwahishe hospital plz!

Mke wangu amekuua?
kivipi hebu niambie!!!

Dah!Kweli mkeo anasali.......
Aisha anaongea huku akilia kwa uchungu mkubwa akatamka neno la mwisho akasema
"Nakufa kwa upumbavu wangu mwenyewe, niwahishe hospital labda ntapona mimi!

Jamaa dakika 15 akawa amefanikiwa kufika hospital akaingia nae ,jopo la madaktari wakiwa wanamhangaikia yeye akawa amewasha gari akatoroka kukwepa msala.......huku nyuma Aisha ikawa ndio kwa heri bye bye!

Kuchunguzwa ikaonekana amekufa kwa kula chakula au kinywaji chenye sumu.

Kumtafuta aliyemleta hospital wakashangaa hawamwoni.na bahati nzuri simu ya marehemu akawa ameondoka nayo.

Taarifa ikafika police.

Na ilipotangazwa iwapo angetokea ndugu wa marehemu ,wa kwanza akawa ni binti wa saluni.

Police ilibidi waanze nae yeye kuchunguza simu yake,Bahati nzuri au mbaya kwake,zile Meseji walizochati na dada hakuzifuta.........

binti akawa ni mtuhumiwa namba moja ilionekana kuna MTU walimpa sumu na marehemu lakini ninani?na mbona Aisha ndiyo amekufa tena?wakaenda kuirenew ile line ya marehemu.

Upelelezi ulipokuwa ukiendelea tayari yule binti akabanwa mpaka akakiri kuhusu mpango waliousuka na marehemu dhidi ya mke wa jamaa aitwaye japhert..... Walipomtafuta akaja japhert pamoja na mkewe.

Magdalena akahojiwa kama anamfahamu Aisha akaeleza vile walivyojuana kupitia Facebook kama wiki tatu tu.

Akaeleza vile walivyompa na ofa ya kwenda kusuka na
"huyu binti ndiye aliyenisuka na wakaninunulia soda" lakini ile soda sikuinywa nikaenda nayo nyumbani.....................akasimulia kama hapo juu.

Mume akawa anashangaa anaona ni kama move baadae mahakama ikamtia hatiani yule binti.

Walipofika nyumbani Magdalena ilibidi ambane mumewe

"Vipi Mume wangu marehemu kumbe alikuwa hawara wako?"
Ilibidi mumewe awe muwazi tu kwake,akamweleza Kisa kizima
huku akilia kwa uchungu mkubwa.......

Ni kweli Mimi ndio nilitaka kukuua kwa upumbavu wangu,naomba unisamehe,sijui kwanini wanaume haturidhiki na hatutosheki?hakuna chochote ninachokikosa kwako lakini tamaa tu!

Usimwache Mungu unayemtumikia mke wangu,ningefanyaje Mimi kukupoteza wewe!?

ningefanyaje na watoto hawa?
Mama akamfuata mkewe akamkumbatia miguu huku akilia
Jamaa akawa ameishiwa maneno ya kuongea zaidi ya "nisamehe".......wakaangua kilio cha kumshukuru Mungu.

Mwishoni mama Francisco akiwa amemkumbatia mmewe,anasema mwili wote ulikuwa kama unachemka,akasema nyamaza nimshukuru Mungu:

"EEH MWENYEZI MUNGU,BABA WA REHEMA,MUNGU UTULINDAYE,
BIBLIA IMESEMA WEWE USIPOULINDA MJI WAULINDAO WAKESHA BURE.......

USIPOILINDA NDOA,HATUWEZI KUFANYA CHOCHOTE.......

ASANTE KWA UAMINIFU WAKO KWANGU,
ULINIAHIDI IWAPO NIGEKUWA MWAMINIFU KWAKO,USINGENIACHA WALA KUNIPUNGUKIA HATA SEKUNDE TANO!

NA KWAMBA MAADUI ZANGU WANGEKUWA ADUI ZAKO.
NA UMESHATIKIZA AHADI YAKO KWANGU.

ASANTE KWA KUHAKIKISHA NAZIDI KUWA SALAMA.
UMETULINDA MIMI NA MUME WANGU NA WATOTO.

ILE SODA PAMOJA NA KWAMBA IMEINGIA MPAKA NDANI KWANGU,LAKINI HAKUNA ALIYEKUNYWA NAJUA NI UWEZA WAKO LAKINI HATA MMOJA WETU ANGEKUNYWA ASINGEDHURIKA MAANA UMESEMA " TUKILA VYA KUFISHA HAVITATUDHURU............TULINDE TUTUNZE ZAIDI KWA UTUKUFU WA JINA LAKO AMENI.

Baba Francisco yupo ametulia na mkewe sasa hivi na ameshika sana mambo ya imani,anasali balaa.

Anajuta kwanini alijiingiza kwenye matatizo eti kwasababu ya hawara.......hataki kabisa kuisikia michepuko.

Nasema hivi tenda wema UTAVUNA mema
Ukitenda kwa hila UTAVUNA hila.
 
Kabla mahusiano yao hayajakolea
jamaa akamkalisha chini huyu mdada na kumpa misimamo yake.

"Mpaka tumekuwa kwenye mahusiano maana yake nimekupenda
Nilikwambia tangu awali nina mke na watoto.
Nampenda mke wangu ndio maana nilifunga nae ndoa.....

Sitamani hata siku moja aje kuumia eti kwasababu yako

Sina malengo yoyote na wewe hususani ya kindoa maana tayari niko na ndoa.....nakuheshimu pia kwa nafasi yako lakini kuwa na nidhamu kwenye ndoa yangu......kukupenda wewe haina maana kwamba mke wangu simpendi no,ni udhaifu wa wanaume tulionao

Sitaki uwasiliane na mke wangu hata mara moja
Sitaki ajue nina hawara nje,mke wangu anasali anamuomba Mungu.

Hata mahusiano yetu najua ataonyeshwa kwenye ndoto tu!
Ni afadhari akawa ana hisia tu lakini sio ajue.

Aisha akajibu " ina maana huna malengo kabisa na Mimi
Ko una mpango wa kunichezea tu?

"Kwani ulitaka nini ziada kutoka kwangu?jamaa akamuuliza.
Nataka unizalie watoto namimi nataka ndoa hata mke wa pili

Haa eti nini!?kama ni hivyo tuishie hapa ,dini yetu hairuhusu kawatafute wakina mzee Yusufu sihitaji stress ndio maana nimekwambia mapema misimamo yangu kama utaiweza,huiwezi tuishie hapa....

Haya nimekuelewa ntafuata huu utaratibu kwasababu nakupenda.alijibu dada.....poa una amani lakini?aliuliza jamaa
Yes usijari......

Naomba ninapokuwa nyumbani usinitext wala nisiione call yako ni mpaka iwe ninapokuwa kazini tu.....

He sasa si uweke password kama hutaki mkeo asione simu yako?
Hapana sitaki kuonekana kutokuaminiwa na wife...na usichati na Mimi kwa msg za kawaida au Whatsap wala messenger,tutumiane email tu.

Aisha akajibu "sawa"

Uhusiano wao uliendelea lakini Aisha hakuwahi kuwa na amani kwa mapenzi yenye mashart kama yale ,ilikuwa inamuuma akikumbuka maneno ya jamaa na vile anavyo mheshimu mkewe na si yeye.....alivumilia tu kwakuwa jamaa ana hela,chochote alichotaka alipewa.

Alitumia kila mbinu ili kumvutia jamaa,alijaribu kumuuliza kitu anachokipenda huyo buana ili amfanyie mfano chakula anachopenda,lakini jamaa hakuwa muwazi Sana kwake.

Alitamani sana kumjua huyo mke wa jamaa lakini hakuweza
Alijaribu kutafuta hakufanikiwa,ila mara kadhaa alimskia jamaa akiongea nae kwenye simu anamuita Magdalena.....au mama Francisco.

Siku moja akiwa saluni kwake aliyofunguliwa na jamaa akiwa na msichana wake wa kazi
Akaanza kupitia Facebook akaingia kwenye profile ya jamaa aone marafiki zake ,

Akasearch jina la Magdalene akalipata,akafungua profile yake akakuta ni kweli ni mkewe jamaa,kwanza alimuweka mumewe Picha yake ya wasifu.

Akamuomba urafiki,muda huo huo mag akaacept......akamshukuru kwa kumkubalia urafiki mag akamwambia "karibu my"
Akajibu asante....

Wakachat sana siku ile.....huyu Aisha akajisemesha "nimemmaliza tayari.....usiku ule hakulala usingizi akimtafakari yule mwanamke....amfanyie nini maana ndio kikwazo kikubwa chake.

Kulipokucha mchana akiwa nyumbani kwake akamtext msichana wake
" nimeongea na huyu mshamba nimemkaribisha saluni nimemwambia tunampa ofa aje,sasa naomba akija hapo wewe endelea kumfumua hizo nywere zake Mimi nitamnunulia soda ntamuwekea na pilipili atajuta kunifahamu"!

Dada pilipili!!?aliuliza huyo binti
Wewe nawe baki na hilo ilo ,namaanisha sumu!alijibu Aisha
Anhaà hapo sawa,ko nisimuwahishe niende nae taratibu?

No wewe Fanya kawaida Mimi dakika chache ntakuwa hapo...alijibu aisha

Mag dakika 20 akawa amefika na gari yake
Akamjulisha Aisha akampa maelekezo msichana wake akawa amemwona akampokea.....wakaanza kazi

Dakika 10 mbele Aisha akawa amefika ,story zikaendelea
Magdalene hamjui Aisha, Aisha anamjua Magdalena.

Baada ya kumsuka nywere akiwa karibu na kumaliza Aisha akamwambia ngoja nikununulie na soda japo ukanywe hata nyumbani,soda gani vile?

"Yoyote nichukulie my dear nashkur sana"alijibu mag

Aisha akazuga kama anaenda dukani lkn alikuwa kazunguka nyuma ya saluni yake akatoa chupa ya take away kwenye pochi yake, na akapita dukani akaagiza zingine mbili za kwao na binti yake.

Akampa Magdalena soda aina ya pepsi,akashukuru akawasha gari akaondoka.....akionyesha kufurahishwa na Huduma zao na upendo au ukarimu wao asijue mtego wa muwindaji.

Huku nyuma walianza kupongezana wakiamini zoezi lao limefanikiwa walijua kwa vyovyote vile angekunywa njiani
Na iwapo angekunywa tu asingefika mbali kutokana na ujazo wa paketi aliyomimina kwenye chupa......

"sikutaka kumpa mapema halafu afie hapa sitaki mizoga ya watu hapa akafie mbele huko pumbavu kabisa" alijisemesha Aisha.

Kumbe Magdalena ile soda hakunywa kwenye gari.

Akawa amefika nayo mpka home.....

na kwasababu ilikuwa imepoa akaingia nayo ndani akaiweka kwenye friji akazichanganya na zingine.

Ikawa imelala kwenye friji.

Mchana wa kesho yake jamaa akarudi nyumbani kula chakula
Alipokuwa anaondoka kurudi ofisini,akamwomba mkewe ampe soda,na soda yake kubwa ni pepsi akampa ile ya kina Aisha pasipo kujua .

Patamu hapo......

Akiwa anaondoka akaona kuna email imeingia ,kucheki anakutana na text ya Aisha "uko wapi my?"

Natoka nyumbani naenda ofisini, OK basi nipitie saluni Nina shida kidogo..........

Anataka amuulize maendeleo ya familia yake ,ana wasiwasi je soda ilinyweka?au ile sio sumu kadanganywa?

Jamaa alipofika Aisha akaingia kwenye gari akamkiss jamaa
Wakaondoka wote kuelekea ofisini kwa jamaa.

Aisha akalalamika njaa ikabidi ampitishe mahali akala akamsubiri.
walipokuwa wakiondoka akiwa kwenye gari akaona soda akamwomba anywe,jamaa bila ajizi yoyote akampa....kumbe ni ile yenye pilipili!

Na kwakuwa alikuwa kakaukiwa akaanza nayo hapo hapo!
akakata kama nusu hivi

Huku wakipiga story........

Dakika tano peke zilikuwa ni nyingi akaanza kuskia maumivu makali hamna mfano,moja kwa moja akajua ni ile soda.....ha! Akajishika tumbo akatoa macho akamuuliza "hii umeitoa wapi?jamaa akajibu" nyumbani kwenye friji langu"

Ooooooh my god mkeo ameniua jamani! Mkeo ameniua niwahishe hospital plz!

Mke wangu amekuua?
kivipi hebu niambie!!!

Dah!Kweli mkeo anasali.......
Aisha anaongea huku akilia kwa uchungu mkubwa akatamka neno la mwisho akasema
"Nakufa kwa upumbavu wangu mwenyewe, niwahishe hospital labda ntapona mimi!

Jamaa dakika 15 akawa amefanikiwa kufika hospital akaingia nae ,jopo la madaktari wakiwa wanamhangaikia yeye akawa amewasha gari akatoroka kukwepa msala.......huku nyuma Aisha ikawa ndio kwa heri bye bye!

Kuchunguzwa ikaonekana amekufa kwa kula chakula au kinywaji chenye sumu.

Kumtafuta aliyemleta hospital wakashangaa hawamwoni.na bahati nzuri simu ya marehemu akawa ameondoka nayo.

Taarifa ikafika police.

Na ilipotangazwa iwapo angetokea ndugu wa marehemu ,wa kwanza akawa ni binti wa saluni.

Police ilibidi waanze nae yeye kuchunguza simu yake,Bahati nzuri au mbaya kwake,zile Meseji walizochati na dada hakuzifuta.........

binti akawa ni mtuhumiwa namba moja ilionekana kuna MTU walimpa sumu na marehemu lakini ninani?na mbona Aisha ndiyo amekufa tena?wakaenda kuirenew ile line ya marehemu.

Upelelezi ulipokuwa ukiendelea tayari yule binti akabanwa mpaka akakiri kuhusu mpango waliousuka na marehemu dhidi ya mke wa jamaa aitwaye japhert..... Walipomtafuta akaja japhert pamoja na mkewe.

Magdalena akahojiwa kama anamfahamu Aisha akaeleza vile walivyojuana kupitia Facebook kama wiki tatu tu.

Akaeleza vile walivyompa na ofa ya kwenda kusuka na
"huyu binti ndiye aliyenisuka na wakaninunulia soda" lakini ile soda sikuinywa nikaenda nayo nyumbani.....................akasimulia kama hapo juu.

Mume akawa anashangaa anaona ni kama move baadae mahakama ikamtia hatiani yule binti.

Walipofika nyumbani Magdalena ilibidi ambane mumewe

"Vipi Mume wangu marehemu kumbe alikuwa hawara wako?"
Ilibidi mumewe awe muwazi tu kwake,akamweleza Kisa kizima
huku akilia kwa uchungu mkubwa.......

Ni kweli Mimi ndio nilitaka kukuua kwa upumbavu wangu,naomba unisamehe,sijui kwanini wanaume haturidhiki na hatutosheki?hakuna chochote ninachokikosa kwako lakini tamaa tu!

Usimwache Mungu unayemtumikia mke wangu,ningefanyaje Mimi kukupoteza wewe!?

ningefanyaje na watoto hawa?
Mama akamfuata mkewe akamkumbatia miguu huku akilia
Jamaa akawa ameishiwa maneno ya kuongea zaidi ya "nisamehe".......wakaangua kilio cha kumshukuru Mungu.

Mwishoni mama Francisco akiwa amemkumbatia mmewe,anasema mwili wote ulikuwa kama unachemka,akasema nyamaza nimshukuru Mungu:

"EEH MWENYEZI MUNGU,BABA WA REHEMA,MUNGU UTULINDAYE,
BIBLIA IMESEMA WEWE USIPOULINDA MJI WAULINDAO WAKESHA BURE.......

USIPOILINDA NDOA,HATUWEZI KUFANYA CHOCHOTE.......

ASANTE KWA UAMINIFU WAKO KWANGU,
ULINIAHIDI IWAPO NIGEKUWA MWAMINIFU KWAKO,USINGENIACHA WALA KUNIPUNGUKIA HATA SEKUNDE TANO!

NA KWAMBA MAADUI ZANGU WANGEKUWA ADUI ZAKO.
NA UMESHATIKIZA AHADI YAKO KWANGU.

ASANTE KWA KUHAKIKISHA NAZIDI KUWA SALAMA.
UMETULINDA MIMI NA MUME WANGU NA WATOTO.

ILE SODA PAMOJA NA KWAMBA IMEINGIA MPAKA NDANI KWANGU,LAKINI HAKUNA ALIYEKUNYWA NAJUA NI UWEZA WAKO LAKINI HATA MMOJA WETU ANGEKUNYWA ASINGEDHURIKA MAANA UMESEMA " TUKILA VYA KUFISHA HAVITATUDHURU............TULINDE TUTUNZE ZAIDI KWA UTUKUFU WA JINA LAKO AMENI.

Baba Francisco yupo ametulia na mkewe sasa hivi na ameshika sana mambo ya imani,anasali balaa.

Anajuta kwanini alijiingiza kwenye matatizo eti kwasababu ya hawara.......hataki kabisa kuisikia michepuko.

Nasema hivi tenda wema UTAVUNA mema
Ukitenda kwa hila UTAVUNA hila.
Sante mkuu
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom