Funguka: Maisha yamekufunza nini?

Gorgeousmimi

JF-Expert Member
Jun 21, 2010
9,296
7,666
Ningeweza kuongelea kuhusu mimi lakini nisiwe mbinafsi kila mtu ana maisha yaliyoyapitia yawe ya mteremko au magumu,lakini kuna dhana na njia alizotumia kutatua matatizo yake.

Nimejifunza katika maisha yangu kwamba nothing comes for free in life.

Ukitaka maisha mazuri lazima upiganie kuyatafuta,uweke nia na malengo na uyafanyie kazi,usisubirie muujiza ukushukie,tumia hekima, akili na busara ulizozaliwa nazo kujijenga maisha yako ya baadae.

Ukipigana kutafuta mafaniko,hakika utayaona matunda yake."NO SWEETS WITHOUT SWEAT" Usivunjike moyo ukianguka,inuka na usonge mbele,fanya juhudi zaidi.

Sikuwa na maisha rahisi katika malezi yangu,lakini nimeridhika na maisha nilonayo sasa,hayajakamilika na hayapo kama ninavyoombea lakini nimetimiza malengo yangu mengi ya muhimu kwangu kwa maisha ya sasa na ya baadae na kwa hilo napaswa kusema alhamdulillah.

Ewe mwenzangu maisha haya yamekufundisha nini,chochote kile funguka!!

Karibuni wapendwa!
 
in life ni kuwa humble tu....kuna watu they think wao ni 'center of the universe'..kila kitu kianzie na wao...kumbe you are just one among 7 billion people...don't take yourself so serious....life is too short...
 
Nimejifunza:

1. "You can't be my friend unless i know your weaknesses" When you turn rogue i know where exactly to deal with you.

2. Financial Freedom ni muhimu sana, sio kuishi kwa ajira.

3. Being Optimist and Opportunist.

4. Exploit your talents, tumia kama chanzo cha mapato.

5. Do what makes you happy always.
 
Nimejifunza kutokata tamaa na kuwa risk taker...

Nilianza maisha from zero point na kila aliyenifahamu miaka 10 iliyopita hawezi kuamini hatua niliyopiga mpaka sasa kwa usimamizi wangu pekeyangu. Nimepita katika vizingiti kana kwamba mpaka mama yangu mzazi akanambia "mwanangu acha hiko ufanyacho kimeshindikana" lakini niligangamara kwa lazima mpaka kikanitoa. Na hiki sio kingine bali ni shule... Jamani elimu inalipa aisee.... "Kama elimu ni ghali, jaribu ujinga"

Cha muhimu ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kumuomba kwa sana hakika hatakutupa. Hii ni kwa wanaoamini uwepo wake...
 
Mmeongea mengi wadau na ya kweli sana tu!!!!!!
Naongeza kidogo kwa Mkoroshokigoli hapo kwenye social capital!!!!

Pamoja na uzuri wa social capital ni muhimu sana kujua nani ni nani kwa wakati upi sababu wanaotuangusha mara nyingine hutokea humo humo kati ya wanaotujua,tahadhari sana na watu awe business partner or competitor, supervisor kazini au immediate boss spare your "core" kuna watu wakikujua sana taratibu wanajigeuza "enemies from within" kama sio wao basi watatuma wengine kukuhujumu....kikulacho style!!!!!!!!!

The Boss you just did it!!!!!!!!!

Kufanikiwa na kufeli asilimia kubwa kunasababishwa na mtu mwenyewe wengine huchangia tu!!!!!
Unapoamua kuzaa au kujenga familia basi jua umechukua dhamana za maisha ya wengine ni LAZIMA uhakikishe ustawi ,furaha,amani,usalama na faraja miongoni mwao nasema ni LAZIMA!!!!!

Wazazi jamani ndugu zanguni tutunze ,tuheshimu na kunyenyekea wazazi wetu hamna jinsi ya maneno ya kutosha hapa ila hakikisha wazazi wako hawajuti kukupata wewe,hawasikitikii matendo yako,hawasononekii uwepo wako hata kama huna cha kuwapa basi TUSIWAKERE WAZAZI WETU!!!!!!

IMANI YAKO NI SEHEMU KUBWA YA MAISHA YAKO
 
Last edited by a moderator:
When life throw you a burger, eat it! Yaani hakuna lisilowezekana. Look around you and there is a million opportunities, ukienda hatua kwa hatua.

above all, there is a God somewhere, but stop mesmerizing about the God all day(kwa ajili ya wale wanaoshinda nyumba za ibada kutwa kumuomba Mungu awaondolee umaskini). Work! Treat everyone with respect and choose your battles wisely.

you are never defeated until you give up.
 
Life offers a lot of ways to learn everyday...najifunza mengi sanaaa,kwa uchache tu...
1.I can make the life i want to have,the key is praying,working hard(no shortcuts yani) and overcoming fear
2.simple things in life give us most hapiness and its not about how our end will be ,what matters is how you live along through good and bad times,
3.i have learnt how to choose happiness most of the time and do what i want to do
,i hardly have regrets
4.to do and give the best in everything,it satisfies me most of the time
5.and of course to keep most things in balance,being neither too much nor too less
 
nmejifunza1. kuwa mtumishi serikalini ni hamna stress kuliko kuwa kwenye private institutes 2.leo haifanani na kesho wala kesho kutwa au jana.3,ukiona uko na wakati mgumu sana jua mambo mazuri yatabisha hodi soon 4.hata iweje mke wako ni rafiki tu sio ndugu yako 5.vijana wengi hawapendi kazi ngumu yaani hawajitumi.
 
There is no easy money rafiki, namba 1 na namba 5 zinakinzana! Huwezi kupata mali za kutosha kama haujistress kuzipata. Serikali tu ndo kuna miujiza, mtu analipwa mshahara milioni moja na anajenga jumba hataree, anaendesha gari la maana na watoto wanaenda shule nzuri. Lazma uwe MWIZI!

jiongeze.
nmejifunza1. kuwa mtumishi serikalini ni hamna stress kuliko kuwa kwenye private institutes 2.leo haifanani na kesho wala kesho kutwa au jana.3,ukiona uko na wakati mgumu sana jua mambo mazuri yatabisha hodi soon 4.hata iweje mke wako ni rafiki tu sio ndugu yako 5.vijana wengi hawapendi kazi ngumu yaani hawajitumi.
 
Back
Top Bottom