Muda unakwenda kwa kasi sana. Tutashuhudia mengi pia.
Kwa muda wa miaka 4 na ushei, kuna mambo ambayo hayasemwi hadharani ndani ya CCM hasa Zanzibar. Kwa ufupi wa maneno CCM Zanzibar wana fundo rohoni, wamehifadhi mengi kuhusu mwenendo wa chama chini ya ndugu Mwenyekiti Magufuli.
Hicho kinachoendelea kuhusu kugombea ni salamu kwa Mwenyekiti.
Tunazo taarifa zisizo shaka kwamba baadhi ya CCM, Zanzibar hawakubaliani na Mwenendo wa Maamuzi anayoyafanya Mwenyekiti wao na hawaridhishwi na tabia ya kutotabirika kwa Mwenyekiti jambo ambalo linahatarisha maslahi yao.
UZOEFU WA CCM ZANZIBAR KUELEKEA CHAGUZI
CCM Zanzibar wamezidi deko na wamezoea kuwa na makundi sana unapofika wakati wa mabadiliko ya Rais mpya kutoka CCM. Kule wana CCM wako kimaslahi kwa kuegemea zaidi timu na si utendaji. Timu hupangwa kwa minajili ya watu kugawiwa vyeo baada ya ushindi . Tokea aingie madarakani Rais Magufuli mianya mingi na vichochoro vya ulaji wa kujuana ndani ya chama vimezibwa.
Lakini ndani ya serikali ya Dr shein kuna kundi la walaji wengi. Zipo taarifa pia Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM haridhishwi na mambo yanavyokwenda kwenye utendaji wa Serikali ya Zanzibar na kwamba haiendani na falsafa zake. Kule ni kubwagia tu bila kikomo, ufisadi, kujuana na kulindana.
Zipo taarifa pia si mara moja kumekuwa na ukinzani kuhusu baadhi ya mawaziri wa Zanzibar kupendekezwa kutumbuliwa ili kukisafisha chama lakini kumekuwa na ugumu wa kuchukuliwa hatua. Mazoea ndio kikwazo kwa CCM Zanzibar
MWENYEKITI ATAWEZA KUKATA MZIZI WA FITINA 2020?
Picha iko wazi, Rais wa Zanzibar huchaguliwa bara Dodoma bila ya ridhaa ya CCM Zanzibar. Kilichopo ni Timu baina ya walaji, wenye mazoea dhidi ya uchapa kazi na utendaji. Timu ya Uchapakazi ina maono ya Mwenyekiti na Timu ya mazoea, na walaji iko chini ya wahafidhina.
Itoshe kuwaeleza tu kwamba utitiri wa wagombea urais CCM Zanzibar 2020 ni vita ya pande mbili hizo. Pale kuna wana mikakati wameelekezwa kuchukuwa fomu kwa hesabu. Mwisho kuna makundi hayo mawili.
Ijulikane kwamba wahafidhina wana mtu wao na timu ya kazi ina mtu wake, hao wengine ni wapambe tu na wana mikakati ambao watatumika kudhoofisha upande mwengine muda ukifika.
Bahati mbaya CCM hawajadili mtu anayeweza kuleta ushindi Zanzibar na anayekubalika na wazanzibari , hilo sio tatizo kwao, wao mtu wao akishapitishwa tu Dodoma basi kazi imeisha. Kinachoangaliwa ni maslahi.
Tunazo taarifa pia katika hili kwamba mikakati imepangwa vyema na mwisho wa siku turufu inakwenda upande wa mwenyekiti ambaye ndie Amiri Jeshi Mkuu anayehusika na dhamana ya kuhakikisha anasimamia kupatikana rais anayetakiwa Zanzibar na mfumo na sio aliye chaguo la wazanzibari walio wengi.
Ikumbukwe pia Mwenyekiti wa CCM amepewa nguvu nyingi ndani ya chama na serikali za kumuhakikishia kufikia malengo yake. Kitendawili kinabaki jee mara hii Mwenyekiti atakata mzizi wa fitina? maana mfumo ulishamuandaa mtu mwengine ambaye kwa taarifa zilizopo sio chaguo la MWENYEKITI.
SALAMU KWA MWENYEKITI NA TIMU YAKE
Kwanza wagombea kupitia timu zao wamepuuza kabisa dhana ya kukigawa chama kwa kjitokeza wagombea lukuki bila kuzingatia maelekezo.
Hao waliochukuwa fomu kila mmoja ana lengo lake katika makundi haya.
1. Kuna wahafidhina ambao hukitikisa chama ili wakumbukwe kwenye teuzi hapo baadae
2. Kuna watu wa mikakati kudhoofisha wengine wasiotakiwa (system oriented)
3. Kuna wapambe mahususi na wasindikizaji wa mteuliwa rasmi. (timu ya mteuliwa na marafiki zake)
Kupitia wagombea hao waliochukuwa fomu utawapata wote kwenye makundi haya ambao wanatokana na yale makundi mawili makuu niliyoyataja hapo juu.
Tatizo kwa Zanzibar ni kwamba lazima CCM itajeruhiwa na makundi haya na kuwafaidisha wapinzani. Mara zote ulaji na mazoea huiathiri CCM kwa namna moja au nyengine.
Wadadisi wa mambo mara hii wamefika mbali. Zipo tetesi kuwa WAHAFIDHINA WA CCM ZANZIBAR WANAUNGWA MKONO NA TIMU MOJA KUBWA UPANDE WA BARA ambao nao haukubaliani na Mwenyekiti namna anavyokiendesha chama na serikali.
Fumbo bado linabaki jee Mwenyekiti ataweza? Muda utasema.
Kishada.
Kwa muda wa miaka 4 na ushei, kuna mambo ambayo hayasemwi hadharani ndani ya CCM hasa Zanzibar. Kwa ufupi wa maneno CCM Zanzibar wana fundo rohoni, wamehifadhi mengi kuhusu mwenendo wa chama chini ya ndugu Mwenyekiti Magufuli.
Hicho kinachoendelea kuhusu kugombea ni salamu kwa Mwenyekiti.
Tunazo taarifa zisizo shaka kwamba baadhi ya CCM, Zanzibar hawakubaliani na Mwenendo wa Maamuzi anayoyafanya Mwenyekiti wao na hawaridhishwi na tabia ya kutotabirika kwa Mwenyekiti jambo ambalo linahatarisha maslahi yao.
UZOEFU WA CCM ZANZIBAR KUELEKEA CHAGUZI
CCM Zanzibar wamezidi deko na wamezoea kuwa na makundi sana unapofika wakati wa mabadiliko ya Rais mpya kutoka CCM. Kule wana CCM wako kimaslahi kwa kuegemea zaidi timu na si utendaji. Timu hupangwa kwa minajili ya watu kugawiwa vyeo baada ya ushindi . Tokea aingie madarakani Rais Magufuli mianya mingi na vichochoro vya ulaji wa kujuana ndani ya chama vimezibwa.
Lakini ndani ya serikali ya Dr shein kuna kundi la walaji wengi. Zipo taarifa pia Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM haridhishwi na mambo yanavyokwenda kwenye utendaji wa Serikali ya Zanzibar na kwamba haiendani na falsafa zake. Kule ni kubwagia tu bila kikomo, ufisadi, kujuana na kulindana.
Zipo taarifa pia si mara moja kumekuwa na ukinzani kuhusu baadhi ya mawaziri wa Zanzibar kupendekezwa kutumbuliwa ili kukisafisha chama lakini kumekuwa na ugumu wa kuchukuliwa hatua. Mazoea ndio kikwazo kwa CCM Zanzibar
MWENYEKITI ATAWEZA KUKATA MZIZI WA FITINA 2020?
Picha iko wazi, Rais wa Zanzibar huchaguliwa bara Dodoma bila ya ridhaa ya CCM Zanzibar. Kilichopo ni Timu baina ya walaji, wenye mazoea dhidi ya uchapa kazi na utendaji. Timu ya Uchapakazi ina maono ya Mwenyekiti na Timu ya mazoea, na walaji iko chini ya wahafidhina.
Itoshe kuwaeleza tu kwamba utitiri wa wagombea urais CCM Zanzibar 2020 ni vita ya pande mbili hizo. Pale kuna wana mikakati wameelekezwa kuchukuwa fomu kwa hesabu. Mwisho kuna makundi hayo mawili.
Ijulikane kwamba wahafidhina wana mtu wao na timu ya kazi ina mtu wake, hao wengine ni wapambe tu na wana mikakati ambao watatumika kudhoofisha upande mwengine muda ukifika.
Bahati mbaya CCM hawajadili mtu anayeweza kuleta ushindi Zanzibar na anayekubalika na wazanzibari , hilo sio tatizo kwao, wao mtu wao akishapitishwa tu Dodoma basi kazi imeisha. Kinachoangaliwa ni maslahi.
Tunazo taarifa pia katika hili kwamba mikakati imepangwa vyema na mwisho wa siku turufu inakwenda upande wa mwenyekiti ambaye ndie Amiri Jeshi Mkuu anayehusika na dhamana ya kuhakikisha anasimamia kupatikana rais anayetakiwa Zanzibar na mfumo na sio aliye chaguo la wazanzibari walio wengi.
Ikumbukwe pia Mwenyekiti wa CCM amepewa nguvu nyingi ndani ya chama na serikali za kumuhakikishia kufikia malengo yake. Kitendawili kinabaki jee mara hii Mwenyekiti atakata mzizi wa fitina? maana mfumo ulishamuandaa mtu mwengine ambaye kwa taarifa zilizopo sio chaguo la MWENYEKITI.
SALAMU KWA MWENYEKITI NA TIMU YAKE
Kwanza wagombea kupitia timu zao wamepuuza kabisa dhana ya kukigawa chama kwa kjitokeza wagombea lukuki bila kuzingatia maelekezo.
Hao waliochukuwa fomu kila mmoja ana lengo lake katika makundi haya.
1. Kuna wahafidhina ambao hukitikisa chama ili wakumbukwe kwenye teuzi hapo baadae
2. Kuna watu wa mikakati kudhoofisha wengine wasiotakiwa (system oriented)
3. Kuna wapambe mahususi na wasindikizaji wa mteuliwa rasmi. (timu ya mteuliwa na marafiki zake)
Kupitia wagombea hao waliochukuwa fomu utawapata wote kwenye makundi haya ambao wanatokana na yale makundi mawili makuu niliyoyataja hapo juu.
Tatizo kwa Zanzibar ni kwamba lazima CCM itajeruhiwa na makundi haya na kuwafaidisha wapinzani. Mara zote ulaji na mazoea huiathiri CCM kwa namna moja au nyengine.
Wadadisi wa mambo mara hii wamefika mbali. Zipo tetesi kuwa WAHAFIDHINA WA CCM ZANZIBAR WANAUNGWA MKONO NA TIMU MOJA KUBWA UPANDE WA BARA ambao nao haukubaliani na Mwenyekiti namna anavyokiendesha chama na serikali.
Fumbo bado linabaki jee Mwenyekiti ataweza? Muda utasema.
Kishada.