FULL TEXT: HOTUBA ya Kambi ya Upinzani iliyosomwa na Lissu, Katiba na Sheria, yaibua makubwa bungeni

Wee kigoli mbona hueleweki? watu wanaongelea hotuba ya Mheshimiwa Tundu Lissu wewe umeng'ang'ania Dr Slaaa tu basi kaanzishe thread yako na watu watakufuata huko, pls waache watu wadiscuss ki mature na peleka ujinga wako Lumumba
Huyu jamaa ni mpuuzi kama wapuuzi wengine tu ndani ya chama chake.
infact hakuna asiye mpuuzi kwenye chama chake, wameziadiana kiwango cha upuuzi tu.
 
ZeMarcopolo, acha ujuha wewe. Soma hapa.

Unasoma vitu halafu huvielewi!!!

Soma vizuri uelewe kinachosemwa halafu fananisha na alichosema Mbowe...

Vijana wa bavicha ni SIFURI kama Msigwa tu. Hata hamjui tofauti kati ya kujitoa kwenye mchakato na kuhamasisha watanzania kuikataa rasimu...
 
Fahamu hawa ni wavivu wa kufikiri na mvivu yeyote hana fadhila isipokuwa lawama tu na kebehi za kijinga
 
Nimekuwa mfuatiliaji wa Bunge lakini kila msemaji wa Chadema anapoinuka ni lawama kwa serikali bila mapendekezo ya suluhu na kutupa vijembe hata kama jambo analozungumzia lina maslahi ya umma. Acheni kuwawapinzani wa nchi yenu

C03CM013 Imethibitishwa umepokea posho Tsh 7,000 kutoka kwa NAPE LUMUMBA Tatehe 03/05/13 saa 02:38 pm Salio lako la M-PESA ni Tsh 7,000
 
cjaona mahali ikizungumzia mahakama, kesi kurundikana, mazingira mabovu ya utendaji kazi wa waandaaji wa haki ya mtu kupatikana na mengine. au yapo kwenye page zilizosalia?

Nadhani wewe ni mgeni na CHADEMA,
walishasema 2013 ni mwaka wa KATIBA,
hayo unayotaka wewe walisha sema sana na hakuna jipya!
 
Kwa sisi tulioshiriki kwenye mchakato wa Uchaguzi wa mabaraza ya katiba ya Wilaya, tungewashangaa sana kama Chadema wasingejitoa, lakini mtu kama wewe mramba viatu vya ccm huwezi kuliona hilo.

Umenijibu kwa matusi ila nitakujibu kwa upole tu. In this world there are leaders and followers. Those who follow might follow different leaders but at the end of the day they are still followers. Tafakari kwa makini hiyo kauli. Mshabiki wa Yanga au mshabiki wa Simba tofauti yao rangi ya jezi tu ila at the end of the day bado ni shabiki tu.
 
Hii hotuba ni nzuri sana na ya kisomi.
Msigwa alipaswa kuomba msaada kwa Tundu Lissu ili na yeye aandae hotuba ya kisomi sio ule uchafu alioleta juzi Bungeni.
Hongera Tundu Lissu.
Hoja za Lissu zinahitaji kujibiwa kwa hoja...

Halo umeniacha na maswali kadhaa, Hivi Kama ametoa hoja nzuri zinahitaji kujibiwa kwa hoja au kwa vitendo?, Na kama kwa hoja ambayo ni maneno, je hoja hizo zitakuwa zimesaidia kurekebisha tatizo lililoongelewa katika hoja ya mwasilishaji?. Mi nadhani serikali ingeweza kuchambua kipi cha kufanyia kazi ili kiwekwe katika utendaji na kile kisichofaa kiwekwe katika kabati kama tulivyozoea.
 
SEHEMU YA HOTUBA YA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, MHESHIMIWA MATHIAS M. CHIKAWE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/2014

....Uratibu wa Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba

4. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2012/2013 Wizara yangu imeendelea kuratibu Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba. Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeanza kazi rasmi tarehe 01 Mei, 2012. Madhumuni ya kuanzishwa kwa Tume ni kuratibu, kukusanya, kuchambua na kutathmini maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya Katiba. Kwa kuzingatia muda ambao Sheria imeelekeza, Tume imeweka malengo ya kuwezesha kupatikana kwa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ifikapo Aprili 26, 2014.

5. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2012/2013, Tume ilitekeleza shughuli zake kama ifuatavyo:-

(i) Kutoa elimu kwa umma na kuhamasisha wananchi kushiriki katika hatua zote za mchakato wa mabadiliko ya Katiba kupitia vyombo vya habari (Redio, Luninga, Magazeti, Tovuti) machapisho mbalimbali na katika mikutano;

(ii) Kuandaa na kusambaza nakala 1,700,000 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, nakala 400,000 za Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83, Katiba ya Zanzibar nakala 19,000, Vipeperushi 800,000 vinavyoeleza majukumu ya Tume, Vipeperushi 670,000 vyenye maswali yanayoulizwa mara kwa mara na majibu yake nakala 588,600 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba sura ya 83 kwa lugha nyepesi;

(iii) Kuandaa mifumo/njia mbalimbali ya ukusanyaji wa maoni ya wananchi kama vile mikutano ya hadhara katika Wilaya zote nchini, mikutano ya Makundi Maalum, tovuti na mitandao ya kijamii, barua kwa njia ya posta, barua pepe, nukushi, ujumbe wa simu, makala, kujaza fomu maalum za Tume pamoja na magazeti;

(iv) Kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Mabadiliko ya Katiba katika Wilaya zote nchini na kuyachambua maoni hayo;

(v) Kuandaa, kuchapisha na kusambaza nakala 50,000 za Mwongozo kuhusu Muundo na Utaratibu wa kuwapata Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya (Mamlaka ya Serikali za Mitaa);

(vi) Kutoa elimu kwa umma kuhusu utaratibu wa uundwaji wa Mabaraza ya Katiba, majukumu ya Mabaraza hayo na kuandaa ratiba ya uchaguzi wa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba (Mamlaka ya Serikali za Mitaa);

(vii) Kuunda Mabaraza ya Katiba ya Wilaya (Mamlaka ya Serikali za Mitaa;

(viii) Kusimamia uchaguzi wa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya (Mamlaka ya Serikali za Mtaa);

(ix) Kuandaa Mwongozo wa Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi ya Watu; na

(x) Kuandaa Ripoti ya Awali na Rasimu ya Katiba.

6. Mheshimiwa Spika, Tume hii pia, inalo jukumu kubwa la kusimamia Mabaraza ya Katiba. Tume imeyagawa Mabaraza ya Katiba katika Makundi mawili; kundi la kwanza ni Mabaraza yatakayosimamiwa na Tume (Mabaraza ya Katiba ya Wilaya – Ngazi ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa) na kundi la pili ni Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi ya Watu wenye malengo yanayofanana.

Hadi sasa Tume imeweza kuwapata Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba katika Ngazi ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa kupitia chaguzi na taratibu mbalimbali ambapo jumla ya Wajumbe 10,932 wamepatikana katika Mikoa 17. Katika kufanikisha kupatikana kwa Wajumbe, Tume ilitumia Mfumo wa Serikali za Mitaa na taratibu za Mikutano katika ngazi za Serikali za Mitaa zilizopo sasa (Vijiji, Mitaa na Kata).Utaratibu huu ndio ulioainishwa kwenye Sheria zinazosimamia Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Aidha, kwa mujibu wa Ratiba ya shughuli za Tume, mikutano ya Mabaraza ya Katiba itaanza mwezi Juni, 2013 na itaendelea hadi mwezi Agosti, 2013.

7. Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kifungu cha 10 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayo mamlaka na uhuru katika utekelezaji wa majukumu yake. Aidha, Tume imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kuhusu jambo lolote linalopangwa kutekelezwa na kutoa taarifa baada ya utekelezaji wake kupitia mikutano na vyombo vya habari, magazeti, majadiliano katika redio, luninga na majarida ya kijamii... Inaendelea
 
Yaani nusu ya hotuba inazungumza habari za mkoa mmoja tu Arusha tena kata ya Sombetini tu, hiki chama kina kazi kuba sana kujivua tuhuma za ukabila na ukanda

Kwani lisu nae ni mtu wa Arusha?
 
Halo umeniacha na maswali kadhaa, Hivi Kama ametoa hoja nzuri zinahitaji kujibiwa kwa hoja au kwa vitendo?, Na kama kwa hoja ambayo ni maneno, je hoja hizo zitakuwa zimesaidia kurekebisha tatizo lililoongelewa katika hoja ya mwasilishaji?. Mi nadhani serikali ingeweza kuchambua kipi cha kufanyia kazi ili kiwekwe katika utendaji na kile kisichofaa kiwekwe katika kabati kama tulivyozoea.

Unapoongea hivyo unamanisha Lissu ametoa MAAGIZO. Lissu hana mamlaka ya kutoa MAAGIZO kwa serikali, anachotoa yeye ni hoja. Serikali inatakiwa kujibu hoja zake. Katika kujibu huko itasema nini kitafanywa na serikali. Ndio maana ya Bunge. Bunge sio mahali ambapo mmoja anasema mwingine anatekeleza, HAPANA - Bunge ni sehemu ya mijadala ya hoja...
 
swaadakta.......endelea kunywa dawa matokeo yanaonyesha unaendelea vzr, soon utarejea kwenye hali yako ya Uzalendo
 
Kuhusu barua pepe ya mama Asha-Rose Migiro:

2CHADEMA inapaswa kutambua kuwa kuingilia mawasiliano binafsi ya watu ni kuvunja sheria za nchi. Hii ni sawa na mtu kusema kuwa "nimeingia chumbani kwa mtu fulani nikafungua kabati lake nimekuta ana shilingi laki mbili, ?

Hii ndio tabia waliyoanzisha CHADEMA hivi karibuni...

Kwa hiyo CHADEMA inyamaze tu wakati mkipanga namna ya kuwahujumu? Mkuki kwa nguruwe!!
 
Maswali ya msingi ya kujiuliza ni

1.je, kwanini CHADEMA haijahamasisha viongozi na wanachama wake kuhakikisha mchakato wa uundwaji wa mabaraza ya katiba hauwapitii pembeni.

2. je, mamilioni anayolipwa Dr. Slaa ili aende vijijini kutoa elimu ya uraia kupitia M4C imezaa matunda gani kama haijawawezesha viongozi na wanachama wa CHADEMA kushiriki kidete katika mchakato wa uundwaji wa mabaraza ya katiba?

3. je, kwanini vijana wa BAVICHA hapa JF kila ilipoanzishwa thread ya uundwaji wa mabaraza ya katiba walikuwa hawachangii mada na badala yake wanajikita kwenye kujadili UDAKU mbalimbali unaoandikwa na gazeti la Tanzania Daima?

CHADEMA wanategemea mama Migiro atalala kama jinsi wao walivyolala juu yamchakato wa uundwaji wa mabaraza. Huo ni UTOTO...

Kaka kuna kitu unamiss kidogo...katika tuhuma anazotoa mjenga hoja ni kwamba hata baada ya kuhamisika na ZeMarcopolo akapigiwa kura za ndio kwenye mtaa kuna kamati ya watu 4 au 5 yenye veto unakutana nayo kwenye kata.

Swali la msingi la kujiuliza je ni kweli kamati za Kata zimetenda isivyo?

Na kwa nini kuwe na mchujo katani upande wa Bara wakati Zanzibar wananchi wanafursa ya moja kwa moja??

Kuna kitu nakiona hapa....wajumbe wa Zanzibar wako kwa maslahi ya Zanzibar hakuna uCUF wala uCCM wakati wajumbe wa Bara wameegemea kwenye siasa za vyama.

Wabara tusiposhtuka sasa, kesho tutakuwa tumechelewa
 
Last edited by a moderator:
Aisee hivi ndo vichwa vya chadema!! Du kamanda anatisha hilo halina ubishi,, mwenye historia yake ya kimasomo anisaidie, ila nina wasiwasi kuwa hawa magamba hawataielewa!! But it a recorded one.
 
Yaani nusu ya hotuba inazungumza habari za mkoa mmoja tu Arusha tena kata ya Sombetini tu, hiki chama kina kazi kuba sana kujivua tuhuma za ukabila na ukanda

Duh, mkuu mbona unachemka hivo????
 
Back
Top Bottom