Nimemsikia mkuu wa wilaya ya muheza bi subira kwenye taarifa ya itv ya saa 2 akizunguzia suala la watu waliovamia msitu. Kwamba serikali yake itakuwa full mass nondo. Hivi maana yake ni nini?
Kutumia maneno kama haya ni uzembe wa viongozi wetu kutumia maneno ya mitaani pasipo mahali pake.
Kwa kiasi kikubwa viongozi wetu wanachangia sana kuharibu kiswahili chetu kwa kutumia maneno yasiyo na maana kama haya. BAKITA nao wapo hoi, hawawezi hata kutoa tamko au kukaripia upotoshwaji wa kiswahili!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.