Fukwe za baharini oysterbay

Marigwe

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
228
18
Nampongeza Mheshimiwa Rais na uongozi wa serikali kuu mkoa wa Daressalaam na NEMC kuingilia kati kwa wakati muafaka na kusitisha ujenzi wa structures kwenye eneo la fukwe pwani ya Oysterbay na Masaki.
Mwanzoni nilipoona kuna bulldozers zinafyeka eneo hilo niliamini kuwa kuna wawekezaji ambao wameamua kuwekeza kwenye eno hilo kwa madhumuni na maslahi ya Watumiaji wote wa fukwe.
Inasikitisha kuona kuwa Halmashauri za Mkoa wa DSM kupitia idara yake ya mipango miji na Kamati ya madiwani wa mipango miji, haielewi kitu kingine zaidi ya kutoa vibali vya ujenzi wa majengo tu. Na majengo yenyewe yawe yale yanayojengwa na watu wenye nia ya kujenga kwa nia ya kupangisha majengo ya nyumba za kuishi au maduka. Masuala ya kupendezesha fukwe na mazingira haimo kabisa kwenye agenda zake. So sad indeed.
Hebu fikiria kwa nini eneo la fukwe kuanzia Seacliff hotel urudi mpaka Golden Tulip hotel halafu uanzie nje ya Police mess uje hadi kibandani Coco beach moja kwa moja mpaka light house karibu na kasri ya Agakhan wasipatengeneze kwa kuweka pavements za na walkways ambapo wangeweka taa za usiku. Eneo lote hilo wangepanda maua na miti ikawa park ambapo watu wangeweza kufan ya mazoezi yajogging, ya kutembea au hata kukaa na kula upepo wa bahari. Na wale vijana wanaojinasisha kwenye daladala au malori wakati wana roller skates zao, wangeweza kucheza michezo yao kwenye pavements hizi.
Ninamuunga mkono pia mheshimiwa Janet Zebedayo Mbene Mwenyekiti wa mtaa wa Masaki na sasa mbunge wa kuteuliwa, kwa kuwa mstari wa mbele kupinga zoezi hilo la kujenga ati maeneo ya recreation. Well done Mheshimiwa.
 
nilipita pale nako utafikiri tuko kwenye beach za Capetown in 1980's

Upande wa mwanzoni ukitokea kwa Rostam utakuta Waarabu,wadosi na wenye rangi za benki

Ukienda Mbele kule kwenye ile structure utakuta waafrica wengiiii

makes you wonder mhhhhhh
 
Nampongeza Mheshimiwa Rais na uongozi wa serikali kuu mkoa wa Daressalaam na NEMC kuingilia kati kwa wakati muafaka na kusitisha ujenzi wa structures kwenye eneo la fukwe pwani ya Oysterbay na Masaki.
Mwanzoni

Hakuna cha wakati muafaka wala nini hapo! Wakati muafaka ni wao kuhakikisha tangu mwanzo kuwa haya mambo hayatokei!!

Halafu pongezi ya nini wakati ndiyo kazi yao? Hivi wewe hapo kazini kwako tuseme kwa mfano una wajibu wa kufuatilia mambo fulani kama sehemu ya kazi yako, ukifanya huo ufuatiliaji huwa unapewa pongezi?

Si kuwa nakushambulia ndugu yangu, ni kwamba nimeshachoshwa na mambo ya serikali yetu! Kwenye yanayostahili kufuatiliwa na uongozi wa juu hakuna linalofanyika lakini kwenye ishu ndogo kama ujenzi wa "flyovers" na fukwe ndio uongozi mkuu unasikika!!

What happened to "delegating responsibilities that others can handle"?
 
Ndugu yangu Injinia ulitaka niseme nini kuhusu suala la fukwe? Nitumie matusi? Au? Pongezi nimetoa kwa sababu mimi ni mstaarabu. Sasa nilitegemea wewe siyo lazima upongeze ila ungetoa maoni yako labda ujenzi uendelee?

Mimi kwa ustaarabu nilio nao sioni kuwa unanishambulia ila nakuona hujui kujenga hoja na badala yake unajielekeza kwenye "trivialities". Pole sana
 
Wanavuta subira tu....nearer to eletions wataanza ujenzi wa nguvu pale.Kama wameweka na beacons hamna kurudi nyuma.Ironically the area used to be a sisal estate pre 1980s kuanzia Police OM mpaka kule kwenye makombora yetu yenye kutu.Mimi mwenyewe niliuona mkonge pale na wala hapajawahi kuwa open to public.Wengine hapa tunachanganya Coco Beach na hiyo TAANKE ESTATE.Sehemu hizo awali zilitenganishwa na Police officers mess kabla ya hiyo estate kumegewa Ladwa na Mwinyi administration na kujengwa Indian Ocean Hotels(Golden Tulip) na Sea Cliff,ilipokuwa pia plot ya Mama Karume(Cassanova Restaurant sasa Seacliff Village).Wakati wa Mkapa huyu Ladwa akataka kumegewa eneo zaidi kwenda north(anapofanya temporary parking kwa sasa) na akazuiwa.Ikisahafanyika hiyo ESIA(Environmental and Social I Impact Assessment) basi ujenzi utaanza rasmi.Baraka zote zilishatolewa...
 
Back
Top Bottom