GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
· Yadaiwa ana Ushawishi Mkubwa katika Maamuzi ya Chama
· Wakati mwingine kwa Utashi hata kuliko Kanuni na Maadili ya Uongozi
· Wanaoitwa Pandikizi wadai hofu ni Urais 2015
· Walaani kutumiwa jina Rais kwa Katibu Mkuu katika safari za M4C kuwa ni chanzo cha migogoro mingi ndani ya CDM
M2 ni Zaidi ya Anavyofikirika
SOMA KWA MAKINI UZI HUU HALAFU TUKUTANE BAADA YA PRESS CONFERENCE:
Mabingwa wa misamiati na nahau wanaamini kabisa ''Kila matokeo ya mafanikio au kuporomoka kwa mwanamume nyuma yake kuna mkono wa mwanamke''.
Ni dhahiri kama mama ni nguli wa kupanga, kuamua na kuongoza njia sahihi hapana shaka matokeo ya tunu hizo yataakisiwa na mafanikio katika familia hiyo, na akiwa bingwa wa kutaka makuu, mbwembwe na daima awe juu faraka na sintofahamu hujenga makazi katika familia hii.
Siku chache baada ya kufukuzwa uanachama kwa waliokuwa madiwani wa CDM huko Igoma kumeibuka malalamiko mazito juu ya mwenendo wa Maamuzi yanayochukuliwa na Katibu Mkuu wa CDM kwamba hufanyika kwa ushauri mkubwa ubavu wake.
Madai haya ambayo hakuna hata kiongozi mmoja tuliyeongea naye jana aliyekubali kuyathibitisha huku kila mmoja akirusha mpira kwa mwenzie yanadaiwa kuongeza hali ya ujoto wa kisiasa na vuguvugu la kutoaminiana kwa madereva ndani ya CDM huku mzimu wa mkasa wa timuatimua makao makuu zama za Mwigamba hadi Arusha, Mbeya na mapokezi ya Mama Josephine hadi sakata hili la Mwanza na mengine mengi yakiongeza ufa katika uimara wa chama.
Kwa afya ya Chama naomba nisiandike mengine zaidi katika kulibaini hili ili kutoa nafasi kwa viongozi wangu kulishughulikia hili na kusisitiza katika misingi na maadili ya uongozi huku wakizingatia ukomo wa fikra mbadala katika maamuzi mazito ya kichama.
Huku haya yakitajwa kama ni moja ya Agenda inayokusudiwa kusambazwa rasmi kwa umma kupitia mikutano ya hadhara kwa kundi linaloonekana kuwekwa pembeni ndani ya CHADEMA wanachagizwa na madai kuwa kutumiwa kwa jina Rais kwa baadhi ya wanachama katika ziara za M4C mikoani kwa Katibu Mkuu zimemtia wingu katika fikara zake na kuamini kuwa yeyote ndani ya chama anayedaiwa kuwa na nia na nafasi hiyo kuwa dhihaka kwake na mtovu wa nidhamu kwani kote apitapo wanachama tayari wanamtambua yeye kama Rais.
Jina hili ambalo linasemekana chimbuko lake ni muda mfupi baada ya uchaguzi mkuu ambapo kinadharia chama kiliamini kupokwa nafasi hiyo kwa mchezo mchafu wa tume mgombea kiti hicho na katibu Mkuu alikuwa akishangiliwa kama Rais katika mikutano yake ya hadhara kama ishara ya kuonyesha uungwaji mkono wa wanachama licha ya unaodaiwa kuwa udhalimu wa Tume kepeleka mambo kama watakavyo.
Kibwagizo hicho cha Rais, Rais, Rais kila asimamapo katibu Mkuu katika mikutano yake mingi kimedaiwa kunasa katika fikara za mashabiki wa CDM mpaka sasa na kumhakikishia usultani huo ambao kamwe anaelekea kuamini hakuna Rais tena 2015 ndani ya CDM zaidi yake.
Kwa mintarafu hiyo hata migongano na nyuzi nyingi hapa Jamvini za kumpima ubavu na ZZK zinatokana na ukweli huu kwamba hutakiwi kusikika ndani ya chama mwanaCDM mwingine unawaza kuikwaa nafasi hiyo. Hang over hiyo imepelekea kuibuka hofu hewa ya kuwepo kwa mapandikizi wa ZZK ambao wanadaiwa kumuunga mkono na kwamba watakuwa tatizo kubwa katika vikao vikuu vya chama wakati wa mchakato wa kumpitisha mgombea wa Urais, wanafanywaje sasa? Jibu ni kwamba watengenezewe mazingira ya kuonekana watovu wa Nidhamu kisha fukuza wote kusafisha chama.
Inadaiwa Orodha bado ni ndefu na wote watakwenda mmoja baada ya mwingine ili kuhakikisha kwamba 2015 mambo saafi. Hii siyo CDM inayokusudiwa hayumkini kuna tatizo la msingi hapa.
Wengi wameaminishwa kuwa ZZK ni pandikizi wa Chama fulani na amekuwa mmoja wa Viongozi wanaoyumbisha maamuzi CDM na wanaojitenga katika harakati nyingi kumbe anaepukwa yeye kuwepo katika maeneo hayo kwa makusidi kabisa ili kumtengenezea chuki mbaya na wanaCDM hii ni hatari sana bila shaka.
Moja ya udhaifu mkubwa unaotajwa katika muendelezo huu ni kuchukuliwa kwa maamuzi bila kufanya tafiti za kutosha kuhusu kushutumiana huko na pia kutekeleza malengo kwa hasira na jazba bilakujali matokeo yake ya muda mrefu na taswira ya chama kwa jamii.
Licha ya madai haya M/Kiti anatajwa kama Icon muhimu sana isiyofungamana na upande wowote katika shutuma hizi na hivyo kumpa nafasi kubwa ya kuendelea kuimarisha chama na kuondosha matabaka haya yanayokomaa sasa.
My Take:
Muarobaini wa tatizo hili upo na moja ni kuhakikisha ule usultani wa Mama kuamua mambo mazito alioupinga hata Baba wa Taifa pale Kilimanjaro Hotel enzi za Uhai wake unapunguzwa makali nakuwekwa mbele ustawi wa chama badala ya Urais ambao unaelekea kuwa binafsi badala ya taasisi.
Adhabu mbadala kwa viongozi na wanachama zipo ila kama ililazimika kufukuza pia si vibaya lakini tukubali kuteswa na mizimu ya kama ya akina Malema na ANC.
ADIOS
· Wakati mwingine kwa Utashi hata kuliko Kanuni na Maadili ya Uongozi
· Wanaoitwa Pandikizi wadai hofu ni Urais 2015
· Walaani kutumiwa jina Rais kwa Katibu Mkuu katika safari za M4C kuwa ni chanzo cha migogoro mingi ndani ya CDM
M2 ni Zaidi ya Anavyofikirika
SOMA KWA MAKINI UZI HUU HALAFU TUKUTANE BAADA YA PRESS CONFERENCE:
Mabingwa wa misamiati na nahau wanaamini kabisa ''Kila matokeo ya mafanikio au kuporomoka kwa mwanamume nyuma yake kuna mkono wa mwanamke''.
Ni dhahiri kama mama ni nguli wa kupanga, kuamua na kuongoza njia sahihi hapana shaka matokeo ya tunu hizo yataakisiwa na mafanikio katika familia hiyo, na akiwa bingwa wa kutaka makuu, mbwembwe na daima awe juu faraka na sintofahamu hujenga makazi katika familia hii.
Siku chache baada ya kufukuzwa uanachama kwa waliokuwa madiwani wa CDM huko Igoma kumeibuka malalamiko mazito juu ya mwenendo wa Maamuzi yanayochukuliwa na Katibu Mkuu wa CDM kwamba hufanyika kwa ushauri mkubwa ubavu wake.
Madai haya ambayo hakuna hata kiongozi mmoja tuliyeongea naye jana aliyekubali kuyathibitisha huku kila mmoja akirusha mpira kwa mwenzie yanadaiwa kuongeza hali ya ujoto wa kisiasa na vuguvugu la kutoaminiana kwa madereva ndani ya CDM huku mzimu wa mkasa wa timuatimua makao makuu zama za Mwigamba hadi Arusha, Mbeya na mapokezi ya Mama Josephine hadi sakata hili la Mwanza na mengine mengi yakiongeza ufa katika uimara wa chama.
Kwa afya ya Chama naomba nisiandike mengine zaidi katika kulibaini hili ili kutoa nafasi kwa viongozi wangu kulishughulikia hili na kusisitiza katika misingi na maadili ya uongozi huku wakizingatia ukomo wa fikra mbadala katika maamuzi mazito ya kichama.
Huku haya yakitajwa kama ni moja ya Agenda inayokusudiwa kusambazwa rasmi kwa umma kupitia mikutano ya hadhara kwa kundi linaloonekana kuwekwa pembeni ndani ya CHADEMA wanachagizwa na madai kuwa kutumiwa kwa jina Rais kwa baadhi ya wanachama katika ziara za M4C mikoani kwa Katibu Mkuu zimemtia wingu katika fikara zake na kuamini kuwa yeyote ndani ya chama anayedaiwa kuwa na nia na nafasi hiyo kuwa dhihaka kwake na mtovu wa nidhamu kwani kote apitapo wanachama tayari wanamtambua yeye kama Rais.
Jina hili ambalo linasemekana chimbuko lake ni muda mfupi baada ya uchaguzi mkuu ambapo kinadharia chama kiliamini kupokwa nafasi hiyo kwa mchezo mchafu wa tume mgombea kiti hicho na katibu Mkuu alikuwa akishangiliwa kama Rais katika mikutano yake ya hadhara kama ishara ya kuonyesha uungwaji mkono wa wanachama licha ya unaodaiwa kuwa udhalimu wa Tume kepeleka mambo kama watakavyo.
Kibwagizo hicho cha Rais, Rais, Rais kila asimamapo katibu Mkuu katika mikutano yake mingi kimedaiwa kunasa katika fikara za mashabiki wa CDM mpaka sasa na kumhakikishia usultani huo ambao kamwe anaelekea kuamini hakuna Rais tena 2015 ndani ya CDM zaidi yake.
Kwa mintarafu hiyo hata migongano na nyuzi nyingi hapa Jamvini za kumpima ubavu na ZZK zinatokana na ukweli huu kwamba hutakiwi kusikika ndani ya chama mwanaCDM mwingine unawaza kuikwaa nafasi hiyo. Hang over hiyo imepelekea kuibuka hofu hewa ya kuwepo kwa mapandikizi wa ZZK ambao wanadaiwa kumuunga mkono na kwamba watakuwa tatizo kubwa katika vikao vikuu vya chama wakati wa mchakato wa kumpitisha mgombea wa Urais, wanafanywaje sasa? Jibu ni kwamba watengenezewe mazingira ya kuonekana watovu wa Nidhamu kisha fukuza wote kusafisha chama.
Inadaiwa Orodha bado ni ndefu na wote watakwenda mmoja baada ya mwingine ili kuhakikisha kwamba 2015 mambo saafi. Hii siyo CDM inayokusudiwa hayumkini kuna tatizo la msingi hapa.
Wengi wameaminishwa kuwa ZZK ni pandikizi wa Chama fulani na amekuwa mmoja wa Viongozi wanaoyumbisha maamuzi CDM na wanaojitenga katika harakati nyingi kumbe anaepukwa yeye kuwepo katika maeneo hayo kwa makusidi kabisa ili kumtengenezea chuki mbaya na wanaCDM hii ni hatari sana bila shaka.
Moja ya udhaifu mkubwa unaotajwa katika muendelezo huu ni kuchukuliwa kwa maamuzi bila kufanya tafiti za kutosha kuhusu kushutumiana huko na pia kutekeleza malengo kwa hasira na jazba bilakujali matokeo yake ya muda mrefu na taswira ya chama kwa jamii.
Licha ya madai haya M/Kiti anatajwa kama Icon muhimu sana isiyofungamana na upande wowote katika shutuma hizi na hivyo kumpa nafasi kubwa ya kuendelea kuimarisha chama na kuondosha matabaka haya yanayokomaa sasa.
My Take:
Muarobaini wa tatizo hili upo na moja ni kuhakikisha ule usultani wa Mama kuamua mambo mazito alioupinga hata Baba wa Taifa pale Kilimanjaro Hotel enzi za Uhai wake unapunguzwa makali nakuwekwa mbele ustawi wa chama badala ya Urais ambao unaelekea kuwa binafsi badala ya taasisi.
Adhabu mbadala kwa viongozi na wanachama zipo ila kama ililazimika kufukuza pia si vibaya lakini tukubali kuteswa na mizimu ya kama ya akina Malema na ANC.
ADIOS