Fukuto la kungojea majibu ya VVU/Ukimwi or HIV/AIDS

KITAULO

JF-Expert Member
Apr 27, 2018
1,926
2,776
Wana JamiiForums,

Hamna jambo zito kama kusubiria majibu baada ya kufanya vipimo vya maambukizi ya VVU. Ni kipindi ambacho mtu hujikuta upo kwenye ulimwengu mwingine kiroho na ndo kipindi mwanadamu heweka nadhiri nyingi na Mungu wake endapo tu atamuepusha na hilo dhahama.

Hata mkiwa wengi hamna anayepata nguvu ya kuongea na mwenzake. Kila mtu anazama kwenye dimbwi mawazo kujaribu kutafakari ni wapi anahisi alizingua na kuanza kuevaluate makoloni yake yote aliyopitia.

Hakika hamna kipindi kigumu kama hiki. Pale unaitwa kuchukua majibu yako mwili huwa unapoteza nguvu ndo kipindi tumbo la kuhara hukushika na mapigo ya moyo yanakuwa kwenye speed ya ajabu.

Sasa ukute mshauri ana mbwembwe wakati wa kutoa majibu huwa mtu unahisi kama dunia yote siyo yake tena.

Hakika kusubiri majibu ni kipindi kizito na chenye siri nzito..

Wadau hebu tupeane experience wakati wa kusubiri majibu ya VVU/AIDS
 
Alafu kwa nn watu weng wanaogopa ukimwi ?huwa najiuliza Mara kadhaa cpati majibu ,Kuna magonjwa mfano presha ,kisukari,kufery kwa Figo ,kansa, n.k iweje ukimwi ndo tishio nadhani Yale matangazo ndo yalichangia kutuogopesha siku hzi siyasikii
 
Alafu kwa nn watu weng wanaogopa ukimwi ?huwa najiuliza Mara kadhaa cpati majibu ,Kuna magonjwa mfano presha ,kisukari,kufery kwa Figo ,kansa, n.k iweje ukimwi ndo tishio nadhani Yale matangazo ndo yalichangia kutuogopesha siku hzi siyasikii
Ngoma haijawah kuzoeleka ndugu...tuache kudanganyana...
 
Kusubiri majibu ya HIV hakuna shida yoyote, tatizo linakuja unapokuwa mzinzi ndio presha inakupanda, sasa kama unaviogopa virusi kwanini usiache zinaa, kupima ukimwi mnakugeuza tendo la kijasiri kumbe ni upuuzi mtupu, wacha dhambi, wacha uzinzi, hutaogopa kupima HIV maisha yako yote.

Njia nyingine za maambukizi ni asilimia ndogo sana, haziwezi kukuogopesha kupima, uzinzi/zinaa ndio tatizo kubwa linaloepukika, ukishindwa tumia kinga. Maginjwa kama kansa hayo ndio yakuogopa kupima, yako nje ya uwezo wetu unless uwahi kuyagundua, but sio HIV.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niende kupima ili iweje? wana dawa za kunipa nipone?

Mi mnaopima nawambia tu mtakipata mnachokitafuta.
Ni kweli lakn kuijua afya yako ni jambo jema...kuliko kuishi kwa hofu
 
jd41, Tatizo vijana wengi..tuna ile inaitwa kusahua...utapima leo na kujiapiza hautorudia tena kezembea...lkn baada ya week unarudi kule kule
 
Majibu mazuri ni yale unapewa moja kwa moja. Sio mambo ya kuanza kupeana ushauri. Hii huongeza hofu na presha kuwa juu.

Haiwezekani mimi mwenyewe nimejileta afi wewe uanze kutoa nasaha. Hayo yote nakuwa nimeshamalizana na halmashauri ya kichwa changu ndiyo maana nafikia maamuz ya kuja kupima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Majibu mazuri ni yale unapewa moja kwa moja. Sio mambo ya kuanza kupeana ushauri. Hii huongeza hofu na presha kuwa juu.

Haiwezekani mimi mwenyewe nimejileta afi wewe uanze kutoa nasaha. Hayo yote nakuwa nimeshamalizana na halmashauri ya kichwa changu ndiyo maana nafikia maamuz ya kuja kupima.

Sent using Jamii Forums mobile app
True man...
 
Wakati unaserebuka kwanini hukufikiria haya, Kama ungefanya hivyo, wakati unapima usingefikiria haya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom