Fukuto la Katiba: Wasira azomewa mkutanoni, akasirika na kufunga mkutano ghafla!

CCM wamebaki na Amri, Bunduki, mabomu na maji washa tu.. hata warusha mabomu na risasi nao wako cdm- G Lema
 
Wasira Need to count down he is Days are numbered. It is real shame kwani watu wa Bunda wamemchoka mzee huyu nae bado anaota kuwania Urais wa nchi hii ni ajabu na kweli. Why mtu usikubali tu kuwa kila wakati na zama zake.
 
siamini kama kweli tukio la namna hii lilitokea,unless mtoa thread anataka tu tujadili uozo/ubovu wa sheria ile

Wewe endelea tu kutoamini lakini ukweli ndo huo. Kabla ya kwenda bunda walikuwa wilayani serengeti na kufanya mkutano mugumu mjini, kilichowakuta ndo hicho walichokutana nacho bunda.

Sasahivi wananchi wameamka na wanatambua haki zao, kuwatengenezea sheria inayowabana kutoa maoni yao kwa uhuru ndicho kitu kimewaudhi sana, has kuweka kipengele cha kuwaadhibu watu watakao toa elimu ya uraia na juu ya sheria ya mapitio ya katiba.
 
Siku zote kenye kuhesabu vitu huwezi kuanza na namba kubwa ukaziruka ndogo,na hivi ndo Magamba wanavyojaribu kufanya,ni wavivu wa kufikiri na wepesi wa kufanya,wavivu wa kutafakari wepesi wa klaumu,wagonjwa wa kifikra wpesi wa kukatiza Dosi kabla hajapona sababu wanajiona wao ndio bwana wakubwa......... Lazima tukae chini wote tuelimishane kuhusu hili,sababu ni haki yetu ya msingi kulipigania,kama halina faida kwao why wanatunga sheria za kubana watu na kuwanyima watu uhuru wa kutoa maoni au kuelimisha kuhusu katiba,hakuna ugonjwa mbaya kama Ufinyu wa ki fikra,kama fikra yako ni duni na unaendekeza ubabe,jua kuna wababe zaidi yako,halafu la safari ina mwisho wake inategeme na Dereva anavyoendesha gari,jua kuwa ndani ya Basi abiria ndo wana conrol jinsi gani dreva aende speed,akichemka wanamshusha,magamba ni km dereva na wananchi ni abiria sasa kwa vile wamechemka... PIGAA CHIIINIII...
 
Chadema kusanyeni kumbukumbu hizi huyu ni kiongozi watatu anavunja sheria ya kukusanya maoni,isije na nyie mkateleza mkaenda jela chukueni reference hizo za viongozi wa ccm,hawakujua kwamba sheria waliyoitunga inawabana hadi wao hahahahahahahahahaaa
 
CCM and its co. hawakujadili muswada ule, badala yake waliijadili wabunge wa chadema waliotoka nje ya bunge, hivyo hata wao wanashangaa kilichomo ktk sheria hiyo. In short hili bunge la ccm lilifanya kazi ya kutransform ule mswada kuwa sheria pasipo kujadiliwa matokeo yake nao wanashangaa kcontent ya sheria ile. Wasira oyeee!
 
Hongereni sana wanachi wa Bunda hii inaonyesha jinsi ukomavu wenu wa kisiasa ulivyo juu,inatakiwa huyo waziri wa magamba ajue kusoma nyakati na ishara kwamba sasa haitajiki jimboni hapo tena!
 
Wasira ni mmoja ya watu ambao CCM inaamini ana influence sasa kama ameanza kuzomewa sijui atabaki nani?
 
Hakulala hapo mkutanoni...?kuzomewa ndo saiz yao..mpaaka nashangaa zile kura mil5 walizzipata wap...maana kila wanakoenda wanaonekana watu wa ajabu
 
Kwahali ilivyo tutegemee kama hawajaleta madiliko bungeni hasa kile kifungu cha 21, kinachozuia mtu yoyote kujadili. Basi tutegemee kama kawaida ya magamba kukanyaga twende.
 
Wanafikiri wananchi hawakuusikiliza mjadala ule bungeni waanze kuweka yao, wakati huo umepita kila mtu anajua ubabe waliotumia ccm kwenye mjadala huo kwa manufaa yao. Sasa wameshaanza kupata malipo na bado.
Ndugu yangu, kule bungeni hawakujadili mswaada bali kwa siku zote tatu walimjadili Tundu Lisu na baadae wakaupitisha mswada kuwa sheria, hatimae raisi wao akauweka saini yake. Sasa wanapopita kutetea sheria hiyo wanakumbana na watanzania makini na kumwagwa kinyesi!
 
Sheria inayohusu katiba Mpya = Sheria ya Uchaguzi 2010. Mbwembwe nyingi mwisho Uharo wa damu.
 
Back
Top Bottom