JF Member
JF-Expert Member
- Dec 14, 2014
- 7,298
- 9,524
Nimekua nikifuatilia kampeni tangu zianze. Niseme kwamba kampeni za mwaka huu zinautulivu kuliko kampeni za 2015.
Kuna vitu vichache ambavyo vinahitaji kukemewa.
Kitendo cha mtu kuzomea, kuzuia, ama kufanya fujo kwenye mkutano wa kampeni si cha kufumbiwa macho na kiongozi yeyote awe wa kisiasa, wa kidini ama wa kijamii.
Nimeona Matukio yakifanywa na watu kadhaa katika hizi harakati za kisiasa za uchaguzi ambayo sio mazuri Wala hayana umuhimu.
Nitoe mifano michache.
1. Lissu akiwa Hai alizomewa na vijana na hata mmoja wa hao vijana kuhatarisha maisha.
2. Magufuli akiwa Bukoba wamesimama vijana wakidai hawamtaki. Huku wafuasi wake eneo lile walikuwa wamefurika kuliko kawadia
Matukio kama haya yanaeweza kuleta maafa makubwa sana.
Nitashangaa iwapo viongozi wetu wa kisiasa wataendelea kushangilia matukio ya aina hii.
Ukiona mgombea anamwaga sera mpinge kwa sera kwenye mkutano wako. Mtu akiwa na wafuasi wake anakuwa na ulinzi mkali kuliko hata ulinzi wa jeshi lenye mizinga.
Chonde chonde, tuache mara moja.
Nawatakia uchaguzi mwema.
Kuna vitu vichache ambavyo vinahitaji kukemewa.
Kitendo cha mtu kuzomea, kuzuia, ama kufanya fujo kwenye mkutano wa kampeni si cha kufumbiwa macho na kiongozi yeyote awe wa kisiasa, wa kidini ama wa kijamii.
Nimeona Matukio yakifanywa na watu kadhaa katika hizi harakati za kisiasa za uchaguzi ambayo sio mazuri Wala hayana umuhimu.
Nitoe mifano michache.
1. Lissu akiwa Hai alizomewa na vijana na hata mmoja wa hao vijana kuhatarisha maisha.
2. Magufuli akiwa Bukoba wamesimama vijana wakidai hawamtaki. Huku wafuasi wake eneo lile walikuwa wamefurika kuliko kawadia
Matukio kama haya yanaeweza kuleta maafa makubwa sana.
Nitashangaa iwapo viongozi wetu wa kisiasa wataendelea kushangilia matukio ya aina hii.
Ukiona mgombea anamwaga sera mpinge kwa sera kwenye mkutano wako. Mtu akiwa na wafuasi wake anakuwa na ulinzi mkali kuliko hata ulinzi wa jeshi lenye mizinga.
Chonde chonde, tuache mara moja.
Nawatakia uchaguzi mwema.