William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
- Freeman Haikaeli Mbowe au kama tunavyomuita mtaani "MCHAGGA" ni rafiki yangu wa karibu sana sana nimemfahamu toka utotoni na ndio maana mpaka leo ninamuheshimu sana kwani ni mmmoja wa Binadam wachache sana ninaowafahamu Duniani wenye msiamo na walio radhi kupoteza anything kwa ajili ya msimamo. Toka utotoni Freeman hakuwahi kuwa mpenzi au shabiki wa TANU au CCM, na sitashangaa kwamba hakuwahi kuwa hata Mwanachama ni msimamo mzito aliokuwa nao kwamba TANU/CCM zilikuwa zinakosea na zinahitaji kurekebishwa. Na ndio maana wakati ulipofika hakuwa na tatizo kujiunga na Upinzani, yaani Chadema chama ambacho kilianza kwa kasi sana chini ya Mzee Mtei, lakini kikashuka sana chini ya Marehemu Mzee Makani na kikaja kuamka tena chini ya Freeman Mbowe Mwenyekiti wa sasa. Amekichukua chama hicho kikiwa mahututi sana akapigana mpaka kukipa meno na kuitingisha sana CCM, na cha msingi sana akafanikiwa kuwaingiza Chadema Vijana wengi wenye misimamo kama yake ya Kipinzani na kukifanya kuwa Chama kweli cha Upinzani na pia ni yeye ambaye amekifikisha chama hicho kilipo sasa hoi bin taabani.
- Freeman alikipatia uhai chama hicho kwa kujikita kwenye mbinu mbali mbali za michezo ya kisiasa ambayo inakubalika kwenye lengo la kuhakikisha ushindi na the end justifying the means, kwa mfano alikikuta Chadema kikiwa na Wabunge wachache sana kulinganisha na sasa na the number one mark ya Uongozi wa Freeman ambayo kama historia ya siasa na Taifa hili itamkumbuka kwenye uongozi ni the FACT ya uongozi wake wa Chadema kuweza kuwa attract Mawaziri Wakuu wawili wa zamani wa CCM, kuwaunganisha Wapinzani karibu wote nchini under UKAWA katika kuikosesha usingizi Serikali ya CCM..... lakini kwenye maisha kila chenye mwanzo ni lazima kiwe na mwisho na hatimaye mwisho wa uwezo na akili nyingi za Freeman kuongoza Upinzani wa kweli sasa zimeaanza kufika mwisho, Chadema inahitaji Kiongozi mpya mwenye mbinu mpya kuweza kupambana na CCM.
- Pamoja na makubwa yote aliyokifanyia Chadema kuna maamuzi mengi Freeman aliyafanya kwa kucheza bahati nasibu ya Siasa ambayo matokeo hayakuwa kama alivyotegemea lakini kuna faida kiasi fulani Chadema waliipata kutokana na his gambling na hasa kwenye kuwapokea Mawaziri Wakuu 2 wa zamani wa CCM, kwa upande mmoja alikiongezea Chama chake nguvu ya Muda na pia kwa upande mwingine alikipunguzia chama chake nguvu ya muda mrefu, isipokuwa cha msingi sana ni kwamba akiwa kwenye kilele cha Utawala wake Freeman aliwekeza sana kwenye Media na Social Media ndio the best political investment inayokibeba chama hicho sasa hivi wakati kikiwa almost mwisho wa uhai wake. Kuwekeza kwake kwa Vijana wenye msimamo na Media ndio kunakisaidia sana chama hicho kuendelea kupumua mpaka leo huku the Natural Fate ikiwa inakipa nafasi chama hicho nafasi ya kujikarabati ingawa Viongozi na Wanachama wengine wa Chama hicho wanashindwa kuielewa hiyo concept.
- Huu ni wakati muafaka wa Freeman kujiuliza kama je kuna nini ambacho bado hajakifanya katika uwezo wake wa kufikiri na kuongoza Upinzani, kwa sasa Chama hicho sio siri kimejipiga dhoruba kwa kamali ya kisiasa aliyoamua kuicheza yeye mwenyewe Freeman kwa niaba ya Chama chake na ndio maana ya Uongozi wa Taifa ni kwa Kiongozi kuwa na uwezo wa kuona mbali kwa niaba anaowaongoza. Chadema imefika mahali inahitaji ukarabati mkubwa sana na wa hali ya juu sana kuweza kurudi tena au kufikia zaidi ya kilipokuwa huko nyuma. Chadema haina agenda yoyote tena zaidi ya kusubiri Viongozi wa CCM wakosee herufi na maneno na kuanza kuyarudia rudia kama utani badala ya hoja nzito kwa Umma ambao ulifikia hatua ya kuwaamini sana nyakati fulani zilizopita. toka Utawala mpya wa Awamu ya Tano ya CCM ushike madaraka Chadema imepwaya mno ni kawaida kwenye siasa za Kitaifa ni kama chama cha Democrats huko USA na wao sasa hivi wanakabiliwa na wakati kama huu wa Chadema ni wakati unaohitaji Viongozi wake wa juu kujitafakari upya kama kweli wapo sawa na wanachohitajika kukifanya yaani Upinzani.
- Kutumia muda mwingi kuwashambulia kwa maneno ya mafumbo mafumbo na lugha zisizokuwa za kistaarabu siamini kama inaweza kuisaidia Chadema kurudi kwenye mstari wake wa kuaminiwa na Wananchi kama ilivyokuwa huko siku za nyuma. Binafsi ninakubaliana sana na maneno ya Mwenyekiti Mao Tse tung kuwa...... "Ukiona binadam wawili wanakubaliana kwa kila kitu na kwa wakati wote ujue kwamba aidha Mmojawapo ni Mgonjwa au wote wawili sio wazima".....Historia ya Dunia inaonyesha Chama kimoja kikikaa madarakani kwa zaidi ya Miaka 50 huwa kunakuwa na tabia za kujisahau kwa chama hicho so kinahitaji kukumbushwa kumbushwa kurudi kwenye mstari so ni muhimu sana kuwepo kwa Upinzani nchini, lakini sio kwa huu upinzani uliopo sasa. Freeman amekisaidia sana Chadema sana, lakini Chadema ilipofikia sasa hivi nina wasi wasi ndio mwisho wa uwezo wake kufikiri kisiasa ni wakati muafaka akatafakari kama ni wakati wa kufanya maamuzi magumu sasa au kuja kujutia baadaye.
- MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
Le Mutuz Nation
- Freeman alikipatia uhai chama hicho kwa kujikita kwenye mbinu mbali mbali za michezo ya kisiasa ambayo inakubalika kwenye lengo la kuhakikisha ushindi na the end justifying the means, kwa mfano alikikuta Chadema kikiwa na Wabunge wachache sana kulinganisha na sasa na the number one mark ya Uongozi wa Freeman ambayo kama historia ya siasa na Taifa hili itamkumbuka kwenye uongozi ni the FACT ya uongozi wake wa Chadema kuweza kuwa attract Mawaziri Wakuu wawili wa zamani wa CCM, kuwaunganisha Wapinzani karibu wote nchini under UKAWA katika kuikosesha usingizi Serikali ya CCM..... lakini kwenye maisha kila chenye mwanzo ni lazima kiwe na mwisho na hatimaye mwisho wa uwezo na akili nyingi za Freeman kuongoza Upinzani wa kweli sasa zimeaanza kufika mwisho, Chadema inahitaji Kiongozi mpya mwenye mbinu mpya kuweza kupambana na CCM.
- Pamoja na makubwa yote aliyokifanyia Chadema kuna maamuzi mengi Freeman aliyafanya kwa kucheza bahati nasibu ya Siasa ambayo matokeo hayakuwa kama alivyotegemea lakini kuna faida kiasi fulani Chadema waliipata kutokana na his gambling na hasa kwenye kuwapokea Mawaziri Wakuu 2 wa zamani wa CCM, kwa upande mmoja alikiongezea Chama chake nguvu ya Muda na pia kwa upande mwingine alikipunguzia chama chake nguvu ya muda mrefu, isipokuwa cha msingi sana ni kwamba akiwa kwenye kilele cha Utawala wake Freeman aliwekeza sana kwenye Media na Social Media ndio the best political investment inayokibeba chama hicho sasa hivi wakati kikiwa almost mwisho wa uhai wake. Kuwekeza kwake kwa Vijana wenye msimamo na Media ndio kunakisaidia sana chama hicho kuendelea kupumua mpaka leo huku the Natural Fate ikiwa inakipa nafasi chama hicho nafasi ya kujikarabati ingawa Viongozi na Wanachama wengine wa Chama hicho wanashindwa kuielewa hiyo concept.
- Huu ni wakati muafaka wa Freeman kujiuliza kama je kuna nini ambacho bado hajakifanya katika uwezo wake wa kufikiri na kuongoza Upinzani, kwa sasa Chama hicho sio siri kimejipiga dhoruba kwa kamali ya kisiasa aliyoamua kuicheza yeye mwenyewe Freeman kwa niaba ya Chama chake na ndio maana ya Uongozi wa Taifa ni kwa Kiongozi kuwa na uwezo wa kuona mbali kwa niaba anaowaongoza. Chadema imefika mahali inahitaji ukarabati mkubwa sana na wa hali ya juu sana kuweza kurudi tena au kufikia zaidi ya kilipokuwa huko nyuma. Chadema haina agenda yoyote tena zaidi ya kusubiri Viongozi wa CCM wakosee herufi na maneno na kuanza kuyarudia rudia kama utani badala ya hoja nzito kwa Umma ambao ulifikia hatua ya kuwaamini sana nyakati fulani zilizopita. toka Utawala mpya wa Awamu ya Tano ya CCM ushike madaraka Chadema imepwaya mno ni kawaida kwenye siasa za Kitaifa ni kama chama cha Democrats huko USA na wao sasa hivi wanakabiliwa na wakati kama huu wa Chadema ni wakati unaohitaji Viongozi wake wa juu kujitafakari upya kama kweli wapo sawa na wanachohitajika kukifanya yaani Upinzani.
- Kutumia muda mwingi kuwashambulia kwa maneno ya mafumbo mafumbo na lugha zisizokuwa za kistaarabu siamini kama inaweza kuisaidia Chadema kurudi kwenye mstari wake wa kuaminiwa na Wananchi kama ilivyokuwa huko siku za nyuma. Binafsi ninakubaliana sana na maneno ya Mwenyekiti Mao Tse tung kuwa...... "Ukiona binadam wawili wanakubaliana kwa kila kitu na kwa wakati wote ujue kwamba aidha Mmojawapo ni Mgonjwa au wote wawili sio wazima".....Historia ya Dunia inaonyesha Chama kimoja kikikaa madarakani kwa zaidi ya Miaka 50 huwa kunakuwa na tabia za kujisahau kwa chama hicho so kinahitaji kukumbushwa kumbushwa kurudi kwenye mstari so ni muhimu sana kuwepo kwa Upinzani nchini, lakini sio kwa huu upinzani uliopo sasa. Freeman amekisaidia sana Chadema sana, lakini Chadema ilipofikia sasa hivi nina wasi wasi ndio mwisho wa uwezo wake kufikiri kisiasa ni wakati muafaka akatafakari kama ni wakati wa kufanya maamuzi magumu sasa au kuja kujutia baadaye.
- MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
Le Mutuz Nation