Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,472
- 215,292
Taarifa za Kidunia zinaonyesha kwamba huyu ndiye kiongozi wa kisiasa mwenye kuheshimika zaidi duniani kwa sasa , ndiye mwanasiasa anayeongoza kwa siasa za kistaarabu , ni mvumilivu asiye na kisasi hata kwa watesaji wake waliojiapiza hadharani na gizani kumshughulikia.
Huyu ndio Mwanasiasa aliyefirisiwa na kudhulumiwa kuliko yeyote barani Africa , ambapo wote waliosaidia kudhulumiwa kwake ama wamepandishwa cheo au wamefutiwa mashitaka yao ya ufisadi , RC wa Mtwara na Mh Mchechu ni miongoni mwa wanufaikaji wa mateso ya Mbowe , Huyu Mbowe Taarifa mpya zinaonyesha kwamba ndiye mwanasiasa aliyetukanwa zaidi katika historia ya siasa za Tanzania , huyu ametukanwa hata na watu waliokuwa hohehahe aliowaokota majalalani na kuwapa maisha akiwemo Mwita Waitara aliyeokotwa na Chadema baada ya kukimbia UVCCM alikopangiwa kuwa mpika chai wa Nchimbi aliyekuwa mwenyekiti wa UVCCM Taifa ( hii ni kwa mujibu wa kauli ya Waitara mwenyewe )
Ni mwanasiasa wa kizazi kipya asiyetishwa wala kuyumbishwa na wenye mamlaka , ni miongoni mwa wanasiasa wachache wa Tanzania WANAOFAHAMISHWA MAPEMA JUU YA NJAMA DHIDI YAO , lakini haogopi , hii imejidhihirisha hata alipofungwa jela miezi minne bila hata kuhukumiwa kifungo na Mahakama , ni miongoni mwa Magwiji wa siasa nchini Tanzania na sasa Africa na duniani , wengi wanamfananisha na kizazi cha akina Nelson Mandela na Kwame Nkurumah .
Hii ni tunu ya Dunia