Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe amesema baada ya kuzuiliwa mikutano ya hadhara kwa hila chama hicho kimeimarika maradufu.
Akihutubia mkutano mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema katija ukumbi wa Mlimani City kiongozi huyo amesema chama hicho kiliamua kufanya siasa mpya za kuzunguka kata zote nchini kuandikusha wanachama na kufanya mikakati ya ndani.
Mbowe amesema chama hicho hakitamani tena siasa za mikutano ya hadhara kwani wamegundua mikutano ya ndani ndiyo njia muhimu zaidi ya kujijenga kwani kuna uhalisia na unaweza kupima matokeo
Katika hatua nyingine Mbowe ametangaza rasmi idadi ya wanachama wa Chadema wenye kadi na kusema imefikia milioni 6.
Mbowe amesema chama kina database ya wanachama wote milioni 6 kwamba wapo wapi na jinsia yao ikiwemo idadi ya vijana,wazee,watoto,wanawake na wanaume.
Muda wote Mbowe alikuwa anashangiliwa kwa shangwe na mayowe na wanawake hao Bawacha kiasi kwamba wakati mwingine hotuba yake ilikuwa haisikiki vyema kwa kushangiliwa.
Kiongozi huyo wa Chadema amesema pia chama hicho siku ya mkutano mkuu tarehe 18 Dec kitazindua rasmi program ya chama ijulikanayo kama CHADEMA DIGITAL.Katika program hiyo wanachama watatumia simu zao kupata taarifa zote za chama na pia kulipia ada za uanachama.Pia Mbowe amesema ataliomba Baraza Kuu kuidhinisha ada ya uanachama kuwa shilingi elfu 2 badala ya elfu 1 kwa mwaka.
Akihutubia mkutano mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema katija ukumbi wa Mlimani City kiongozi huyo amesema chama hicho kiliamua kufanya siasa mpya za kuzunguka kata zote nchini kuandikusha wanachama na kufanya mikakati ya ndani.
Mbowe amesema chama hicho hakitamani tena siasa za mikutano ya hadhara kwani wamegundua mikutano ya ndani ndiyo njia muhimu zaidi ya kujijenga kwani kuna uhalisia na unaweza kupima matokeo
Katika hatua nyingine Mbowe ametangaza rasmi idadi ya wanachama wa Chadema wenye kadi na kusema imefikia milioni 6.
Mbowe amesema chama kina database ya wanachama wote milioni 6 kwamba wapo wapi na jinsia yao ikiwemo idadi ya vijana,wazee,watoto,wanawake na wanaume.
Muda wote Mbowe alikuwa anashangiliwa kwa shangwe na mayowe na wanawake hao Bawacha kiasi kwamba wakati mwingine hotuba yake ilikuwa haisikiki vyema kwa kushangiliwa.
Kiongozi huyo wa Chadema amesema pia chama hicho siku ya mkutano mkuu tarehe 18 Dec kitazindua rasmi program ya chama ijulikanayo kama CHADEMA DIGITAL.Katika program hiyo wanachama watatumia simu zao kupata taarifa zote za chama na pia kulipia ada za uanachama.Pia Mbowe amesema ataliomba Baraza Kuu kuidhinisha ada ya uanachama kuwa shilingi elfu 2 badala ya elfu 1 kwa mwaka.