MdogoWenu

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
555
915
Baada ya upekuzi wa Polisi kukamilika nyumbani Kwa M.Kiti Mbowe, tumepokea taarifa za kushtua na kushangaza kuwa Polisi wamemwambia kuwa ataunganishwa kwenye kesi ya Ugaidi na watuhumiwa walioko gereza mojawapo DSM. Tutaendelea kutoa taarifa za kina hapo baadaye.

Screenshot 2021-07-22 at 08.56.30.png


====

UPDATES;

=====

TAARIFA KWA UMMA

JESHI LA POLISI LAMTUHUMU MWENYEKITI WA CHAMA
MHE.FREEMAN MBOWE NA "MAKOSA YA UGAIDI"

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe. Freeman Mbowe alifikishwa Dar es Salaam jana majira ya saa tatu usiku chini ya ulinzi wa Polisi , walimpeleka nyumbani kwake Mikocheni Kwa ajili ya kumfanyia upekuzi ambao ulichukua takribani saa mbili na nusu.

Baada ya upekuzi huo Polisi waliondoka na Kompyuta mpakato (Laptop) na Vishikwambi (tablets) za watoto wake, Kompyuta mpakato moja ya kwake na modem ya Internet Kwa ajili ya uchunguzi wao.

Leo majira ya saa Saba mchana Polisi walimfikisha Mhe. Freeman Mbowe Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano na kuchukua maelezo yake.

Polisi walitaka maelezo kutoka Kwa Mhe. Freeman Mbowe kuhusiana na kosa waliloliita 'KULA NJAMA ZA KUTENDA KOSA LA UGAIDI'

Baada ya maelezo hayo ya Polisi Mhe. Freeman Mbowe alitumia haki yake ya kisheria na aliamua kutokutoa maelezo yoyote Polisi kwa mujibu wa Sheria. Baada ya maelezo hayo Polisi wamemrejesha Mhe. Freeman Mbowe katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay ,Jijini Dar es Salaam.

Aidha , viongozi wengine waliokuwa wanashikiliwa Mkoani Mwanza wameendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi na baadhi yao walifanyiwa upekuzi nyumbani kwao na vyumba vya hotel ambako walikuwa wameshukia .

Waraka wa Mbowe kwa Watanzania
Mwenyekiti Taifa Mhe. Freeman Mbowe ametuma waraka kwa Watanzania kama ifuatavyo;
"Hatimaye madai ya Katiba Mpya yamenisababishia kesi ya ugaidi, nipo tayari kwa mashtaka ya kuchongwa siogopi. Ninaamini Dunia itaujua ukweli wa kile kinachoendelea Tanzania na kile tunachokipitia Watanzania. Lakini pia itajua ukweli juu ya makosa haya ya kuchongwa.

Natoa wito kwa watanzania kuendeleza mapambano, haki hutafutwa” Mhe.
Freeman Mbowe.”

Imetolewa leo Alhamisi tarehe 22 Julai, 2021.

John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

=====

UPDATE:

2DC622DC-FB08-4FF3-8334-A53920A56AA3.jpeg

887CD98B-45D9-48ED-9BC3-EBCC22235398.jpeg
 
Ukishika mkia wa mnyama mkali lazima akushughulikie. Ukikaribishwa sebuleni usifanye haraka kutaka kuingia chumbani bali subiri ukaribishwe chumbani baadaye.

Vingenevyo unaweza ukafikiriwa kwamba wewe ni mwizi kumbe siyo. Hekima inatakiwa unapotekeleza- mikakati ya kukabiliana na adui/mshindani wako. Amemlazimisha mama kwenda maili nyingi. Ajiandae !
 
samia afanye udikteta tu lakini mashirika ya Kimataifa na Nchi za wafadhili zikiamua kutotoa mikopo na misaada kutokana na nchi kukosa demokrasi hapo ndiyo Watanzania watatia akili kichwani kwani ugumu wa maisha utaongezeka mara tatu ya ilivyo sasa na Serikali itakuwa haina jinsi bali kupitisha fagio la chuma Serikalini litakalosomba Wafanyakazi wengi sana.

Ukishika mkia wa mnyama mkali lazima akushughulikie. Ukikaribishwa sebuleni usifanye haraka kutaka kuingia chumbani bali subiri ukaribishwe chumbani baadaye. Vingenevyo unaweza ukafikiriwa kwamba wewe ni mwizi kumbe siyo. Hekima inatakiwa unapotekeleza- mikakati ya kukabiliana na adui/mshindani wako. Amemlazimisha mama kwenda maili nyingi. Ajiandae !
 
samia afanye udikteta tu lakini mashirika ya Kimataifa na Nchi za wafadhili zikiamua kutotoa mikopo na misaada kutokana na nchi kukosa demokrasi hapo ndiyo Watanzania watatia akili kichwani kwani ugumu wa maisha utaongezeka mara tatu ya ilivyo sasa na Serikali itakuwa haina jinsi bali kupitisha fagio la chuma Serikalini litakalosomba Wafanyakazi wengi sana.
Hata mahakama ya uhalifu wa kimataifa ICC sasa wanaanza kuangazia hilo taasisi za haki za binadamu zote wameona uonevu mateso waliofanyiwa wananchi kule mwanza, hii inaenda kumletea chuki kubwa Mama na itaharibu mazuri machache aliyokuwa kaanza kuyafanya
 
samia afanye udikteta tu lakini mashirika ya Kimataifa na Nchi za wafadhili zikiamua kutotoa mikopo na misaada kutokana na nchi kukosa demokrasi hapo ndiyo Watanzania watatia akili kichwani kwani ugumu wa maisha utaongezeka mara tatu ya ilivyo sasa na Serikali itakuwa haina jinsi bali kupitisha fagio la chuma Serikalini litakalosomba Wafanyakazi wengi sana.
Nani kakudanganya vyama vya upinzani ni CHADEMA? mnajiita chama kikuu cha upinzani na hamna hata wabunge, chama cha upinzani kinacholazimisha vurugu ambazo wananchi hawaziungi mkono wafadhili gani hao wataokisikiliza?

kama JPM licha ya kuwakalia kooni na kuingilia maslahi yao hao mabeberu bado akihitaji mkopo walimpa sembuse huyu mama alowalegezea?
 
Pesa ya walipa kodi zinatumika hovyo kukandamiza demokrasia kwa njia haramu za kishetani, wametumia gharama kubwa kumsafirisha mbowe tokea mwanza hadi huko Dsm kwenda kusachi nyumbani kwake ni Aibu iliyoje
 
Washauri wa mama huenda wamepanga njama za kumharibia lakini yeye hajajua undani wake kaingia mkenge kiwepesi sasa jumuia za kimataifa zitamlaani vikali sana
Akitaka kuharibikiwa ni aende tu kinyume cha JPM, sisi the majority tulimchagua JPM na hulka yake na si kwamba hatukujua tunachagua mtu wa namna gani, hilo mnalifahamu vyema na ndo maana mkaanza kumwingiza mother mkenge ili achukiwe na wafuasi wa JPM ambao ndo the majority ya wapiga kura mkitegemea wapige kura za hasira 2025, mama kashtuka ngoja awanyooshe..
 
Nani kakudanganya vyama vya upinzani ni CHADEMA? mnajiita chama kikuu cha upinzani na hamna hata wabunge, chama cha upinzani kinacholazimisha vurugu ambazo wananchi hawaziungi mkono wafadhili gani hao wataokisikiliza? kama JPM licha ya kuwakalia kooni na kuingilia maslahi yao hao mabeberu bado akihitaji mkopo walimpa sembuse huyu mama alowalegezea?
Vurugu zipi? Wananchi wapi unawasemea? Hivi Unafikiri wananchi ni wapumbavu kama wewe? Wananchi wanaona wanaujua ukweli acha kuendekeza njaa zako kujinufaisha kupitia uonevu unyanyasaji uovu mateso ya kishamba kwa chadema
 
Akitaka kuharibikiwa ni aende tu kinyume cha JPM, sisi the majority tulimchagua JPM na hulka yake na si kwamba hatukujua tunachagua mtu wa namna gani, hilo mnalifahamu vyema na ndo maana mkaanza kumwingiza mother mkenge ili achukiwe na wafuasi wa JPM ambao ndo the majority ya wapiga kura mkitegemea wapige kura za hasira 2025, mama kashtuka ngoja awanyooshe..
Uchaguzi upi ulimchagua magufuli? Mwananchi yupi? Kura zipi? Tume upi? Hakuna uchaguzi Tanzania kilichofanyika ni CCM kuulawiti kuubaka kuunajisi uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani tu
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom