Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,220
- 9,647
Ndugu zangu mchana kutwa sikuingia humu jukwaani kwa kuwa nilikuwa katika mapambano ya maisha kama kijana, ndugu zangu nimeiona na kushtuka Sana video inayomuonesha mh Mbowe akitutukana watanzania kuwa sisi ni wajinga, nimesikitika sana ndugu zangu kwa dharau zake Mbowe kwetu watanzania.
Ndugu zangu yaani Mbowe anatutukana watanzania kisa tu tumeamua kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe? Kwamba Mh. Mbowe haoni namna moyo na uamuzi huo wa kuamua kujenga nchi yetu ulivyosaidia kusogeza huduma muhimu kwa mwananchi.
Kwamba Mbowe haoni namna jambo hilo lilivyosaidia watoto wa wanyonge kupata elimu bila shida kwa kwenda shule kwa wakati baada ya kuwa madarasa yamejengwa na kukamilika kwa wakati?
Kwamba mh Mbowe anafikiri sisi watanzania ni vipofu kwamba hatuoni namna kwa sasa ambavyo huduma za maji umeme na hata miundombinu ilivyoboreshwa na kusogezwa kwa mwananchi?
Kwamba mh Mbowe anadhani sisi wote watanzania tuna mapesa mengi Kama yeye? Anadhani sote tutakwenda Ulaya kusoma au kutibiwa, anadhani na sisi tutakuwa na madaktari binafsi?
Anataka nani atujengee nchi yetu, anataka nani awajibike kwa niaba yetu katika kubeba mzigo wetu, anataka tuijenge nchi yetu kwa madeni? Anataka tuijenge kwa misaada? Je hiyo mikopo na misaada tutaipokea hadi lini? Tutalipa madeni hadi lini? Kwamba hata matundu ya vyoo tukakope na kusubiri misaada itufikie? Je wakati huo wanafunzi watakuwa wanatumia nini? Au watapanga foleni kusubiri matundu yaje kwa ndege?
Kwanini asipongeze juhudi za Mh. Rais wetu kuongoza njia katika kuijenga nchi yetu kwa kujitegemea wenyewe? Kwa nini asimuunge mkono Rais katika kuhakikisha tunapunguza mzigo wa madeni kwa nchi yetu, anataka tukope mpaka tuweke rehani vitu vyetu, anataka tukope mpaka tushinde tunafanya kazi ya kulipa tu madeni bila kufanya maendeleo.
Watanzania tunasema kuwa sisi siyo wajinga, siyo wajinga watanzania, tumeamua kuijenga nchi yetu wenyewe, tumeamua kubebaa mzigo wetu wenyewe, tumeamua wajibu wetu uwe juu ya mabega yetu, tumeamua kuwa acha tuumie leo lakini tufaid matunda yake kesho, tumeamua vizazi vijavyo vijuwe kuwa kuna kizazi kilipita na kilikuwepo ambacho kilitekeleza wajibu wake vyema ili wao waishi vizuri.
Mh. Mbowe atuache tuijenge nchi yetu, asitukatishe tamaa maana tumeamua kusonga mbelee, atupishe mbele katika kuibeba nchi yetu,tupo katika kuipambania nchi yetu kuhakikisha inasimama na kupigiwa mfano.
Ombi langu na ushauri wangu kwa Mh. Rais wetu Kama kijana wake mtanzania napenda kumwambia kuwa asikatishwe tamaa Wala kuvunjika moyo, tumeona juhudi zake na tupo tunamuunga mkono ,maana kazi zake zimegusa maisha yetu watanzania, Mh. Rais wetu mpendwa songa mbele bila hofu wananchi tupo nawewe bega kwa bega.
Ndugu zangu yaani Mbowe anatutukana watanzania kisa tu tumeamua kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe? Kwamba Mh. Mbowe haoni namna moyo na uamuzi huo wa kuamua kujenga nchi yetu ulivyosaidia kusogeza huduma muhimu kwa mwananchi.
Kwamba Mbowe haoni namna jambo hilo lilivyosaidia watoto wa wanyonge kupata elimu bila shida kwa kwenda shule kwa wakati baada ya kuwa madarasa yamejengwa na kukamilika kwa wakati?
Kwamba mh Mbowe anafikiri sisi watanzania ni vipofu kwamba hatuoni namna kwa sasa ambavyo huduma za maji umeme na hata miundombinu ilivyoboreshwa na kusogezwa kwa mwananchi?
Kwamba mh Mbowe anadhani sisi wote watanzania tuna mapesa mengi Kama yeye? Anadhani sote tutakwenda Ulaya kusoma au kutibiwa, anadhani na sisi tutakuwa na madaktari binafsi?
Anataka nani atujengee nchi yetu, anataka nani awajibike kwa niaba yetu katika kubeba mzigo wetu, anataka tuijenge nchi yetu kwa madeni? Anataka tuijenge kwa misaada? Je hiyo mikopo na misaada tutaipokea hadi lini? Tutalipa madeni hadi lini? Kwamba hata matundu ya vyoo tukakope na kusubiri misaada itufikie? Je wakati huo wanafunzi watakuwa wanatumia nini? Au watapanga foleni kusubiri matundu yaje kwa ndege?
Kwanini asipongeze juhudi za Mh. Rais wetu kuongoza njia katika kuijenga nchi yetu kwa kujitegemea wenyewe? Kwa nini asimuunge mkono Rais katika kuhakikisha tunapunguza mzigo wa madeni kwa nchi yetu, anataka tukope mpaka tuweke rehani vitu vyetu, anataka tukope mpaka tushinde tunafanya kazi ya kulipa tu madeni bila kufanya maendeleo.
Watanzania tunasema kuwa sisi siyo wajinga, siyo wajinga watanzania, tumeamua kuijenga nchi yetu wenyewe, tumeamua kubebaa mzigo wetu wenyewe, tumeamua wajibu wetu uwe juu ya mabega yetu, tumeamua kuwa acha tuumie leo lakini tufaid matunda yake kesho, tumeamua vizazi vijavyo vijuwe kuwa kuna kizazi kilipita na kilikuwepo ambacho kilitekeleza wajibu wake vyema ili wao waishi vizuri.
Mh. Mbowe atuache tuijenge nchi yetu, asitukatishe tamaa maana tumeamua kusonga mbelee, atupishe mbele katika kuibeba nchi yetu,tupo katika kuipambania nchi yetu kuhakikisha inasimama na kupigiwa mfano.
Ombi langu na ushauri wangu kwa Mh. Rais wetu Kama kijana wake mtanzania napenda kumwambia kuwa asikatishwe tamaa Wala kuvunjika moyo, tumeona juhudi zake na tupo tunamuunga mkono ,maana kazi zake zimegusa maisha yetu watanzania, Mh. Rais wetu mpendwa songa mbele bila hofu wananchi tupo nawewe bega kwa bega.