mayowela
JF-Expert Member
- Nov 2, 2014
- 2,124
- 1,745
Fred Fidelis aka Fredwaa
Kipindi cha Powe breakfast kimepwaya sana kama sio kupoa, kwa muda wa alfajiri kuanzia saa11 mpaka 12, amsha amsha za Fredwaa hazipo, Utabiri wa Hari ya hewa hamna, Paza Sauti pamoja na Ripoti ya Bonge ya alfajiri hakuna.
Pia zile reggae za alfajiri siku ya Ijumaa hakuna, sasa huyu jamaa ni likizo tu au kuna lingine nyuma ya pazia, imekuwa muda sana hayupo kwenye Kipindi, Inaleta shaka flani kama jamaa kapiga chini hivi, post yake kwenye akaunti ya Instagram siku mbili zilizopita inanipa mashaka, inasema: "FORGIVE, FORGET and move on, everyone got history in their life".
Pia kituo kiko kwenye kampeni ya siku ya mwanamke, na karibu asilimia 90 ya staff wameweka picha ambayo inatangaza kampeni hiyo ila yeye sijaona hiyo kitu.
PM Mr Shafii Dauda fanyeni mpango huyu jamaa arudi, tunajua kwenye riziki yoyote hapakosi husda kama ni hivyo basi weka sawa, kama ni likizo basi wasikilizaji wa kipindi wajuzwe, tumemiss sauti, jingle, drops za Mr Energy Man, hakuna kama yeye hapo.
UPDATES: Huyu bwana ni mwezina wiki kadhaa sasa bila kusikika masikioni mwa watu, duru zinasema mfumo umemkataa yeye pamoja na mwenzie wa Kunduchi ndio alizingua balaa na pendo lake tayari linakaribia kupata mzibaji, yote heri watumie vipaji vyao kufanya mengine