fasiliteta
JF-Expert Member
- Jul 2, 2014
- 2,165
- 3,655
Wachaga pia ni wezi,tunawajua wala huna haja ya kupiga tilalila saaana.Nilioa uchagani sijutii kabisa. Mungu alinipa mke ambaye kwa umoja wetu tuliufuta umaskini wangu na ndugu zangu. Kuna siku nilisema hapa kuwa baada ya Mimi kuoa mchagga na rafiki zangu na ndugu wakashuhdia maisha yetu mazuri mno ya kuelewana na upendo basi ndugu zangu wa kuzaliwa tumbo Moja wote tumeoa wachagga. Ndugu wa ukoo wengi wameoa wachagga. Best friends zangu nao walioa wachagga. Kifupi sote tulioa wachagga tumebadili kila kitu kimaisha na kijijini tutokapo. Wazee wangu kabla ya kufariki walituita wakaomba kuwa sote tumuite mke wangu "Mama". Hivyo mke wangu haitwi Wifi wala shemeji. Na Mimi ninamuita mama na simkumbuki siku nimemuita kwa jina lake. Mungu akubariki mama Bahati
Endeleeni kuwabeza wachagga Ila niseme tu Wachagga ni taifa lingine kabisa. Tena kwa sasa vijiji uchagani utafikiri ni Miji mikubwa. Hata maisha ni kama mjini mpaka hata mapishi Yao.