Freddie Mercury na Magic Johnson

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,787
30,080
FRED MERCURY NA MIMI NA MAGIC JOHNSON NA MIMI

Ilikuwa katika miaka ya mwanzoni ya 1990 naishi mji mmoja mdogo Uingereza unaitwa Cardiff.

Nyumba ninayoishi ni ya wanafunzi na jirani yangu anakaa gorofa ya juu yangu ni kijana wa Kigiriki anaitwa Panothiakis George Foundas.

Mdogo sana kwa umri kwangu.

Baba yake huyu kijana, Giorgos (George) Foundas ni mmoja wa waigizaji maarufu duniani katika miaka ya 1960s viwango vya Anthony Qinn na Irene Papas.

George Foundas alicheza movie, ''Zorba the Greek,'' na Anthony Quinn na Irene Papas mwaka wa 1964.

Panos kama tulivyopenda kumwita alinipenda toka siku ya kwanza aliponiona naingia nyumba ile.

Akinihurumia kuwa mimi "siishi."
Weekend niko ndani.

Siku za kawaida niko ndani.

Anashangaa kwa nini sichezi mchezo wowote wala hajaniona kwenye lile ''discotheque,'' ambalo Panos ananiambia vijana kutoka Greece muziki ukinoga wanavunja sahani.

Akanieleza kuwa hiyo ni mila ya kwao Ugiriki kuwa muziki ukikolea wanavunja sahani.

Panos ana msichana wake Mwingereza akimtembelea basi atamleta kwangu aje apige keyboard organ yangu.

Mimi na Panos tukawa marafiki wakubwa.

Siku moja jioni nasikia mlango wangu unagongwa kwa kishindo utadhani nyumba inawaka moto.

Kumfungulia Panos anaingia ndani anatweta.

"Mohamed Fred Mercury is dead."
"Who is Fred Mecury?"

Namuuliza kwa kuwa sijapata kusikia jina hilo.
Panos kachoka kuwa mimi simjui Fred Mercury ilhali kazaliwa Zanzibar na usitoshe a ajulikane dunia nzima.

Siku nyingine tena kanibishia hodi kunipa, "Breaking News," kutoka BBC taarifa za Magic Johnson kuwa kakutwa na virusi vya UKIMWI.

Nikamuuliza, "Who is Magic Johnson?"

Nina hakika hapo ndipo alipojihakikishia pasi na shaka yoyote kuwa mimi hakika sina moja nilijualo ulimwenguni.

Picha ya kwanza ni Fred Mecury akiwa mtoto na yaya wake wako Zanzibar na pcha ya pili kulia ni Giorgos Foundas baba yake rafiki yangu Panos na huyo mwingine ni Anthony Quinn.

Screenshot_20211120-223359_Chrome.jpg
 
Story ya Freddie Mercury niliifuatilia Youtube miaka michache iliyopita,alipendwa sana na mwanamke fulani ila akamkataa na kwenda kufanya michezo ileee mwisho akapata Ukimwi na kufa
inasikitisha
 
Sijaisoma yote ila si unajua Mercury alikuwa shoga na alikufa kwa ukimwi?!

Maana kwa uandishi wako uliozoeleka humu unaweza kuficha weaknesses zake kwa sababu tu alikuwa mwenzako kiimani!
 
Sijaisoma yote ila si unajua Mercury alikuwa shoga na alikufa kwa ukimwi?!

Maana kwa uandishi wako uliozoeleka humu unaweza kuficha weaknesses zake kwa sababu tu alikuwa mwenzako kiimani!
Saint Anno,
Fred Mercury hakuwa Muislam.

Umepata kusoma chochote kutoka kwangu cha kumdhalilisha mtu?

Uandishi una sheria na adabu zake.
Mathalan wewe umeandika jambo usilolijua.

Haitakiwi kufanywa hivyo.
 
Story ya Freddie Mercury niliifuatilia Youtube miaka michache iliyopita,alipendwa sana na mwanamke fulani ila akamkataa na kwenda kufanya michezo ileee mwisho akapata Ukimwi na kufa
inasikitisha
Ina maana Freddie Mercury alikuwa shoga? Kama ni kweli,je, alikuwa too au bottom?
 
Ina maana Freddie Mercury alikuwa shoga? Kama ni kweli,je, alikuwa too au bottom?
Alikua bottom hiyo inajulikana na mume alikua nae kabisa na mabasha kadhaa yaani ms enge malaya.akishakula miunga anagongwa mpk vyooni.
Hela alikua nayo so mibazazi ya mtelemko ikawa inampelekea moto tu mzanzibara yule.
 
Alikua bottom hiyo inajulikana na mume alikua nae kabisa na mabasha kadhaa yaani ms enge malaya.akishakula miunga anagongwa mpk vyooni.
Hela alikua nayo so mibazazi ya mtelemko ikawa inampelekea moto tu mzanzibara yule.
Aisee,inasikitisha Sana,nimepata kufahamu mwezi Jana na bendi yake ya Queens kumbe alikuwa na hiyo changamoto.Ndo maana alibadili hadi jina lake la asili.Dunia ina mambo sana hii.
 
dooh!!!!!hatwareeeeeeeee.....i didnt know about the meaning of the those two words..(too or bottom).....now i know..
 
Nilidhani waliambukizana UKIMWI!!! Ila Mercury alikuwa anaimba si utani. "I want it all, hey hee. I want it all, and i want it now."

Umeicheki movie ya maisha yake? Inaitwa Bohemian Rhapsody imechezwa na Muegypt/mmarekani Rami Malek.
 
Aisee,inasikitisha Sana,nimepata kufahamu mwezi Jana na bendi yake ya Queens kumbe alikuwa na hiyo changamoto.Ndo maana alibadili hadi jina lake la asili.Dunia ina mambo sana hii.
Alichange jina ili apate stage name inayokubalika.
 
Nilidhani waliambukizana UKIMWI!!! Ila Mercury alikuwa anaimba si utani. "I want it all, hey hee. I want it all, and i want it now."

Umeicheki movie ya maisha yake? Inaitwa Bohemian Rhapsody imechezwa na Muegypt/mmarekani Rami Malek.
Kwa hyo kwenye I want it all alikuwa analilia mkuyenge!
 

Similar Discussions

8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom