Fred Mpendazoe: Uchumi wa nchi umo mikononi mwa familia tisa za matajiri!

MISHAHARA- walimu 200000/= - Madaktari 957000/=+marupurupu kidogo - Wabunge 2700000/=+ Shangingi+allowance nyingi SABABU- Walimu ni wengi kuliko madaktari na madaktari ni wengi kuliko wabungeMIKOPO VYUO VIKUU-wanafunzi sayansi -FIRST PRIORITY (100%) - wanafunzi wengine-NON PRIORITY (unreliable) SABABU -Tuna wanafunzi na wataalamu wachache wa sayansi kuliko wengineITIKADI YA TAIFA- Ubepari (Capitalism) ni mzuri kwa maendeleo yetu hasa ubinafsishaji na uwekezaji kutoka nje. Ujamaa ( Socialism) umepitwa na wakati na hautufai kwa nchi yetu ambayo wengi wetu ni wavivu. SABABU- Ubepari rasilimali nyingi huwa mikononi mwa wachache lakini Ujamaa rasilimali ni za woteMITAZAMO YA WATU- watu wachache: Tanzania ni nchi yenye maziwa na asali watu wengi : Tanzania ni kana jangwani kusikokuwa na maji,chakula wala matumaini yoyote. watu wachache: Tunajivunia kuwa watanzania watu wengi : Tunavumilia kuwa watanzania UKWELI -mkiwa wachache mtanufaika lakini mkiwa wengi mtajuta MTAZAMO WANGU-walimu wangekuwa wachache kuliko wabunge wangelipwa mishahara mikubwa kuliko wabunge SWALI- Je, mlio katika kundi la watu wengi mnaweza kuamia kwenye kundi la watu wachache hili na nyinyi mnufaike?
 
Observation yako inaweza kuwa sahihi to some extent na unaonekana unapigania usawa kwa watu wote, hilo naungana na wewe pamoja na hakuna mtu mwenye akili timamu asiyeona inbalance katika suala la mishahara na marupurupu na stahiki zingine, sasa mwana JF unatakiwa uje na solution au majawabu kulalamika na kukandamiza keyboard kila siku hakuna kitakachobadilikazaidi ya keyboard yako kuchakaa na vidole kuwa na sugu, ni muda wa kuleta mada na majawabu yake sio kulalamika tu hapana,mimi jawabu nalaliona ni katiba mpya na uchaguzi wa 2015,. popote ulipo toa elimu ya uraia kwa wananchi, waonyeshe matatizo yanayowakabili, chanzo cha hayo matatizo na njia mbadala za kupata majawabu, ikifika 2015 tuamue kama taifa tuendelee kuoga kwa tope lilelile au sasa tuoge maji safi na mapya!
 
Te te teheee..! Eti Chenge na mafisadi wenzake wameshikilia uchumi!! Unachekesha kweli, hao wanahujumu uchumi. Pombe, sigara na kodi zetu ndo zinashikilia uchumi na kuendesha nchi. Topic na content bila bila
 
Jamani, hapa wataalam wa uchumi wanaweza kutuongoza katika kutengua kitendawili hiki. Kwa ufahamu wangu kiduchu nilionao katika eneo hili ni kwamba haweza kujua hizi familia tisa kwa majina. Ni mahesabu tu ya kiuchumi ambayo hutoa idadi ya watu wanaokuwa wanashikiria sehemu (asilimia) fulani ya uchumi katika nchi. Sasa mtu akitaka kwenda beyond that LABDA anaweza kufanya research yake yenye lengo la kuwafahamu kwa majina. Lakini mchakato mzima wa kuuchambua uchumi na kubaini usawa wa umiliki wa uchumi katika nchi ataishia tu hapo kujua idadi lakini ni zipi kwa majina kinabaki kitendawili.

Kwa mchumi baada ya kufahamu idadi ya wamiliki wa uchumi katika nchi jukumu linalofuata ni kuona ni namna gani ya kufanya uchumi huo umilikiwe na wananchi walio wengi zaidi
 
Back
Top Bottom