Form VI Leavers na maendeleo ya Jamii

Quemu

JF-Expert Member
Jun 27, 2007
984
127
Hivi karibuni nimekuwa najiuliza ni vipi nchi yetu inaweza kushirikisha vijana waliomaliza Form VI katika maendeleo ya jamii. Vijana wamalizapo Form VI huwa wana gap ya zaidi ya miezi nane kabla hawajapata nafasi ya kujiunga vyuoni kwa masomo ya juu. Sasa je, tunawezaje kuwashirikisha vijana hawa kwenye maendeleo chanya ya jamii, badala ya kuwaacha wamezubaa tu majumbani wakisubiri muda wa kwenda vyuoni?

Mpaka mwanzoni mwa miaka ya tisini, watahiniwa hawa walikuwa wanakwenda kwenye mandatory army service. Lakini kwa sababu zilizotolewa wakati huo (sizikumbuki), hii service ilikuja kuvunjwa. Matokea yake, vijana wengi hawa wameishia kurandaranda tu mitaani, wakisubiri nafasi za kujiunga vyuoni.

Sasa basi, kwa sababu tuna institutions nyingi mno kwenye jamii ambazo zinahitaji marekebisho ya hapa na pale. Na kwa sababu mahitaji haya hayako kwenye priorities za serikali yetu. Na kwa sababu tuna vijana ambao pengine wana nguvu na muda wa kuanza kulitumikia taifa, kwa hiyo…..

Ningeshauri serikali ianzishe programs ndogo ndogo ambazo zitawahamasisha vijana hawa kujihusisha na ujenzi wa jamii (community service programs). Natumia neno “jamii” badala ya “taifa” kwa sababu lengo ni kuanzisha programs ambazo zitawashirikisha vijana hawa kwenye ujenzi wa institutions zinazowazunguka. Of course, jamii ndio taifa lenyewe hilo.

Mfano, kuna institutions kama shule na hospitali/zahanati ambazo zinahitaji marekebisho ya mara kwa mara. Shule mara nyingi zinahitaji upanuzi na ukarabati wa madarasa (ujenzi, upigaji rangi, utengenezaji wa mazingira, n.k.), pamoja na utengenezaji wa madawati, ubao wa kuandikia na vifaa vingine muhimu. Hospitali/zahanati huwa zinahitaji upanuza na ukarabati wa majengo, pamoja na utengezanaji wa vitanda vya wagonjwa na vifaa vingine muhimu.

Sasa basi, kinachotakiwa kufanyika ni kutumia muda na nguvu za vijana hawa katika utekelezaji wa ujenzi wa institutions hizo. Mimi ningependekeza muswada ambao utatunga sheria ambayo itakuwa ni mandatory kwa Form VI Leavers wote kujishirikisha kwenye community service programs kama nilizozitaja hapo juu. Vijana hawa watapaswa kutumia muda wao (kati ya miezi 3 – 6) kushiriki kwenye community services katika jamii zinazowazunguka. Mfano, vijana wanaomaliza kidato cha sita kwenye shule zilizopo wilaya ya kinondoni, watalazimika kujishirikisha kwenye ukarabati wa institutions zilizoko kwenye wilaya hiyo.

Kwa kutumia njia hii, tutaona kwamba institutions nyingi katika jamii zitakuwa kwenye hali mzuri muda wote. Hii itasaidia kuondoa ukiritimba unaosababishwa na kusubiri huduma za serikali (ngazi zote) katika jamii zetu.

Jamani naomba kuwasilisha!

(NB: Nimejaribu kutafuta njia ya kufupisha bandiko hili, lakini nimeshindwa... Mtanisamehe)
 
Hii inaweza kuwa na mazao mazuri, ni moja ya mambo niliyoongelea katika issue ya "unemployment benefit" nikasema kama workforce yetu iko so unemployed / underemployed hatuwezi ku afford UB mpaka tuwe na production.

Huu utakuwa ni wakati mzuri wa kuwaweka sawa kwa workforce vijana na at the same time kufanya shughuli za uzalishaji.

Tatizo linakuja kwenye organisation, logistics na budget.

Nyerere alishawahi kusema kuwa kama nchi tajiri kama Marekani inatumia wanafunzi wake katika uzalishaji, sisi masikini hatuwezi ku afford kuiacha workforce hii.Kusema na kufanya ni vitu viwili tofauti though.
 
Tatizo linakuja kwenye organisation, logistics na budget.

Ni kweli Pundit, tatizo linaweza kuanzia kwenye hivi vitu vitatu muhimu.

Lakini kwenye maswala ya budget na financing, nilikuwa nafikiri kuwa public inaweza kuwa responsible na funding. Serikali inaweza ika introduce a special tax ambayo itakwenda kwenye mfuko wa programs hizi. Pia wananchi wenye uwezo wanaweza kuhamasishwa kuchangia kwenye mfuko huo.

Afterall, gharama itakuwa kwenye ununuzi wa vifaa vya programs pekee. Hakutakuwa na labor costs, kwa sababu vijana hawa watakuwa wanatoa huduma bila ya malipo.

Gharama za usafiri na other miscellaneous kwa vijana hawa zitakuwa zinatolewa na wazazi wao. Kwa hiyo, wazazi watakuwa pushed kuchangia financing kwenye hizi programs indirectly.

It can be done
 
Mimi ningependa zaidi kuona kazi hizi zinajiendesha kibiashara na hazitegemei kodi.

Serikali iweze kukopesha organization hii initially halafu kutoka hapo kila kitu kiendeshwe kibiashara.Hata kama vijana watalipwa kiasi kidogo watapata ujuzi na kujenga discipline.

JKT ilikuwa inafanikiwa kiuchumi in some isolated cases ukiondoa ukiritimba wa kijeshi. Tunaweza kurudisha kitu kama hicho, less militaristic.
 
Hongera kwa hoja nzuri sababu wakimaliza wengine wanaanza kuvuta bangi,umalaya nk
Tatizo hawa viongozi wa sasa watakwambia hakuna FEDHA
 
Mimi ningependa zaidi kuona kazi hizi zinajiendesha kibiashara na hazitegemei kodi.

Serikali iweze kukopesha organization hii initially halafu kutoka hapo kila kitu kiendeshwe kibiashara.Hata kama vijana watalipwa kiasi kidogo watapata ujuzi na kujenga discipline.

JKT ilikuwa inafanikiwa kiuchumi in some isolated cases ukiondoa ukiritimba wa kijeshi. Tunaweza kurudisha kitu kama hicho, less militaristic.

Swala la hizi programs kuendeshwa kibiashara linaweza kuzua matatizo mengine zaidi. Wamiliki hawatachelewa kuigeuza hizo programs for profit. Matokeo yake kutakuwa na ulipuaji wa hali ya juu kwenye ukarabati wa institutions.

Mimi nadhani kuna uwezekano mkubwa wa kuziendesha kwa kutumia public funds. Ninaamini wananchi watakuwa tayari kuchangia pindi wakiona kuna maendeleo kwenye hizo programs.

Kuhusu wazo la kodi maalum. Hizi kodi zinaweza kuwa imposed kwa local businesses kwenye wilaya husika. Kwa hiyo, badala ya wananchi kutozwa kodi hiyo, wafanyabiashara ndio wataingia burden ya ku-fund hizo programs.
 
Hongera kwa hoja nzuri sababu wakimaliza wengine wanaanza kuvuta bangi,umalaya nk
Tatizo hawa viongozi wa sasa watakwambia hakuna FEDHA

Ni kweli. Hizo programs sio tu zitawa keep busy, bali pia zitawasaidia kuwajenga kimalengo.

Tatizo hawa viongozi wa sasa watakwambia hakuna FEDHA

Na ndio maana ninashauri funds zitoke kwa public au local businesses.

Hata fedha zikiwepo zitafisadiwa!

Pundit,
Kama tukiogopa ufisadi kwa kila kitu, basi hatutaweza kwenda kokote. Ukweli ni kwamba, ufisadi Tz hautaondoka leo wala kesho. Kwa hiyo, inabidi tutafute mbinu za kudeal nao sambamba na kumove forward kimaendeleo. Tukisubiri mpaka uishe ndio tuanze shughuli za maendeleo, basi tutasubiri forever...
 
Hii inaweza kuwa na mazao mazuri, ni moja ya mambo niliyoongelea katika issue ya "unemployment benefit" nikasema kama workforce yetu iko so unemployed / underemployed hatuwezi ku afford UB mpaka tuwe na production.

Huu utakuwa ni wakati mzuri wa kuwaweka sawa kwa workforce vijana na at the same time kufanya shughuli za uzalishaji.

Tatizo linakuja kwenye organisation, logistics na budget.
Nyerere alishawahi kusema kuwa kama nchi tajiri kama Marekani inatumia wanafunzi wake katika uzalishaji, sisi masikini hatuwezi ku afford kuiacha workforce hii.Kusema na kufanya ni vitu viwili tofauti though.

Pesa zipo nyingi tu, kwani mabilioni ya Jk si yanaweza fanya kazi hii badala ya kuliwa na wajanja wachache?
 
Kinachotakiwa ni usimamizi, vitu vinaweza kuendeshwa kibiashara.Wananchi washachoka mikodi na michango left right and centre.

Market economy inatuondoa katika serikali kuwa na role ya ku hand out largesse kila pahali, serikali inatakiwa kuwa muangalizi tu.Tunaweza kuendesha vitu hivi kibiashara.

Kama unavyosema rightly kwamba hatuwezi kuogopa ufisadi kila sehemu kiasi cha kushindwa kuanzisha programs hizi (by the way the comment was meant to be cautionary, not a paralyzed resignation) basi vile vile tusiogope ku venture kibiashara kwa hofu za abuse.
 
Pesa zipo nyingi tu, kwani mabilioni ya Jk si yanaweza fanya kazi hii badala ya kuliwa na wajanja wachache?

Rwabs,

Budget, si pesa per se.Tuna matatizo mangapi na mangapi yanahitaji pesa hizi hizi dollar bilioni sita tu?

Hapo kabla hujaongelea panga la watu.

BTW nimeambiwa matokeo ya kufaulu Form Six yameimprove kwa about 5% kulinganisha na miaka ya nyuma, sasa sijui kufaulu ni kutokupata 0 au vipi? Hizi habari za kweli?
 
Ok - labda kwanza tujaribu kuongelea ufanisi wa programs hizi...

Wiki chache zilizopita niliangalia show mmoja ya Oprah iliyokuwa inazungumzia jinsi these kids ambao wapo kwenye kids club moja ya Oprah walivyo safiri all the way to Kenya kwenda kujenga madarasa. Hawa watoto walijitolea, na walijenga madarasa mawili kwa mikono yao mwenye. I am talking about 15 - 17 year old kids.

Sasa hebu niambieni kweli tunashindwa kuwatumia Form 6 leavers (ambao ni at least miaka 19+) kujihusisha na ujenzi/ukarabati wa institutions zetu.
 
Ok - labda kwanza tujaribu kuongelea ufanisi wa programs hizi...

Wiki chache zilizopita niliangalia show mmoja ya Oprah iliyokuwa inazungumzia jinsi these kids ambao wapo kwenye kids club moja ya Oprah walivyo safiri all the way to Kenya kwenda kujenga madarasa. Hawa watoto walijitolea, na walijenga madarasa mawili kwa mikono yao mwenye. I am talking about 15 - 17 year old kids.

Sasa hebu niambieni kweli tunashindwa kuwatumia Form 6 leavers (ambao ni at least miaka 19+) kujihusisha na ujenzi/ukarabati wa institutions zetu.

Nnakufahamu mkuu,

Lakini hawa vijana hawana skills kama za ujenzi na wanachofanya ni kushiriki shughuli zile ili zimalizike katika muda uliopangwa.

Jambo jema ni kwa serikali kuwalipia gharama za mafunzo ya skills yoyote iwe umeme na ufundi magari kwani si VETA ipo?

Suala hapa ni vipi fwedha za kuwahudumia wananchi zikiwemo fwedha za mikopo yenye riba nafuu zinatumika.

Nikupe mfano wa Ulaya, mtoto anapomaliza A level tayari anakuwa anajua anaenda chuo kikuu kama amefaulu na hata kama hana uwezo atakopeshwa fwedha hizo ambazo always zipo kwa ajili hiyo na sio malumbano.

La sivyo kama kuna mapungufu basi itabidi asome foundation degree ili afanye kazi akiwa chuoni ambapo anakuwa amekaa kwa miaka miwili tu.

Sasa anapomaliza chuo tayari ana nafasi pale alipokuwa akifanya mafunzo.

Pili serikali inayojali watu wake inakuwa imeelekeza funds katika makampuni au viwanda ambapo vijana huweza kwenda kupata mafunzo ya kazi na kuwa na skills zinazohitajika kujisaidia kimaisha.

Hapa nimeongelea suala la wale wa A level tu, kuhusu GCSE ambapo ni sawa na form 4 wa Tanzania, akimaliza shule ana options nyingi tu kwani kuna vyuo lukuki katika kila tarafa zenye kutoka mafunzo mbalimbali kama ushonaji, kutengeza nywele na hata mambo ya muziki.

Kijana anapomaliza kozi yake anajaribu kuingia ofisi zenye funds maalum kwa ajili ya vijana wanaomaliza mafunzo fulani na kuwapa mshiko wa kuanzisha biashara anayotaka.

Hapa nnazungumzia kijana ambae tayari pia amejifunza kutengeneza business plan au atapata msaaada wa kutengeneza moja.

Kwa hio tunakuwa tunarudi kulekule kwamba bila kudhibiti mambo kama EPA na kodi inayokusanywa kutwa kucha, basi fwedha za kusaidia watanzania haziwezi kuonekana.
 
Lakini hawa vijana hawana skills kama za ujenzi na wanachofanya ni kushiriki shughuli zile ili zimalizike katika muda uliopangwa.

Richard,
Naona umezungumzia mambo mengi kweli....

Idea ni kuwashirikisha vijana ambao wako idle wakisubiri kuingia vyuoni (baada ya kumaliza kidato cha 6) kwenye community services. Hii aina maana ya kuwa vijana hawa wamekwama kimasomo. La hasha! Hizi programs zitalenga kuwashirikisha vijana hawa kwenye ujenzi wa jamii.

Kuhusu skills za ujenzi, wala hakuna haja ya vijana hawa kwenda mafunzo yoyote ya ujenzi au ufundi wowote. Kinachotakiwa ni kuwa na adult supervisors ambao wana kila aina ujuzi. Let's say, kwenye ujenzi wa darasa, kunakuwa na adult mjenzi ambaye anakuwa assigned kwenye usimamiaji wa ujenzi huu.
 
...kweli naanza kuamini TZs kuna kashida kidogo ka kujiletea maendeleo,yaani topic muhimu kama hii lakini input ni zero kabisa,seems watu wengi wanafikiri maendeleo labda ni mpaka Cabinet/bunge wakae chini ...maendeleo ya kweli tutajiletea wenyewe kwenye hizo community zetu zinazotuzunguka sio kivukoni.
 
...kweli naanza kuamini TZs kuna kashida kidogo ka kujiletea maendeleo,yaani topic muhimu kama hii lakini input ni zero kabisa,seems watu wengi wanafikiri maendeleo labda ni mpaka Cabinet/bunge wakae chini ...maendeleo ya kweli tutajiletea wenyewe kwenye hizo community zetu zinazotuzunguka sio kivukoni.

Koba,
Watu humu wako interested na "drama za kisiasa" na "mipasho" zaidi.

Hizi mada zinazolenga kwenye direct involvement katika maendeleo ya nchi yetu huwa hazina nafasi kabisa.

Kichekesho ni kwamba, ukisoma post nyingi kwenye hizo mada za drama za kisiasa, utaona kuwa watu wengi wanao post hawana hata clue wanachokiandika. Yaani ili mradi wameandika tu.

Anyway, kazi kweli kweli........lakini tutafika tu!!!
 
...kweli naanza kuamini TZs kuna kashida kidogo ka kujiletea maendeleo,yaani topic muhimu kama hii lakini input ni zero kabisa,seems watu wengi wanafikiri maendeleo labda ni mpaka Cabinet/bunge wakae chini ...maendeleo ya kweli tutajiletea wenyewe kwenye hizo community zetu zinazotuzunguka sio kivukoni.
Mkuu umepiga ikulu....ndio falsafa yangu hiyo,huwa naamini kuwa katika vitabu vitakatifu na mafundisho ya wazee.....

Vitabu vinatuambia kuwa ukitaka kutoa boriti kwanza toa kwako.....na wazee wet wanatuambia kuwa jenga kwako kwanza.....Hii ni topic nzuri sana ambayo kweli inahitaji inputs za kutosha jamani tunaanza kwenye msinngi hawa vijana wetu wasije kuwa kama baba zao mafisadi.....
 
[...kweli naanza kuamini TZs kuna kashida kidogo ka kujiletea maendeleo,yaani topic muhimu kama hii lakini input ni zero kabisa../QUOTE]

Ndugu yangu, Watanzania ndivyo tulivyo. Tazama hata forum ya education ilivyodorora. Sisi ni wazee wa short cut na kulaumu!

NN
 
...kweli naanza kuamini TZs kuna kashida kidogo ka kujiletea maendeleo,yaani topic muhimu kama hii lakini input ni zero kabisa..

Ndugu yangu, Watanzania ndivyo tulivyo. Tazama hata forum ya education ilivyodorora. Sisi ni wazee wa short cut na kulaumu!

NN

Kulaumu ni hulka ya binadamu wote - mimi nikiwemo. Wewe pia Nungunungu katika maoni yako kuna elements za kutoa lawama. It is a matter of not choosing to complain but do something kusukuma gurudumu.

Constructive criticism will be most welcome. "Ndivyo tulivyo" is not constructive most of the time.

Jukwaa la SIASA limepamba moto kwa sababu ambazo ziko wazi. Sitamlaumu mtu kwa kusahau UCHUMI au community development topics.




.
 
Jukwaa la SIASA limepamba moto kwa sababu ambazo ziko wazi. Sitamlaumu mtu kwa kusahau UCHUMI au community development topics..

Lazydog,
Sasa unajua nini kitatokea? Once drama za ufisadi zitakapoisha (kama kweli zitakuja kuisha), tutajikuta tuna mlima mkubwa wa kupanda katika kuleta maendeleo katika jamii zote.

Kwa sababu kila mjenga nchi sasa hivi amesimama, anatupia lawama kwenye ufisadi kutwa kucha. Matokeo yake, gurudumu la maendeleo limekwama kwenye matope, likisubiri wasukumaji (ambao wanashinda kulalama kuhusu ufisadi).

My point ni kwamba, tunaweza kufanya hivi vitu viwili kwa pamoja. Yaani tunatumia mkono mmoja kurusha jabs kwa mafisadi, na mkono mwingine kusukuma gurudumu la maendeleo. Hii inawezekana kabisa, ukizingatia kuwa dunia la leo ni dunia ya "multitasking."
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom