Forever living VS. ARVs

KIWAVI

JF-Expert Member
Jan 12, 2010
1,817
699
Wadau, leo katika mihangaiko yangu hapa dodoma nimekutana na shida kubwa, watu wansema kwamba forever living products has Aloe Vera inaondoa ukimwi na wana ushahidi

Ombi langu kwa wale waliojaaliwa kupata ilmu ya medika, watupe undani kwani tunakwazika sana na taarifa tofauti
 
Wadau, leo katika mihangaiko yangu hapa dodoma nimekutana na shida kubwa, watu wansema kwamba forever living products has Aloe Vera inaondoa ukimwi na wana ushahidi

Ombi langu kwa wale waliojaaliwa kupata ilmu ya medika, watupe undani kwani tunakwazika sana na taarifa tofauti

Sidhani kama kusoma medicine tu kutamfanya mtu akujibu swali lako, anatakiwa mtu aliyespecialize zaidi kwenye hii mitishamba.
Otherwise, that could be gud nyuz!
 
Wadau, leo katika mihangaiko yangu hapa dodoma nimekutana na shida kubwa, watu wansema kwamba forever living products has Aloe Vera inaondoa ukimwi na wana ushahidi

Ombi langu kwa wale waliojaaliwa kupata ilmu ya medika, watupe undani kwani tunakwazika sana na taarifa tofauti


Hakuna dawa inaweza kuuondoa UKIMWI once ukishaingia mwilini.
ARVs zinasaidia tu katika kupambana na kumuongezea mgonjwa muda wa kuishi na wala zenyewe hazitibu UKIMWI.Dawa pekee ni kuzuia usiambukizwe VVU/HIV. BASI!
 
Wadau, leo katika mihangaiko yangu hapa dodoma nimekutana na shida kubwa, watu wansema kwamba forever living products has Aloe Vera inaondoa ukimwi na wana ushahidi

Ombi langu kwa wale waliojaaliwa kupata ilmu ya medika, watupe undani kwani tunakwazika sana na taarifa tofauti

Kwanza ni lazima ujue kuwa kuna tofauti kubwa tu kati ya UKIMWI (AIDS) na VVU (HIV). VVU bado hakuna dawa ya kuviangamiza au kuzuia visitende kazi katika mwili wa binaadamu. Unaweza ukawa na VVU lakini usiwe na UKIMWI. Na kimantiki, unaweza ukawa na upungufu wa kinga mwilini lakini usiwe na VVU (magonjwa kama kansa ya damu husababisha kinga ya mwili kupungua).

Kwa sehemu kubwa UKIMWI, hupimwa kwa kuangalia kiasi cha CD4 (zikianza kuwa pungufu ya 200 counts, then kitaalamu una UKIMWI na ndipo hapo wengi huanza kutumia ARVs). Kuna 'vyakula' vingi tu ambavyo husaidia kuongeza kinga ya mwili (including baadhi ya products za Forever Living) na hivyo kumsaidia mtu mwenye VVU asiingine kwenye stage ya UKIMWI mapema kama bado au kumsaidia mwenye ukimwi kuongeza kinga yake.

Binafsi, bado siamini kama products za Forever Living (FL) zinaweza kuwa mbadala wa ARVs hasa ukizingatia kuwa ARVs zipo za aina nyingi na zinaendana na stage na aina ya VVU. Sidhani kama products za FL zinazingatia haya.
 
kwakweli nimekua nikisikia habari za hayo madawa ya forever, ila inapaswa kujiuliza swali moja je yanatengenezwa nchi gani, je mamlaka ya chakula na madawa imeyauhusu kutumika, je yana dozi kweli ama yananywewa kama mwarubaini tu yaani kunywa weeh mpaka uone matokeo , na je imethibitika yanatumiwa nnchi nyingine.
 
wadau endeleeni kujipa moyo mtashinda.hakuna cha dawa wala nn na uvicheche wa malaya ukimwi utaishaje?dawa ni moja tu kuacha ngono zembe tikishajifahamu tumeshanyemelea michangudoa huko gizani tunaanza kuzua ooh! dawa zimepatikana.dawa tunazo wenyewe hatuzitumii.
 
watu wa forever wanaamini kwamba wanaweza kutibu KI-SUKARI kwa dawa zao...!tulibishana mpaka sauti zikatukauka
 
ila haya madawa mala foreva livingi mala sijui nini hata sijui inakuwaje cause hivi yanatibu kweli??
 
watu wa forever wanaamini kwamba wanaweza kutibu KI-SUKARI kwa dawa zao...!tulibishana mpaka sauti zikatukauka

Geoff mie pia huwa nashindwa kuyaamini ..nimeshatumia yale ma Aloe Gel nakunywaga tu eti kwa afya hizi Colgate zao ,sijui Lotion na vitu vya urembo mbaya zaidi vina bei sana kwa mtu mwenye maisha ya chini mtu huwezi kabisa ku afford
 
Geoff mie pia huwa nashindwa kuyaamini ..nimeshatumia yale ma Aloe Gel nakunywaga tu eti kwa afya hizi Colgate zao ,sijui Lotion na vitu vya urembo mbaya zaidi vina bei sana kwa mtu mwenye maisha ya chini mtu huwezi kabisa ku afford
wasanii sana hawa viumbe
MIMI NI MWANACHAMA HAI WA TIENS!..ninajua ins and outs
 
Jamani tusifarijiane tukaja danganyika kirahisi. Mpaka sasa hakuna dawa yenye uwezo wa kuondoa VVU kwa mtu aliye athirika. Hii ni kutokana na tabia ya VVU ambavyo ni virusi vilivyo kwenye kundi la RETROVIRUS.
Virusi hawa kwanza wanauwezo mkubwa sana wa kujibadilishabadilisha, kiasi cha kwamba ndani ya mwili wa mtu mmoja kunakuwa na aina tofautitofauti ya virusi hawa ( Kitaalamu Quasy species)(strains). Hii hufanya kinga ya mwili kushindwa kuwaondoa.

Pia virusi hivi huathiri seli zinazohusika na kinga mwilini zenye kitambulishi cha CD4, kama CD4 +ve T-Lymphocytes, Macrophages(monocytes), na Dendritic cells. Ndani ya hizi seli kirusi hiki huweza kukaa kwa miaka mingi wakiwa katika hali ya utulivu i.e. latent state. Na dawa haiwezi kuja kuwaua hawa virusi ndani ya hizi seli bila kuziua hizi seli , kitu ambacho ni hatari kwa afya ya muathirika.
Hawa virusi wanazaliana ndani ya hizi seli zinazohusika na kinga ya mwili na ili kutoa virusi wapya hizi seli hufa. na ndo maana kiwango cha CD4 seli ndani ya mwili hupungua.

Kilichowezekana sasa ni kupunguza kasi ya kuzaliana kwa hawa virusi ndani ya mwili na hivyo kupunguza kasi ya kuuwawa kwa CD4 +ve seli na hatimaye kupandisha kinga ya mwili. Ila seli zilizo athirika zitaendelea kuwa na virusi bali watakuwa hawazaliani.

Tuendelee kumuomba mungu tafiti zinaendelea kufanyika ili tuweze kupata kinga mbadala ya VVU/UKIMWI.
Mpaka sasa kinga pekee madhubuti ya ukimwi ambayo itakupunguzia uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kwa asilimia kubwa sana ni abstainace from having unprotected penetrative sex with multiple patners.
 
jamani ni vile tu watanzania tunautamaduni wa kuenzi vya nje na kuponda vya kwetu ila hizo product za fl mimea wanayotumia hapa kwetu ipo ila aijapakiwa kitaalamu kama fl na zinafanya kazi sawa na kuzidi kwani vyetu vingi avijawekwa kemikali ili kuviifazi
mwisho aiwezekani itibu ukimwi labda kuongeza kinga mwilini kama wafanyavyo wazawa kama dr ndondi
 
wadau endeleeni kujipa moyo mtashinda.hakuna cha dawa wala nn na uvicheche wa malaya ukimwi utaishaje?dawa ni moja tu kuacha ngono zembe tikishajifahamu tumeshanyemelea michangudoa huko gizani tunaanza kuzua ooh! dawa zimepatikana.dawa tunazo wenyewe hatuzitumii.

asante sana... sasa je ile promotion wanayofanya hawa watu wa forever ni sawa? au wanibia wateja kwa kutoa kitu kisicholigana na sifa zake?
 
Are you FirstLady1 ? or Jokes? pole kumbe na wewe unatumia FL sasa njoo upate Mpako hapa Ubungo Please I beg you!!! dont worry
 
Jamani tusifarijiane tukaja danganyika kirahisi. Mpaka sasa hakuna dawa yenye uwezo wa kuondoa VVU kwa mtu aliye athirika. Hii ni kutokana na tabia ya VVU ambavyo ni virusi vilivyo kwenye kundi la RETROVIRUS.
Virusi hawa kwanza wanauwezo mkubwa sana wa kujibadilishabadilisha, kiasi cha kwamba ndani ya mwili wa mtu mmoja kunakuwa na aina tofautitofauti ya virusi hawa ( Kitaalamu Quasy species)(strains). Hii hufanya kinga ya mwili kushindwa kuwaondoa.

Pia virusi hivi huathiri seli zinazohusika na kinga mwilini zenye kitambulishi cha CD4, kama CD4 +ve T-Lymphocytes, Macrophages(monocytes), na Dendritic cells. Ndani ya hizi seli kirusi hiki huweza kukaa kwa miaka mingi wakiwa katika hali ya utulivu i.e. latent state. Na dawa haiwezi kuja kuwaua hawa virusi ndani ya hizi seli bila kuziua hizi seli , kitu ambacho ni hatari kwa afya ya muathirika.
Hawa virusi wanazaliana ndani ya hizi seli zinazohusika na kinga ya mwili na ili kutoa virusi wapya hizi seli hufa. na ndo maana kiwango cha CD4 seli ndani ya mwili hupungua.

Kilichowezekana sasa ni kupunguza kasi ya kuzaliana kwa hawa virusi ndani ya mwili na hivyo kupunguza kasi ya kuuwawa kwa CD4 +ve seli na hatimaye kupandisha kinga ya mwili. Ila seli zilizo athirika zitaendelea kuwa na virusi bali watakuwa hawazaliani.

Tuendelee kumuomba mungu tafiti zinaendelea kufanyika ili tuweze kupata kinga mbadala ya VVU/UKIMWI.
Mpaka sasa kinga pekee madhubuti ya ukimwi ambayo itakupunguzia uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kwa asilimia kubwa sana ni abstainace from having unprotected penetrative sex with multiple patners.

very good points, lakini je vinajibu point ya mtoa mada?
 
Back
Top Bottom