Fursa Pesa
JF-Expert Member
- May 30, 2012
- 4,432
- 3,253
Kama ndio mfumo ulio bora waambieni CRB wafute makampuni ya Ujenzi .Nimekuwa mdau wa matumizi ya Force Account tangu JPM aingie madarakani na sasa Mama Samia. Mtoa mada huujui huu mfumo unavyofanya kazi. Na kama kawaida ya wachangiaji wengi humu watalaumu kweli bila kujua mfumo huu. Kifupi, mpaka sasa ndio mfumo bora kabisa wa matumizi ya Serikali kwa sasa.
Force Account umeharibu mzunguko wa fedha mtaani na kusababisha makampuni mengi ya ushauri na ujenzi kujifunga yenyewe.
Kwa ufupi ni mfumo ambao haufai hata kidogo kwa kuwa athali zake ni nyingi kuliko faida mfano Graduates wengi wako mtaani na wale walioko masomoni hawapati mentors wa kuwafundisha kazi kwa vitendo/field kazi nyingi zinafanywa na mafundi bila weledi /usimamizi mathubuti.