Forbes yamtaja Rais Samia Suluhu Hassan katika Wanawake 100 wenye nguvu zaidi duniani mwaka 2021. Yupo nafasi ya 94

Mtangazaji mashuhuri Zuhura Yunus wa BBC amesema Rais Samia ameingia katika orodha ya Wanawake 100 wenye ushawishi zaidi duniani kutokana na namna alivyolishughulikia kwa weledi mkubwa swala la Corona nchini Tanzania

Orodha hiyo imeandaliwa na Forbes na Rais Samia amekamata nafasi ya 94, anasema Zuhura.

Source: BBC Dira ya Dunia
 
Wanatuchanganya hawa watu,juzi wametangaza kuwa Tanzania siyo Nchi salama kwa kutembelea baada ya kutochukuwa hatua za COVID,Leo yamekuwa hayo Tena?
 
... ukiacha suala la uwanawake, yeye na JPM nani alishughulikia Covid-19 kwa weledi zaidi?
 
Huo ushawishi wake umemsaidia nini mtanzania wa kasimbo,Tandahimba,kipili nk kupata huduma bora za jamii ? na kupunguza mfumuko wa bei.?
 
View attachment 2036208
  • Samia Suluhu Hassan became Tanzania's sixth president and first-ever female leader in March 2021, following the death of President John Magufuli.
  • She rose to the position from vice-president, a role to which she was first elected in 2015.
  • In September, she became just the fifth-ever female African leader to address the U.N. General Assembly. She used her remarks to criticize Covid vaccine inequality.
  • Suluhu has differentiated her leadership from her predecessor by implementing stricter Covid protocols, including mandatory quarantines for travelers coming from countries with new variants.
Source: https://www.forbes.com/power-women/

====

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametajwa na jarida la Forbes kama mmoja wa Wanawake 100 wenye nguvu zaidi duniani kwa mwaka 2021.

Orodha hiyo si kwamba inajumuisha wanawake wenye fedha au madaraka, bali mwanamke aliyetumia kipaji chake, sauti au jukwaa kufanya jambo lenye manufaa kwa jamii.

Katika orodha hiyo Rais Samia ameshika nafasi ya 94 ambapo jarida hilo limeeleza namna alivyotumia jukwaa la Mkutano wa Baraza Mkuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) kukosoa mgawanyo usio sawa wa chanjo za Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO19).

Alihutumia mkutano huo mkubwa duniani ikiwa ni miezi sita tangu alipoingia madarakani kufuatia kifo cha Rais Dkt. John Magufuli, na alikuwa kiongozi mwanamke wa sita kutoka Afrika kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Forbes imetambua namna Rais Samia alivyotofautisha uongozi wake na wa mtangulizi wake katika mapambano dhidi ya UVIKO19, ambapo ametekeleza hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na karantini ya lazima kwa wageni kutoka nchi zenye aina mpya za virusi.

Nafasi ya kwanza kwenye orodha hiyo yupo MacKezie Scott (mtalaka wa Jeff Bezos) ambaye ni mwanamke watatu kwa utajiri duniani. Wengine ni Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris, Melinda Gate, Nancy Pelosi, Spika wa Bunge la Wawakilishi la Marekani.

Wanawake wote 100 wametoka katika nchi 30, katika sekta mbalimbali kama teknolojia, fedha, siasa, burudani, wasaidia jamii, na wote wameunganishwa kutokana na utendaji wao.

Chanzo: Swahili Times
Kaziiendelee
 
View attachment 2036208
  • Samia Suluhu Hassan became Tanzania's sixth president and first-ever female leader in March 2021, following the death of President John Magufuli.
  • She rose to the position from vice-president, a role to which she was first elected in 2015.
  • In September, she became just the fifth-ever female African leader to address the U.N. General Assembly. She used her remarks to criticize Covid vaccine inequality.
  • Suluhu has differentiated her leadership from her predecessor by implementing stricter Covid protocols, including mandatory quarantines for travelers coming from countries with new variants.
Source: https://www.forbes.com/power-women/

====

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametajwa na jarida la Forbes kama mmoja wa Wanawake 100 wenye nguvu zaidi duniani kwa mwaka 2021.

Orodha hiyo si kwamba inajumuisha wanawake wenye fedha au madaraka, bali mwanamke aliyetumia kipaji chake, sauti au jukwaa kufanya jambo lenye manufaa kwa jamii.

Katika orodha hiyo Rais Samia ameshika nafasi ya 94 ambapo jarida hilo limeeleza namna alivyotumia jukwaa la Mkutano wa Baraza Mkuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) kukosoa mgawanyo usio sawa wa chanjo za Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO19).

Alihutumia mkutano huo mkubwa duniani ikiwa ni miezi sita tangu alipoingia madarakani kufuatia kifo cha Rais Dkt. John Magufuli, na alikuwa kiongozi mwanamke wa sita kutoka Afrika kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Forbes imetambua namna Rais Samia alivyotofautisha uongozi wake na wa mtangulizi wake katika mapambano dhidi ya UVIKO19, ambapo ametekeleza hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na karantini ya lazima kwa wageni kutoka nchi zenye aina mpya za virusi.

Nafasi ya kwanza kwenye orodha hiyo yupo MacKezie Scott (mtalaka wa Jeff Bezos) ambaye ni mwanamke watatu kwa utajiri duniani. Wengine ni Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris, Melinda Gate, Nancy Pelosi, Spika wa Bunge la Wawakilishi la Marekani.

Wanawake wote 100 wametoka katika nchi 30, katika sekta mbalimbali kama teknolojia, fedha, siasa, burudani, wasaidia jamii, na wote wameunganishwa kutokana na utendaji wao.

Chanzo: Swahili Times
Kaziiendelee Tanzania
 
Kusadikika "Shabaan Robert"
Kivuli Kinaishi "xxxx xxxx".

Naanza kufuatilia kwa karibu Forbes naona kama mali ya Benson Banna
 
Ukiwa Rais lazima uwe na nguvu unakosaje nguvu wakati kila kilichomo ndani ya nchi ni chako
 
Sema tu Samia Suluhu ameiba hela. Toka lini Forbes wanajishughulisha na watu wenyr nguvu?
 
#2025Fever itawapotezea muda wenu bure,hakuna wakumuangusha Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi hizi kubwa na nzuri anazozifanya,

#KAZIIENDELEE NA MAMA
 
Kama mambo ndio haya basi Tanzania kama kuna wakati tumepata Rais bora na wa kweli nadhani ni sasa,Tufanye kazi kwa bidii sana,

Hakika huyu Mama ni Mpango wa Mungu,

#WATANZANIA TUFANYE KAZI KWA BIDII
 
" Kwa mwendo huu Tanzania tutafika tunakotaka kwenda tena kwa kuwahi sana, Hongera Mama Samia, Watanzania tuko nyuma yako We chapa kazi achana na Wasio na jema "
 
Back
Top Bottom