Taluma
Senior Member
- Jan 22, 2011
- 158
- 2
Habari zenu mabibi! Nipo kwenye harakati za kutafuta mwanamke wa kuishi naye hapa Tanzania: Sifa za mke ninaye mtafuta ni kama ifuatavyo;
Asante na Mungu awabariki sana!
- Awe na umri kati ya miaka 25 hadi 32
- Asiwe amewahi kuolewa kwa ndoa ya aina yeyote ile
- Asiwe amewahi kuishi na mume kama mume wake (zile za kuvutana kimya kimya bila ndoa)
- Awe na umbo linalovutia (si bonge sana, si mwembamba sana) ie good looking ...wale wa mkorogo au mawigi....no please...!ninapenda natural beauty!
- Elimu angalau form four na kuendelea
- Awe mfanyakazi au mjasiliamali
- Awe ni mkristo -RC au kama ni dhehebu lingine (sio ulokole) awe tayari kuwa RC
- Asiwe na kuburi kabisaaaa
- Asiwe na hasira, jaziba au vuvuzela
- Asiwe mchafu, awe anapenda usafi wa mwili wake, nyumba, mazingira anayoishi, viwalo vyake etc
- Awe mke mwenye hekima, busara na adabu kwa wakubwa wake
- Awe mke anayeheshimu mila na desturi za kiafrika...asiwe adicted kwenye western culture tu.
- Awe tayari (if god wishes) kuzaa watoto wasiozidi wawili tu
- Awe tayari kupima VVU -wakati ukiwadia
- Awe mtanzania wa kabila lolote
- Elimu chuo kikuu -na professional certificate
- Umri miaka 34
- Kabila Mnyalu
- Mfanyakazi na mjasiliamali
- Nina huruma sana for the ''needy'' people
- Nina kunywa ....hasa weekends!
- Nina watoto wawili - mama yao tuliachana (hakukuwa na ndoa yeyote) baada ya kushindwa kuelewana
- Niko rafu (kuvaa, kula) lakini napenda mke asiwe rafu kama mimi
- Nina jiamini
- Ni mrefu - 1.67m
- Uzito 84kgs
- Occassionaly huwa naenda club
- Ni mweusi ila kidogo maji ya kunde
- Napenda muziki - wa dini na uraiani
- PM - hapa JF
- Email : taluma77@yahoo.com
Asante na Mungu awabariki sana!