Mi ndio nimepita hapo mida hii 1.15am toka saa 4.30, hii ni balaa; raha ni kwamba nilikuwa na ubavu wangu hivyo siku nyingine hata nikisema nimechelewam sababu ya foleni nitaeleweka!!!
Mkuu chepukia chuo fasta unafika kimara kama unaenda tabata chepukia sinza utafika
Kiukweli sina la kuzungumza...Ndugu yetu maghufuli pls tusaidie,masaa ma5 kwenye junction??
Foleni za dar ni ukosefu wa nidhamu na vision yoyote.
Wao ni watu wa kusubiri wafadhili tu .
Kuna maeneo yenye kufanya foleni yanaweza kupatiwa ufumbuzi mara moja.
Lakini watu wanajikalia ofisini na kulifanya tatizo ni la jiji lote hivo wanasubiri miujiza ya DART.
Hata kwa bajeti zetu ndogo tunaweza kuondoa tatizo hili..
Wala tusidhani Dart ndio mwarubaini wa foleni.ni mradi wa kufaidisha watu fulani na mabasi yao kwa mgongo wa deni kwa taifa.
Mfano akili gani kuua kipande cha morogoro road kinachoanzia bibi titi kuingia katikati ya jiji na kukifanya kuwa cha mabasi tu ?
Hii ndio barabara kubwa ilokua ikitoa magari kutoka katikati ya jiji leo eneo hilo ni balaa tupu baada ya kuifunga njia hii.
Pia akili gani kuzuia ku turn right kuingia morogoro road ukitokea maktaba njia ya bibi titi?
Hivi magari yatokayo katikati ya jiji kwenda morogoro yapite njia gani?
Yazunguke agrey then nini titi ndio kuingia morogoro ? Akili gani ya planner wetu wa jiji na kina magufuli!!
Leo kuingia moro ukitoka mjini centre upite upanga to regency hospital to fire area !!!
Mradi huu mzuri lakini watu walokaa wakaupitisha ni wajinga hawakuchambua kila eneo na umuhimi wake wao waliyaona mabasi makubwa tu...
Mkuu wanachemsha bongo sana kiongozi, si unaona wamekuja na suluhisho la kuzuia bodaboda kuingia mjini kwa sababu ndizo zinazosababisha foleni!!!
Mwanza napo wasipochukua hatua mapema itakuwa kama dar tuu kwa foleni.Karibuni mza hatunaga foleni