Foleni Morogoro Road

keizerjohn

Senior Member
May 12, 2013
113
13
Wadau, hivi mbona foleni ya Morogoro Road haitafutiwi ufumbuzi wa haraka. Kweli mpaka barabara ikamilike miaka miwili ijayo, tutakuwa katika hali gani? Kutoka mbei hadi Stand ya Mkoa mtu unatumia zaidi ya masaa manne wakati ni km 13 tu.
Huu ni ujenzi gani wa kutojali watumia barabara? TANROADS mpo wapi? Serikali nayo ipo wapi? Viongozi wetu mpo wapi, hata wapinzani na nyinyi mpo wapi?
Licha ya watu wote kuathirika, wagonjwa, wanafunzi, wakina maama wana hali mbaya zaidi! Haya ni maendeleo au ni kurudishana nyuma?
Kama Serikali ipo kimya, basi vyama vya hiari vihamasishe maandamano ili tuishurutishe Serikali ije na mbinu mbadala ya haraka ya kupunguza foleni hii wakato ujenzi unaendelea.
Haiingii akilini Kampuni inabomoa kila mahala halafu haitengenezi, inaziba ziba kila mpenyo na kutuacha tunahangaika.

Wadau tujadili hili tufanyaje?
 
Wadau, hivi mbona foleni ya Morogoro Road haitafutiwi ufumbuzi wa haraka. Kweli mpaka barabara ikamilike miaka miwili ijayo, tutakuwa katika hali gani? Kutoka mbei hadi Stand ya Mkoa mtu unatumia zaidi ya masaa manne wakati ni km 13 tu.
Huu ni ujenzi gani wa kutojali watumia barabara? TANROADS mpo wapi? Serikali nayo ipo wapi? Viongozi wetu mpo wapi, hata wapinzani na nyinyi mpo wapi?
Licha ya watu wote kuathirika, wagonjwa, wanafunzi, wakina maama wana hali mbaya zaidi! Haya ni maendeleo au ni kurudishana nyuma?
Kama Serikali ipo kimya, basi vyama vya hiari vihamasishe maandamano ili tuishurutishe Serikali ije na mbinu mbadala ya haraka ya kupunguza foleni hii wakato ujenzi unaendelea.
Haiingii akilini Kampuni inabomoa kila mahala halafu haitengenezi, inaziba ziba kila mpenyo na kutuacha tunahangaika.

Wadau tujadili hili tufanyaje?
Tunajenga kwa ajili yako
 
viongozi wetu. wako kimasilahi zaidi kuliko kutujali. mbo cku zilizo pita barabara. hutengenezwa bila. kuathiei shughuli nyingine?
 
Huu ni mfumo wa kijinga sana,huwezi kuijenga barabara na kuifunga yote kiasi hiki?wafungue sehemu zilizo tayar au waipanue zaidi pembeni ili zipite gar nyingi,mbona eneo la TANROAD ni kubwa?halafu mbona hamna u turn?gari haiwez kwenda ng'ambo ya pili kwanini?waweke barabara za juu walau hata 2 katikati ya kimara na ubungo kwaajili ya magari kwenda upande wa pili.
 
Sasa hivi foleni imezidi zaidi kwa kuwa hata njia za kuchepuka kwa mfano kwenda kupitia chuo kikuu, zimezibwa, huwezi kupita huko na hivyo wote tunalazimika kupita hapo hapo ubungo mataa.

Hii ni balaa.

Tiba
 
Kuna watu humu wanasema eti STRABAG, hiyo Kampuni inayojenga barabara ya Morogoro wako juu ya sheria...
 
Hali inatisha Mimi nilishafika mahali nikatamani bora hata watu kuandamna na kwenda Kuwapiga hawa wakandarasi!! Hawajali kabisa!! Imekuwa Nchi kama haina serekali!! Angalia kuna Mtaalamu mshauri Smec, Sijui anashauri nini? Pia design ni Very poor!!
 
Wakuu, hawa jamaa wanakiburi cha viongozi wetu, haiwezekani watu tunateseka hiv wao hawaelewi kitu Na Serikali ipo kimya.
Kwanza ujenzi Wa kuziba barbr, design very poor, watu wanamagari wanashindwa kwenda upande wa pili, mijitu inaamgalia tu ujenzi huu mbovu.
Watu Wa mikoani wanateseka kweli kufika Dar
Wengine Wa hapa Dar hadi ndoa zinacunjika!
Kweli duniani hakuna haki!
Nasi tupo kimyaaa, ndio maana tunatawaliwa badala ya kuongozwa
 
Hali inatisha Mimi nilishafika mahali nikatamani bora hata watu kuandamna na kwenda Kuwapiga hawa wakandarasi!! Hawajali kabisa!! Imekuwa Nchi kama haina serekali!! Angalia kuna Mtaalamu mshauri Smec, Sijui anashauri nini? Pia design ni Very poor!!
Kaka inauma, tungekuwa wengi wenye uelewa Kama huu wasingetuonea. Wametoona mazezeta
 
Nategemea
hao jamaa wajenzi wana uzoefu ila najiuliza kwa nini wasijenge MUDA ambao
hauna heavy trafick kama USIKU kama inavyofanyika nchi nyingine?
 
Eeeeh poleni watanzania,hiyo foleni itaisha mwanzoni mwa kampeni za uchaguzi ujao ili muwe na kumbukumbu....mie ninamwezi mmoja cjui hiyo foleni. kwa ndg zangu waendao kibaha,mbezi,na kwingineko ni heri ukapita njia ya makongo kupitia goba ukaja tokea mbezi njia ni nzuri imerekebishwa hivi punde. au waweza pita kinyerezi iko poa pia...
 
Sasa hivi foleni imezidi zaidi kwa kuwa hata njia za kuchepuka kwa mfano kwenda kupitia chuo kikuu, zimezibwa, huwezi kupita huko na hivyo wote tunalazimika kupita hapo hapo ubungo mataa.

Hii ni balaa.

Tiba

Sio lazima kuishi Dar. Njooni Shinyanga, Tabora au hata hapo jirani tu Morogoro!
 
Back
Top Bottom