Sikuwa na taarifa hii kabla. Shukrani mkuu mwiba kutuhabarisha. Ni kitu kizuri kwa maendeleo. Nawapa tano kwa walau kujaribu kuanza kufanya hilo. Nchi nyingi duniani wamefanya na wamefanikiwa. Mfano, daraja la treni kati ya Uholanzi na Ubelgiji, kivuko kati ya Uingereza na Ubelgiji/Uholanzi, nk. Kwanini sisi tuwe watu wa kusimulia tu badala ya kutenda! Kufaulu au kushindwa ni sehemu ya maisha, lakini kukaa tu bila kujaribu (iwapo una resources) hakuna maana.
Sasa hivi kwa akili yako kutengeneza umeme na daraja ipi rahisi.Wewe kaa usubiri uone.
Nashauri bandiko hili lifutwe, na mleta bandiko apewe onyo kwa kubandika Tangazo feki. Ukifuatilia tovuti aliyo dokoa picha hizo Mabey & Johnson hawana mradi wowote wa ujenzi wa Daraja katika Tanzania
Apewe server ban.. Kwi kwi kwi..
Maalim Mwiba, kwa mantiki ya kujiondolea adha nzito kwanza haiingii akilini kutengeneza daraja hili badala ya matatizo ya msingi.
Hilo daraja ni kwa traffic volume ipi, na ni kwa kupeleka hiyo traffic wapi.Ndio maana kabla hata ya kujenga barabara huwa kuna feasbility study za kuonyesha economic impact ya barabara hiyo.Hili daraja lako pamoja na kuwa ni a positive thing ni kama Serikali ya Tanzania kuamua kupeleka mtu mwezini!
Hili ni ile hali ya Tit for Tat unajua kuna mfereji wa Suez pale ambapo Afrika ilitengwa kabisa na Nchi za watu majuu. Na meli ikikatisha inalipa ndio hivyo hivyo daraja litakuwa na fedha linaingiza wakati meli inakatisha hata kule Panama nao ndio wanatia feza kwa akili kama hizi.Hili lingekuwa daraja lenye umbali mkubwa kuliko yote duniani, kushinda hata lile linalotaka kujengwa kati ya Djibuti na Yemen ambalo litakuwa na umbali mkubwa kuliko yote.
Ingawa linatengenezwa kwa siri lakini kwa hali lilipofikia si siri tena.
...thubutuuu,
wangejenga la Kigamboni kwanza, BTW umbali toka unguja kwenda Pemba ni maradufu ya umbali toka Unguja kwenda Bagamoyo tu hapo, ...iwe leo wajenge daraja malindi kwenda chwaka?
...Halafu hayo maji mbona tope sana, mkondo umepita nini?