Fizikia ya ajali (The Physics of Accidents): Mabasi yetu yanaundwa au kuunganishwa wapi?

Jioni ya leo nimebahatika kuongea na dereva wa mabasi ya mikoani ambaye anafanya kazi katika moja ya kampuni kubwa. Nimemwuliza kuhusu ajali nyingi tunasikia tairi za mbele zimepasuka. Anasema kuanzia wamiliki wa mabasi,trafiki,sumatra na wao kama madereva wanajua tatizo ni matairi yasiyokidhi viwango. Anasema ni kampuni chache sana ambazo hazizidi hata 7 magari yao yanafunga tairi mpya za michelin ama bridgestone. Anasema ajali zote tunazisikia za kupasuka tairi za mbele,magari yanakua yamefunga tairi za kichina. Kuhusu ajali ya basi la Deluxe anasema basi ilikua chakavu na tairi za mbele zilikua vipara!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mzee Mwanakijiji pamoja na majibu mazuri sana ya wanajamvi ila naomba niongeze kitu hapa body assebly ya magari mengi yanafanywa na quality grop hapa tz lakni pia kuna chinise company na hta nyumbu wanafanya haya hapa ubungo. pia wapao wanaofanyia kenya but wote hawa TBS inatakiwa ikague kuona kama yanameet standards kwenye maeneo yote mechanics and electronics. pia waaangalie minimum factor of safety.

ukiachilia mbali tairi ambazo ni less durable tena nyingine ni zile wanaziita used kuna swala la aina ya body ya gari ambapo juzi nilikuwa naongea na watu fulan wanamiliki mabasi walisema ni bora tena na bodi za mchina manake in case ya ajali basi ubavu wa basi uanyuka na watu wake na kuwatupa nje ila kwa haya ya mabati yanayotengenezwa kibongo bongo kazi ni ngumu manake ajali ikitokea vyuma vile inawachinjia humo ndani pasi matani. kwangu mimi niliona kama hoja hii si nzito sana kwani TBS na SUMATRA wanatakiwa kuangalia je aina gani ya bodi zinazohimili mikiki hapa kwetu, kulingana na aina ya land scape na bara bara.pia waangalie electronics na mechanics ya gari lenyewe iwepo possibilities ya kuweza kuzuia ajali kwenye miundoo hii.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji

Katika ground vehicle dynamics, roll over husababishwa na vitu vitatu tu: (i) speed ya gari husika (ii) geometry ya barabara (curvature and banking angle) na (iii) automobile layout (traction position, center of gravity, na steering angles).

Structural design inaweza kuchangia kwa kiasi kidogo sana kwa vile structural failures zingekuwa zinasabababisha ajali hizo kuambatana na kuvunjika kwa structures fulani za gari. Picha nilizoona hazionyeshi critical structural failures!

jambo linaloweza kufanyika ni kuweka standards ngumu kuhusu automobile layout kwa mabasi; yaani yawe na upana mkubwa kidogo. Hata hivyo bila kuimarisha discipline ya kuheshimu speed limits, nadhani tutaendelea kuliwa kwa muda mrefu sana. Ingesaidia sana iwapo serikali nayo ingechukua initiative ya kuweka islands kwenye barabara kuu kutenganisha magari yanayoelekea pande tofauti za barabara.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: ral
Pia siku hizi police barabarani hawapo kusimamia sheria badala yake wanakuonyesha makosa na kukuambia faini yake hapa ni 120000 ila we nipe hela ya kosa moja tu 30000 ukimpiga sound anachukua 2000 au 3000 huku ukiangalia tairi za mbele za gari ni hazifai zimekwisha kabisa we unadhani kwa hali hii ya police kuhongwa na kiasi kidogo kama hiki ajali zitaisha kweli?
 
Shine umesema kweli kabisa, chanzo kingine kikubwa cha ajali barabarani ni hawa traffick, utakuta gari lina makosa lakini yeye anapokea pesa na kuacha gari liondoke ilhali lile gari ni bovu. hebu tuchukulie mf. wa juz kat ile ajali ya bas lililokuwa limebeba abiria zaid ya 90a.unadhani hawakukutana na traffick? yawezekana kabisa walikutana naye na alipewa kitu kidogo akaliruhusu gari kuendelea na safari matokeo yake ndo yale. USHAURI WANGU: MABASI YANAYOJAZA ABIRIA ZAIDI YA LEVEL SEAT YAFUNGIWE
 
Last edited by a moderator:
[h=1]WATU 3 WAFARIKI DUNIA, 24 WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI LA RS WILAYANI KAHAMA[/h]


Basi la RS katika muonekano wa ubavuni baada ya ajali.
Muonekano wa lori ambalo limegongana uso kwa uso na basi la RS.

Wananchi wakishudia ajali hiyo.
 
Mzee, MMKJ

nasoma post zako mara nyingi, halafu najiuliza hivi wakombozi wa hii nchi tuko wapi? Watu wanafanya maisha ya watu kama mzaha! I think it is time we should say no, it is enough
 
I think Quality Garage bado wanaendelea na kuunganisha mabasi, sina uhakika kama kuna washindani wengine kwenye biashara hii...

Quality Garage ya baba yake Manji ndio walikuwa wanatengeneza na kuunganisha magari. I am interested to find out through research probably, kule Tabata dampo ni body za magari gani zinatengenezwa na zina ubora wa kiasi gani pia. Welding ina utaalamu wake ili kuifanya na quality assuarance inafanywa either kwa destructive or non destructive methods. Sidhani kama jamaa wanafanya hizo test as they are expensive. If yes who controls what is being done in some of the garages that are scattered throughout Tanzania.
Inawezekana kabisa uimara wa vyombo vya usafiri unachangia ajari za barabarani. Isipokuwa uzembe ndio unaoongoza kwa kuleta ajari hizo.
 
1. jenga barabara za ubora unaotakiwa na mbili kwenda mbili kurudi katikati wajenge kiukuta kuzuia upande mmoja usiingiliane na mwingine itazuia kugongana uso kwa uso
2. kagua na lazimisha wenye magari kufunga matairi yenye ubora
3. ujengaji wa mabasi uwe na ubora unaotakiwa kwa kuzingatia viwango
4.sehemu yenye mteremko mkali kisha mlima jenga daraja kuunganisha mteremko na mlima
5. adhabu kali kwa madereva wazembe ikiwezekana kumfungia leseni wala mwaka miezi mitatu kwa kila kifo na mwezi mmoja kwa kila majeruhi ikibainika kuwa alizembea na kusababisha ajali
6. kwa barabara kuu jenga fensi ili watu na mifugo isikatize barabara,
7. jenga maabara kwa ajili ya utafiti na kupima ubora wa muundo wa gari na ajali
 
bado sijasikia ni wapi mabasi haya yanaunganishwa na ni chombo gani kinasimamia? tuachane na ya Katiba mpya kwanza tuzungumzie right now tusije kudhania katiba mpya itatatua matatizo ya ajali au matatizo mengine yoyote yale. Kuna vitu tunaweza kuvifanya sasa hivi

Quality group ya manji inatengeneza bodi za magari na wanatengenezea pale quality garage ila ni taasisi gani inakagia ubora bado sijajua naulizia nitakujibu
 
Matatizo ya Kisayansi yanahitaji utatuzi wa Kisayansi... lakini inakuwaje kama wanaohusika ni Washirikina?
 
Matatizo ya Kisayansi yanahitaji utatuzi wa Kisayansi... lakini inakuwaje kama wanaohusika ni Washirikina?

Ndo nimesikia baadhi ya watu wakidai eti hizi ajali zilizofuliliza mwaka huu ni za kishirikiana kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015.

Hii nchi watu wataangamia kwa kuamini katika ushirikina.
 
Ukiangalia mabas ya Tz yakipata ajali ni kama limepigwa bomu lisilo la kawaida.

Hili ni swali "zuri mabasi yetu yanaunganishwa wapi?"
 
Ndo nimesikia baadhi ya watu wakidai eti hizi ajali zilizofuliliza mwaka huu ni za kishirikiana kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015.

Hii nchi watu wataangamia kwa kuamini katika ushirikina.

kuna ripoti niliisoma kuhusu ajali tanzania,inasema zaidi ya 50% ya ajali za tz ni human error....ubovu wa magari na barabara zinachangia asilimia ndogo sana....na mimi naweza kuongeza
1.hawa wenye mabasi wanapita hizi barabara kila siku wanajua kila km ya hizi barabara ikoje kwahio kwao ubovu wa barabara wanaujua hivyo walitakiwa wawe makini zaidi ya wale amateurs wanaosafiri xmas to xmas
2.ubovu wa magari kama kweli wewe ni dereva wa hilo gari lazima utajua ubovu wake...mimi gari yangu najua ubovu wake wote...dereva kabla ya kuendesha gari safari ndefu anaikagua,anaona ana tairi kipara lakini anashindana na mwenzie mwenye tairi mpya!!!

mwisho wa yote human error ndio inatucost....jinsi haya mabasi yalivyotengenezwa haiwezi kusaidia kama mtu anaamua kuliendesha kama kichaa.....
 
Back
Top Bottom