Fistula: Sababu, dalili, athari na tiba

Chatumkali

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
2,038
458
Nimesumbuliwa na hilo tatizo kwa miaka miwili sasa, nilianza kutibu kwa kutumia ANUSOL SUPPOSITORY bila mafanikio,nimefanyiwa upasuaji mdogo mala tatu katika kipindi cha kuanzia march hadi sasa lakini bado sijapata nafuu kwa sababu kikovu cha kidonda bado kinauma sana sana.

Kifupi tatizo bado halijaisha kabisa, naomba kwa yeyote anayefahamu dawa mbadala tofauti na upasuaji anisaidie kupitia jukwaa hili ili nimalize kabisa hili tatizo.

1594882333134.png
Ugonjwa wa nasuri almarufu kama fistula unaweza kuwasababishia wanawake athari kubwa katika maisha yao. Mara nyingi maradhi hayo huwakumba wanawake kutokana na matatizo wakati wa kijifungua.

Wasichana wanaopata mimba za mapema na kujifungua na wale ambao wamekeketwa wamo katika hatari kubwa ya kupata maradhi hayo.

Ugonjwa huo aidha unaweza kuzuiliwa na vile vile aliyeathirika tayari, anaweza kufanyiwa tiba kupitia upasuaji.

Ugonjwa wa Nasuri ni nini?
Nasuri almaarufu Fistula ni shimo ambalo hutokea katikati ya kibofu cha mkojo na uke au katikati ya njia ya haja kubwa na uke wa mwanamke ambaye amejifungua kwa shida. Shimo hutokea pale ambapo kichwa cha mtoto ni kikubwa kuliko njia ya uzazi.

Fistula inasababishwa na kusukuma mtoto wakati wa kujifungua kwa mda mrefu bila usaidizi au matibabu yeyote, na anachanika katika njia ya uzazi na kusababisha shimo, hivyo husababisha uvujaji wa kinyesi na mkojo bila kujizuiia.

Aidha kujifungua mapema kabla ya umri kumekuwa chanzo kikubwa cha kutokea fistula, hilo linatokana na kutopevuka kwa njia za uzazi pamoja na nyonga.

Wataalamu wa afya wanabaini fistula mara nyingi hutokea kwa wanawake wanaojifungulia majumbani baada ya kukosa matibabu. Ni vema na wajibu kwamba mara kwa mara kwa wajawazito kujifungua katika kituo cha matibabu ili waweze kufuatiliwa na kupata huduma za matibabu kwa wakati mwafaka.

Fistula hutokana na matatizo wakati wa kujifungua wakati mwanamke huchukua muda mrefu kabla hajajifungua. Tatizo hili huwaathiri pakubwa wasichana ambao wanapata mimba za mapema na kujifungua kabla mifupa ya sehemu za kizazi haijakomaa ipasavyo.

Vile vile wanawake ambao tundu la kizazi chao ni dogo sana au wale ambao wamekeketwa wako katika hatari kubwa ya kupata maradhi hayo.

Dalili
Kama unahisi kutokwa na mkojo bila kujizuia, harufu mbaya, maumivu makali sahemu za uzazi unashauliwa kuwahi hospitali au kituo cha afya kilicho karibu ili upate ushauri na matibabu zaidi. Matibabu ya fistula ni bure katika hospitali zote nchini.

Atahri za fistula
Kwa kuwa fistula ni tundu kwenye misuli kati ya uke na kibofu cha mkojo, wanawake ambao wameathirika na maradhi haya huvuja mkojo mara kwa mara bila kukusudia.

Harufu mbovu ya mkojo huo huwafanya waathiriwa kutengwa kwa kudhaniwa ni wachafu.

Familia nyingi huvunjika kutokana na unyanyapaa. Matatizo mengine ya kiafya yanayotokana na maradhi hayo ni ukosefu wa maji ya kutosha mwilini na utapiamlo.

Kuzuia
Ni rahisi kuzuia ugonjwa huu iwapo mama atapata usaidizi wa haraka wa kimatibabu.

La muhimu haswa ni wasichana na wanawake wapate ushauri jinsi wanavyoweza kuepukana na mimba za mapema kwani miili yao huwa haijakomaa ipasavyo ili kukabiliana na uja uzito na uchungu wa kujifungua.

Wasichana wanaoshika mimba wakiwa wangali wachanga wamo katika hatari kubwa ya kuathirika na maradhi haya zaidi ya wale ambao wamehitimu miaka 20.

Upasuaji
Fistula ina tiba. Takriban 90% ya visa vya fistula vinaweza kutibiwa kupitia upasuaji ambao huziba tundu hilo.

Wakati mwanamke anazidi kupona ni vyema azidi kufanya mazoezi ya kuimarisha misuli ya uke ili kurejesha hali yake ya kawaida.

Mashirika mengi yasiyo ya serikali, haswa madaktari ambao hutoa huduma za kimatibabu pasi na kuzingatia mipaka, huwatibu wanawake walioathirika na fistula bila malipo.

Kwa kawaida, matatizo ya fistula huwakumba pakubwa wanawake walio katika maeneo ambayo msaada wa matibabu huchukua muda kuwafikia.

Kulingana na utafiti wa shirika la afya duniani WHO, ripoti iliochapishwa na The Citizen, takriban wanawake milioni mbili wameathirika na fistula.

Idadi kubwa ya wagonjwa hao wanaishi katika bara la Afrika huku nusu yao wakiwa kutoka nchini Nigeria. Hata hivyo, hiyo sio idadi kamili kwani wengi wao wanahofia unyanyapaa.

Baadhi ya Michango iliyotolewa na Wadau wa JF

Asante sana kwa ushauri,kwa maelezo niliyopewa awali na daktari ni kwamba,tatizo hili humpata mtu yeyote na husababishwa na ama kuwa na mazoea ya kukaa muda mrefu,ama kusimama muda mrefu,ama kufanyakazi ngumu mda mrefu huku ukiwa wima kama vile kufundisha<mimi ni mwalimu.ama kutokuwa na ratiba nzuri ya kula chakula<irregular time table>
----
Habari wana wa Forum,

Kwa upeo wangu fistula ni ugonjwa wa kutokwa na haja ndogo mara kwa mara na kwa kutokujijua kama unatokwa na haja ndogo na mara nyingi huwatokea mama zetu baada ya kujifungua.

Sasa wana wa forum nahitaji kujua zaidi maana ya huo ugonjwa na dalili na cause zinazopelekea ugonjwa huo kuwapata mama zetu.

Na pia kuna ukweli wa aina yeyote unaosema kwamba fistula kwa asilimia kubwa huwapata wanawake wafupi? Nipe majibu yenu ili nipate kujua zaidi kuhusu ugonjwa wa fistula.
----
Mkuu, fistula by definition is an abnormal communication between two epithelial surfaces, maana Yale ni mawasiliano yasiyo ya kawaida Kati ya sehemu mbili zisizotakiwa kuwa na muingiliano, ndani njia ya mkojo kibosh na uke, njia ya uke na njia ya haja kubwa, koo la hewa na koromeo la chakula. Mara nyingi mawasiliano haya kuwa bi kwa viungo vilivyo karibu karibu.

Wanawake kupata fistula hii Gironde zaidi wakati Wa kujifungua, mwanamke anapokuwa na nyonga ndogp itakayoshindwa kupitisha mtoto na hapa anakuwa mbali na hospitali kupata huduma ya upasuaji kunyoa mtoto.

Hapa wanapata uchungu pingamizi kwa muda mrefu, kichwa cha mtoto kukandamiza sehemu ya uke kwa juu kuna libido cha mkojo na chini kuna njia ya haja kubwa! Sehemu hizi kukandamizwa kwa muda mrefu hupelekea tissue za sehemu hiyo kukosa blood supply na hatimaye kufa na hivyo kuweka tundu.
----
Kila tarehe 23 mwezi Mei ni Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Fistula ya uzazi. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “TUMAINI, UPONYAJI NA HESHIMA KWA WOTE.”

Kwa Tanzania matibabu ya Fistula ni BURE kabisa ikijumuisha nauli ya kumtoa mgonjwa alipo hadi hospitali, chakula, upasuaji na nauli ya kumrudisha. Hii ni katika kuhakikisha Fistula ya Uzazi inatokomezwa kabisa nchini ambapo kwa takwimu za mwaka 2014, wanawake takribani 20,000 walikuwa na fistula nchini.

Wanawake 20,000 wana ugonjwa wa fistula Tanzania

FISTULA NI NINI?

Fistula si neno geni kwa wengi wetu ingawa inawezekana tusijue maana halisi ya neno hili. Fistula ni tundu linalounganisha njia mbili za mwili zilizo wazi. Kuna fistula za aina nyingi lakini inayozungumziwa hapa ni Fistula ya Uzazi(Obstetric Fistula).

FISTULA YA UZAZI

Fistula ya uzazi ni tundu lisilo kawaida ambalo halikutakiwa kuwepo kati ya kibofu cha mkojo na njia ya uke(Vesico-Viginal Fistula – VVF) au kati ya njia ya haja kubwa na uke(Recto-Vaginal Fistula – RVF). Wanawake wengi hupata VVF, wachache RVF na wachache zaidi hupata zote kwa pamoja.

SABABU ZA KUTOKEA KWA FISTULA

Uzazi Pingamizi


Fistula mara nyingi hutokana na Uzazi pingamizi(Obstructed labour) wa muda mrefu ambao haukuhudumiwa kwa wakati mwafaka. Hali hii inapotokea kunakuwa na msuguano kati ya mfupa katika nyonga na kichwa cha mtoto unaopelekea jeraha katika njia ya haja kubwa au ndogo ambalo baadaye hugeuka kuwa tundu.

Uzazi au uchungu pingamizi ni uzazi usioendelea aidha kwa sababu mtoto ni mkubwa kuliko njia ya uzazi, nyonga za mama kuwa na tatizo(aidha mama hakuwa na ukuaji mzuri kutokana na utapiamlo utotoni au ajali iliyoathiri nyonga) ama ulalo mbaya wa mtoto tumboni.

Upasuaji

Upasuaji kwa ajili ya uzazi au matibabu mengine katika viungo vilivyopo maeneo ya nyonga huweza kusababisha fistula. Hii hutokea pale daktari ama kwa bahati mbaya ama uzembe anatoboa kuta za njia ya haja kubwa au ndogo ya mgonjwa na kusababisha fistula.

Mionzi

Mionzi kwa ajili ya matibabu ya Saratani ya Shingo ya Uzazi huweza kusababisha fistula kwa kuua seli na kupelekea tundu.

Majeraha/Magonjwa ya Kuambukiza

TB ya Kibofu

Majeraha ukeni


DALILI ZA FISTULA

Dalili kuu ya fistula ni mwanamke kutokwa na haja kubwa au ndogo bila ridhaa yake au bila kujua.

Nyinginezo:-

Vidonda sehemu za siri

Kuchechemea kutokana na maumivu yatokanayo na uzazi pingamizi

MADHARA YA FISTULA

Kimwili


Mwanamke kutokwa na haja ndogo au haja kubwa ama vyote kwa pamoja bila kutambua wala kuwa na uwezo wa kuzuia hali hiyo.

Kuungua au kutokwa na vidonda sehemu za siri vitokanavyo na kemikali zilizopo kwenye mkojo.

Kupoteza uwezo wa kuzaa.

Kupoteza uwezo wa kujamiiana.

Kijamii

Unyanyapaa wa mtu binafsi na jamii kwa ujumla

Kutelekezwa ama kutalikiwa na mume au mwenza

Kushindwa kushiriki shughuli za kijamii


Kisaikolojia

Kushuka moyo (Sonona)

Aibu na Kutojiamini

Kujiua kwa baadhi ya wanawake kwa kukosa tumaini (85% hupoteza watoto wao pia)

Kiuchumi

Kushindwa kufanya shughuli za kiuchumi na kuishi maisha ya dhiki.

MATIBABU

Matibabu ya Fistula ni kwa nja ya Upasuaji wa kuziba tundu/matundu yaliyojitokeza.

Baada ya hapo mwanamke huwekewa mpira wa haja ndogo kwa muda wa siku 14 ili njia iweze kupona na baada ya hapo huangaliwa kama amepona.

Baadhi ya wanawake hufikishwa hospitali wakiwa na kibofu cha mkojo kilichoharibika kabisa hivyo hufanyiwa upasuaji na kutengenezewa kibofu cha bandia katika sehemu ya haja kubwa hivyo hujisaidia haja zote kwa pamoja.

Fistula ni ugonjwa wa aibu na fedheha kwa wanawake na hupelekea waathirika kupoteza maana ya maisha hivyo sambamba na upasuaji, huduma za ushauri wa kisaikolojia hutolewa ili kuweza kuwarudishia thamani yao. Mafunzo ya Ujasiriamali pia hutolewa pia ili kuwawezesha wanawake hawa kujiinua kiuchumi na kumudu maisha yao mapya.


KINGA YA FISTULA

Fistula ni ugonjwa ambao unaweza kutokomezwa kabisa endapo hatua sahihi zitachukuliwa

Kuwahi kwenda kujifungulia kwenye kituo cha kutoa huduma za afya

Mama kuhudhuria kliniki ili kujua hatari zozote zilizopo na kupanga mipango ya kuzikabili

Kuzuia mimba za utotoni(Ni rahisi kwa mtoto kupata fistula kwani maungo hayajakua vizuri)

Serikali kuboresha miundombinu na huduma za afya ya uzazi hasa vijijini. Uwepo wa huduma za dharura kama upasuaji au uwepo wa magari ya wagonjwa na barabara thabiti ndio njia pekee ya kutokomeza janga hili.
----
Ni muhimu kwa mjamzito kuanza kuhudhuria kliniki mapema ili kulinda afya yake na mtoto aliye tumboni. Kwa kutambua umuhimu wa kulinda afya ya mama na mtoto, serikali imefanya mapinduzi katika sekta ya afya ikiwa ni ku- jenga miundombinu hasa ujenzi wa vituo vya afya kwa kila kata lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi.

Serikali na taasisi binafsi zime- kuwa na ushirikiano hasa katika kukabiliana na magonjwa yanay- owasibu wajawazito hususani tatizo la fistula.

Fistula ni aina ya ugonjwa ambao huweka shimo kubwa kati ya njia ya uzazi na njia ya mkojo unatokana na mama kuwa na uchungu wa muda mrefu bila matibabu.

Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka hospitali ya CCBRT, Dk. James Chapa, tatizo hilo huwaathiri zaidi wasichana ambao wanapata mimba wakiwa na umri mdogo na kujifungua kabla mifupa ya sehemu za kizazi ikiwa bado haijakomaa ipasavyo.

Anasema wanawake ambao tundu la kizazi chao ni dogo au wale ambao wamekeketwa wako katika hatari kubwa ya kupata maradhi hayo.

Anaeleza kuwa wanawake ambao wameathirika na mara- dhi hayo huvuja mkojo mara kwa mara bila kukusuadia, harufu mbaya ya mkojo hufanya waathirika kutengwa na kunyan- yapaliwa kwa kudhaniwa kuwa ni wachafu.

“Mtatizo mengine yanayoto- kana na maradhi hayo ni ukosefu wa maji ya kutosha mwilini na utapiamlo,” anabainisha.
Dk. Chapa anasema ugonjwa wa fistula humdhalilisha mwan- amke na kumsababishia madhara mengine ya kiafya.
“Ili mwanamke apone ugonjwa huu ni vyema akatibiwe hospi- tali kwani hakuna eneo mbadala ambalo tiba inapatikana.

“Matibabu yakifanyika mape- ma na kuwa na ufasaha majibu huwa mazuri kwa zaidi ya asil- imia 90 hivyo, kama yupo mwe- nye tatizo hili na bado hajafika hospitali afike CCBRT kwaajili ya matibabu,” anasema.

TAKWIMU ZILIVYO
Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), za mwaka 2018 zinaonyesha kuna wanawake takribani milioni mbili wanaishi na fistula duniani.

Inakadiriwa kuwa wagonjwa wapya kati ya 50,000 na 100,00 hupatikana kila mwaka, wakati juhudi za kutibu fistula duni- ani huishia kutibu wagonjwa 20,000 tu.

Idadi kubwa ya wagonjwa wenye fistula wapo zaidi barani Afrika hususan kusini mwa Jangwa la Sahara huku nusu wakiwa nchini Nigeria, mabara mengine ni Asia na Amerika ya Kusini.

Hapa nchini, takwimu za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto zinakadiria kuwa na wanawake takribani 2,500 ambao hupata fistula kila mwaka, huku idadi ya wanaopatiwa matibabu kila mwaka ikiwa ni takribani wa- nawake 1,000 kwa mwaka.

“Katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2015 hadi De- semba, 2019 wanawake zaidi ya 5,500 walitibiwa fistula.

“Mafanikio haya yanatokana na kampeni iliyoendeshwa kwa ushirikiano baina ya serikali na wadau ambayo imeweka mabalozi wa fistula zaidi ya 3,000 nchi nzima wanaosaidia kuratibu rufaa na usafiri kwa wagonjwa kwenda hospitali zinazotoa huduma ya fistula,” anasema Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.

AINA ZA FISTULA
Dk. Chapa anasema zipo fistula ambazo hazisababishwi na masuala ya uzazi.

“Upo ugonjwa wa saratani unaweza kusababisha aina ny- ingine ya fistula, pia matibabu ya mionzi yanaweza kusababi- sha ugonjwa huo.

“Mtu akipata jeraha kuto- kana na ajali yoyote anaweza kupata fistula na magonjwa mengine kama kichocho na kibofu cha mkojo ambayo husababisha fistula,” anasema.

Dk. Chapa anasema upas- uaji nao husababisha fistula na hii huhusisha mirija inapotoa mkojo kwenye figo kupeleka katika kibofu.

“Mirija hii mara nyingi hupita karibu na kizazi na upasuaji huhusisha kizazi, mirija hii ikitokea kukatwa au kufungwa wakati wa upasuaji, pia kibofu cha mkojo kipo ka- ribu na kizazi hivyo wakati wa upasuaji jeraha hutokea eneo la kibofu na kusababisha fistula,” anasema.

INAWEZA KUJIRUDIA
Dk. Chapa anasema mama aliyefanyiwa upasuaji kabla ya kuondoka hospitali ni vyema akamuuliza daktari endapo ku- likuwa na tatizo lolote wakati wa tukio hilo.

“Kuna uwezekano wa kutokea majeraha wakati wa upasuaji hivyo mama anapofa- hamu kama kulikuwa na tatizo akashauriwa nini cha kufanya baada ya kuruhiusiwa.

“Kama kulikuwa na jeraha katika kibofu mama huwekewa mpira wa kutolea mkojo ili apumzishe kibofu cha kutolea mkojo kuanzia siku 10 hadi 14. “Pia mama huyu atashauriwa kunywa maji na kuwa msafi ili kuepusha maambukizi katika viungo vya uzazi,” anasema.

Dk. Chapa anasema mgonjwa aliyetibiwa fistula upo uwezekano wa kuupata ugonjwa huo kwa mara nyingine.

“Tunapowatibu wagonjwa masharti tunayowapa ha- waruhusiwi kujifungua kwa njia ya kawaida baada ya upas- uaji huo, uzazi utakaofuata ni kwa upasuaji ili kumwepusha mtoto kupita njia ya kawaida na kufumua eneo ambalo lilirekebi- shwa,” anasema.

Dk. Chapa anasema mama anashauriwa baada ya miezi minne ndio hupendekezwa kushiriki mapenzi na ataka- poanza kinyume na muda huo uwezekano wa ugonjwa huo kurudi ni mkubwa.

WANAOATHIRIKA ZAIDI
Dk.Chapa anasema wa- naoathiriwa zaidi na fistula ni ambao hawajafika umri salama kwaajili ya uzazi, kuanzia miaka 18 na kuendelea.

“Mtu akipata mimba kabla ya umri huo uwezekano wa kupata fistula ni mkubwa kwa sababu nyonga yake haijakomaa, pia inawapata kina mama wa umri wowote, ukilinganisha na wenye miaka 18 na kuendelea waliopata ujauzito na wenye umri chini ya hapo wanauwezekano wa kupata fistula mbaya zaidi kwa sababu wanapata majeraha makubwa,” anasema.

UELEWA MDOGO
Dk. Chapa anasema bado uelewa wa jamii juu ya ugonjwa fistula ni mdogo. “Watu hawajui chanzo cha ugonjwa na matib- abu yake nini kwahiyo inaathiri mtiririko wa wagonjwa kuja kupata matibabu.

“Kama mtu haamini hili ni tatizo la kawaida ni ngumu kum- shawishi kutafuta matibabu, pia wanapofika hospitali tunakutana na changamoto za afya zao.

“Mtu anakuja akiwa na upungufu wa damu, magonjwa mengine ambayo hayakutibika vizuri kama presha na kisu- kari ambayo hutupa changamoto kumhudumia mgonjwa vizuri,” anasema.

Changamoto nyingine anayoi- taja Dk. Chapa ni tatizo la kiakili ambalo huwakumba wagonjwa hao.“Wengine wanakuja tayari wana shida ya kiakili kum- saidia inakuwa changamoto, kwa sababu matibabu yetu yanahitaji ushirikiano baina ya wataalamu na mgonjwa mwenyewe.

Baada ya upasuaji mgonjwa anapaswa kuwa katika mashine ya kutolea mkojo kwa siku 14 na anahitajika kunywa maji kila siku.

“Kwahiyo, mtu ambaye akili haikuwa sawa hawezi kufuata masharti baada ya upasuaji hivyo tunajitahidi muda wote kukabiliana nao.

Pia baada ya upasuaji watu hawafuati masharti tunayotoa baada ya upasuaji ndio maana utakuta wengine ugonjwa hu- rudi,” anasema.

UMASKINI NI TATIZO
Furaha Mafuru, ni Ofisa Programu Kitengo cha Mama na Mtoto Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), anasema tatizo la fis- tula huwapata wanawake wengi wasio na kipato cha kutosha, hali ambayo huwasababisha kwenda kujifungulia kwa wakunga wa jadi au nyumbani.

“Kwa sababu hawana uwezo inakuwa ni changamoto kwao ku- toka nyumbani kwenda hospitali kwaajili ya matibabu, hii huwa chanzo cha wao kupata ugonjwa huu kutokana na kuchelewa mat- ibabu,” anasema.

Anasema katika kuimarisha huduma za haraka za kujifungua, serikali ikishirikiana na wadau uboreshaji mkubwa wa vituo vya kutoa huduma haraka ume- fanyika.

“UNFPA ikishirikiana na serikali imeboresha vituo katika Mkoa wa Simiyu Kigoma katika kipindi cha miaka miwili, tume- karabati vituo vya afya 40 Simiyu na vituo sita Kigoma na sasa kina mama walio mikoa ya pembezoni kwasasa hawapati shida kwa sababu vituo vilivyoboreshwa vimewekwa vifaa na kina mama wanapatiwa mafunzo ya kukabili- ana na hatari yoyote wakati wa kujifungua,” anasema.

HATUA ZINAZOCHUKULIWA NA SERIKALI
Kutokana na kuimarishwa kwa huduma, Waziri Ummy anasema idadi ya wanawake wanaojitokeza kutibiwa fis- tula katika hospitali za CCBRT, Bugando, Nkinga na Kuvulini Maternity Center, imepungua kwa zaidi ya asilimia 30.

“2016 walikuwa wagonjwa 1356; mwaka 2017 idadi hiyo ikashuka na kufikia 1060, mwa- ka 2018 ikashuka tena na kufikia idadi ya wanawake 900, na 2019 ikashuka zaidi na kufikia wa- nawake 852.

“Hii imetokana na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za upasuaji wa dharura chini ya uongozi wa Rais Dk. John Magu- fuli,” anasema.

Ummy anasema serikali imei- marisha huduma kwa wajawa- zito, hatua ambayo imesaidia kupunguza matatizo ya fistula kwa wanawake wengi nchini.

“Wajawazito waliotimiza mahudhurio manne au zaidi (ANC4+) mwaka 2019/20 wali- fikia asilimia 77 ikilinganishwa na asilimia 41 kwa kipindi kama hicho mwaka 2015/2016.

“Kina mama wanaojifungulia vituo vya kutolea huduma imeendelea kuongezeka hadi kufikia asilimia 83 Machi mwaka huu ikilinganishwa na asilimia 64 kwa kipindi kama hicho mwaka 2015/16. “Idadi ya vituo vya afya vinavyotoa huduma ya dharura kwa wajawazito (CEMONC) im- eongezeka na kufikia vituo 352; Machi mwaka 2020 ikilingan- ishwa na vituo 115 mwaka 2015,” anasema.
 
Unaleta utani mi niko serious mkuu,tikerra kama huna msaada constructive waachie real great thinkers wanisaidie mkuu
 
Fistulas
A fistula is an abnormal channel from a hollow body cavity to the surface (for example, from the rectum to the skin) or from one cavity to another (for example, from the vagina to the bladder). A fistula may be congenital (bladder to navel), the result of a penetrating wound (skin to lung), or formed from an ulcer or an abscess (appendix abscess to vagina, or tooth socket to sinus).
The repeated filling of an abscess or a wound by the fluid contents of some body cavity prevents healing and encourages the formation of a fistula. An anal fistula, for example, begins with inflammation of the mucous lining of the rectum. The area becomes an abscess as it is constantly reinfected by feces; eventually a fistula breaks through to the skin near the anus. The usual treatment is an operation to open the fistula channel completely and drain any abscess so it does not recur.
image003.jpg
 
Nimesumbuliwa na hilo tatizo kwa miaka miwili sasa,nilianza kutibu kwa kutumia ANUSOL SUPPOSITORY bila mafanikio,nimefannyiwa upasuaji mdogo mala tatu katika kipindi cha kuanzia march hadi sasa lakini bado sijapata nafuu kwa sababu kikovu cha kidonda bado kinauma sana sana,kifupi tatizo bado halijaisha kabisa,naomba kwa yeyote anaefahamu dawa mbadala tofauti na upasuaji anisaidie kupitia jukwaa hili ili nimalize kabisa hili tatizo

Jaribu hii maji ya ganda la mgomba unaliponda na kupaka kwenye unyeo kutwa mara tatu kwa wiki mbili.mi nimepona .anusol haikunisaidia pamoja na kuitumia kwa miaka miwili .mgomba just two wiki.
 
Ndio kwanza nimeickia hii anal fistula...pole ndugu,...ila ningkua na raha zaidi kama ningejua imetokana na nn?
 
Nimesumbuliwa na hilo tatizo kwa miaka miwili sasa,nilianza kutibu kwa kutumia ANUSOL SUPPOSITORY bila mafanikio,nimefannyiwa upasuaji mdogo mala tatu katika kipindi cha kuanzia march hadi sasa lakini bado sijapata nafuu kwa sababu kikovu cha kidonda bado kinauma sana sana,kifupi tatizo bado halijaisha kabisa,naomba kwa yeyote anaefahamu dawa mbadala tofauti na upasuaji anisaidie kupitia jukwaa hili ili nimalize kabisa hili tatizo

Kwanza umeipataje?
 
Asante sana kwa ushauri,kwa maelezo niliyopewa awali na daktari ni kwamba,tatizo hili humpata mtu yeyote na husababishwa na ama kuwa na mazoea ya kukaa muda mrefu,ama kusimama muda mrefu,ama kufanyakazi ngumu mda mrefu huku ukiwa wima kama vile kufundisha<mimi ni mwalimu.ama kutokuwa na ratiba nzuri ya kula chakula<irregular time table>
 
Habari wana wa Forum,

Kwa upeo wangu fistula ni ugonjwa wa kutokwa na haja ndogo mara kwa mara na kwa kutokujijua kama unatokwa na haja ndogo na mara nyingi huwatokea mama zetu baada ya kujifungua. Sasa wana wa forum nahitaji kujua zaidi maana ya huo ugonjwa na dalili na cause zinazopelekea ugonjwa huo kuwapata mama zetu. Na pia kuna ukweli wa aina yeyote unaosema kwamba fistula kwa asilimia kubwa huwapata wanawake wafupi? Nipe majibu yenu ili nipate kujua zaidi kuhusu ugonjwa wa fistula.
 
Mkuu, fistula by definition is an abnormal communication between two epithelial surfaces, maana Yale ni mawasiliano yasiyo ya kawaida Kati ya sehemu mbili zisizotakiwa kuwa na muingiliano, ndani njia ya mkojo kibosh na uke, njia ya uke na njia ya haja kubwa, koo la hewa na koromeo la chakula. Mara nyingi mawasiliano haya kuwa bi kwa viungo vilivyo karibu karibu.

Wanawake kupata fistula hii Gironde zaidi wakati Wa kujifungua, mwanamke anapokuwa na nyonga ndogp itakayoshindwa kupitisha mtoto na hapa anakuwa mbali na hospitali kupata huduma ya upasuaji kunyoa mtoto.

Hapa wanapata uchungu pingamizi kwa muda mrefu, kichwa cha mtoto kukandamiza sehemu ya uke kwa juu kuna libido cha mkojo na chini kuna njia ya haja kubwa! Sehemu hizi kukandamizwa kwa muda mrefu hupelekea tissue za sehemu hiyo kukosa blood supply na hatimaye kufa na hivyo kuweka tundu.
 
Mkuu, fistula by definition is an abnormal communication between two epithelial surfaces, maana Yale ni mawasiliano yasiyo ya kawaida Kati ya sehemu
Mbili zisizotakiwa kuwa na muingiliano, ndani njia ya mkojo kibosh na uke, njia ya uke na njia ya haja kubwa, koo la hewa na koromeo la chakula. Mara nyingi mawasiliano haya kuwa bi kwa viungo vilivyo karibu karibu.
Wanawake kupata fistula hii Gironde zaidi wakati Wa kujifungua, mwanamke anapokuwa na nyonga ndogp itakayoshindwa kupitisha mtoto na hapa anakuwa mbali na hospitali kupata huduma ya upasuaji kunyoa mtoto. Hapa wanapata uchungu pingamizi kwa muda mrefu, kichwa cha mtoto kukandamiza sehemu ya uke kwa juu kuna libido cha mkojo na chini kuna njia ya haja kubwa! Sehemu hizi kukandamizwa kwa muda mrefu hupelekea tissue za sehemu hiyo kukosa blood supply na hatimaye kufa na hivyo kuweka tundu Kati ya uke na kibofu
Cha mkojo ndo unaona wanatoka mkojo muda wote au kinyesi kutokea

Asante kwa kunisaidia kujua maana yake ila ni kweli hupata wanawake wafupi?
 
asante kwa kunisaidia kujua maana yake ila ni kweli hupata wanawake wafupi?

Mwanamke mwenye nyonga nyembamba itakayoshindwa kupitisha mtoto na akakosa huduma ya dharura ya upasuaji ataweza kupata fistula. Mwanamke anaweza kuwa mfupi akawa na mtoto ambaye ni mdogo na akazaliwa bila shida.

Sio kila mwanamke mfupi anapata fistula. Muhimu kupeleka mama mjamzito hospitali mapema anapoanza uchungu madaktari watapima njia na kuangalia kama mtoto atapita.
 
Habari zenu wana JF

Samahani naomba msaada kwa mtu yeyote ambaye anajua sehemu gani wapo maspecialist wa FISTULA, Nikimaanisha daktari bingwa wa kutibu fistula!, nimejaribu kufika CCBRT lakini nimeambiwa pale wanadeal na fistula kwa wanawake tu. Ahsanteni
 
habari zenu wana JF

Samahani naomba msaada kwa mtu yeyote ambaye anajua sehemu gani wapo maspecialist wa FISTULA, Nikimaanisha daktari bingwa wa kutibu fistula!, nimejaribu kufika CCBRT lakini nimeambiwa pale wanadeal na fistula kwa wanawake tu. Ahsanteni

Hivi kuna fistula ya wanaume? Mimi ninavyofahamu fistula ni kwa wanawake tu, maana ni tatizo wanalolipata wakati wa kujifungua
 
Hivi kuna fistula ya wanaume? Mimi ninavyofahamu fistula ni kwa wanawake tu, maana ni tatizo wanalolipata wakati wa kujifungua

Ndio kaka fistula inampata mtu yeyote na tena inaweza kutokea sehemu yeyote ya mwili wa binadamu, inayowapata wanawake pia ni aina mojawapo ya fistula, tafadhari hebu tembelea wavuti hii.
 
Wataalamu bingwa wapo hospitali ya CCBRT Msasani, Muhimbili na KCMC
 
Tufahamu maana halisi ya fistula ni communication baina ya two thing n ya body inaweza kuwa veaicalvaginal enterocutaneous rectovesical waterin can in men with obstructive uropathy

So fistula as a fistula can be to everyone ie every sex
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom