BABA JUNJO
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 241
- 14
Hii ni story ya kutungwa.
Hakikutokea kitu kama hiki, hata walinzi waliokuwa zamu siku hiyo wanashangaa mtu anaweza kuandika uongo kama huu.
Thibitisha.
Hii ni story ya kutungwa.
Hakikutokea kitu kama hiki, hata walinzi waliokuwa zamu siku hiyo wanashangaa mtu anaweza kuandika uongo kama huu.
1. hakuna aliyehukumiwa kwenye kesi hii hivyo wote bado ni innocent
2. Issue ya kuingiza gari geti la mbele au nyuma ni kazi za walinzi au watu wa protocal hivyo ni non issue
3. Tangu lini ikulu ikawa ya Nyerere? Ikulu ni ya waTanzania wote au ushasahau kama nyerer naye alikuwa na secretary wake ambaye alikuwa CIA kwenye hiyo hiyo ikulu yetu?
4. Wikileaks doc...hosea mwenyewe anasema tatizo sio watu kupewa kamisheni ya 30% bali je ni halali?
5. Dont hate the player, hate the game...considering huyo Hosea naye ana kashfa za kifisadi pia
Nachukia kuona Rais anakenuakenua meno kama mbayuwayu
Ilikuwa ni siku ya Desemba 9, 2010. Tanzania ilikuwa inasherehekea miaka 49 ya Uhuru wa taifa. Baada ya kukagua gwaride Uwanja wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete alifanya dhifa ya kitaifa Ikulu na kualika viongozi wa serikali, mabalozi, viongozi wa dini na wafanyabiashara wakuu.
Waalikwa wote, walikuwa wanaingia Ikulu kupitia mlango wa nyuma ulio karibu na bahari upande wa ferry. Lango kuu la kuingia Ikulu lilikuwa halitumiki kwa wageni siku hiyo na lilitumiwa na Rais na viongozi wengine wakuu. Magari yote, ikiwemo ya mawaziri na mabalozi yalipaki nje ya Ikulu kwenye uwanja mkubwa ulio karibu na ferry na wageni waalikwa waliingia kwa mguu kwenye viwanja vya Ikulu.
Mmoja wa wageni waalikwa mashuhuri wa Kikwete alikuwa ni Tanil Somaiya, mmiliki wa Shivacom Group of Companies.
Wakati mawaziri na mabalozi waliambiwa na maafisa usalama Ikulu watumie mlango wa nyuma wa kuingia Ikulu na kutembea mpaka kwenye gardens ambako sherehe ilifanyika, Tanil alipewa heshima ya kipekee na kuruhusiwa kutumia main entrance gate.
Tanil aliingia Ikulu na gari la kifahari jekundu (a red FERRARI) na kuipaki gari hiyo kwenye mlango mkuu wa kuingia IKULU ambako huwa gari la Rais ndipo linapaki.
Aliiacha FERRARI hiyo hapo kwenye lango la kuingia Ikulu kwa zaidi ya masaa mawili huku akijimwaga kwenye dhifa.
Mawaziri, mabalozi na vigogo wengine walibaki wamepigwa na butwaa iwaje wageni wote waambiwe waingie Ikulu kupitia mlango wa nyuma kwa mguu na kuacha magari yao nje halafu mfanyabiashara huyu apite main gate na kuweka gari lake kwenye main entrance ya lango kuu la kuingia Ikulu.
Tanil ni rafiki wa karibu na business partner wa Shailesh Vithlani, mfanyabiashara ambaye amekimbia nchi kutokana na kashfa ya rada.
Tanil, ambaye ametajwa kwenye WikiLeaks kuhusu rada, amehusishwa pamoja na Vithlani kwenye kashfa ya rada, military trucks, military choppers, Gulfstream presidential jet na scandal nyingine.
Inaeleweka kuwa Tanil alimchangia pesa nyingi sana Kikwete kwenye uchaguzi wa Rais uliopita na pia alitoa helikopta zake zitumike kwenye kampeni ya CCM, lakini hii ndivyo Ikulu ya Mwalimu Julius Nyerere inavyodharauliwa siku hizi?
Kwa kutumia main entrance na kupaki gari lake mbele ya lango kuu la Ikulu, Tanil alikuwa anataka kuwaonesha wageni wote kuwa yeye yuko karibu sana na Rais wa nchi na Ikulu ni kama nyumbani kwake.
Mbaya zaidi, kufuru hii ilifanywa siku ambayo Tanzania inaadhimisha uhuru wake. Kuna uhuru kamili kweli kama watuhumiwa wakubwa wa ufisadi wanafanya kufuru namna hii mpaka IKULU?
Unatarajia kweli Edward Hoseah wa PCCB anaweza kuondokana na uoga wa kumkamata Tanil kwa ufisadi wa rada wakati Rais wa nchi ni besti wake na Ikulu ni kama playground yake?
Kishongo ukitaka tukuamini lazima utuambie hao walinzi ulikutana nao lini? Na kwa shughuli gani? Na vile vile ulijuaje ya kuwa ni walinzi waliokuwa kwenye zamu siku husika?
Tuseme nini sasa.Ni kama kupigia mbuzi gitaa.
hakuna hata mmoja aliye corroborate hii hadithi?
hakuna cha siku wala saa... ni ndoto za mchana tu ndugu yanguIko siku!
Hata wakati wa Mwinyi mambo yalikuwa similar na tunavyoona sasa.................... Nchi hii inawataka watu kama Slaa na Pombe Magufuri then heshima ya serikali itarudi.
Hata wakati wa Mwinyi mambo yalikuwa similar na tunavyoona sasa.................... Nchi hii inawataka watu kama Slaa na Pombe Magufuri then heshima ya serikali itarudi.