Fisadi wa Rada, Tanil Somaiya afanya kufuru IKULU

1. hakuna aliyehukumiwa kwenye kesi hii hivyo wote bado ni innocent

2. Issue ya kuingiza gari geti la mbele au nyuma ni kazi za walinzi au watu wa protocal hivyo ni non issue

3. Tangu lini ikulu ikawa ya Nyerere? Ikulu ni ya waTanzania wote au ushasahau kama nyerer naye alikuwa na secretary wake ambaye alikuwa CIA kwenye hiyo hiyo ikulu yetu?

4. Wikileaks doc...hosea mwenyewe anasema tatizo sio watu kupewa kamisheni ya 30% bali je ni halali?

5. Dont hate the player, hate the game...considering huyo Hosea naye ana kashfa za kifisadi pia

RAFIKI YA JK
Nataka kuchangia hiyo ya 5
ndo maana tunasema ccm itoke kabisa kwa sababu tunauchukia mchezo wa ccm na hatumchukii huyo rafiki yako.
kwa hiyo kama hoseah anakashfa za ufisadi asiseme ukweli amerepent na tunataka wanaccm mafisadi mtubu pia.
Hii ya kusema mbona hata flani yupo hivyo ni kufanya mapambano yawe magumu zaidi tunafanya kwa ajili ya nani sasa.??
 
Hili ndilo Ombwe la uongozi ambalo uongozi wa CHADEMA umekuwa ukijaribu kulinusuru Taifa kuondokana nalo. Taifa liko kwenye hangover kubwa ya uongozi, watanzania wenye mapenzi na nchi hii tuendelee bila kuchoka kuliombea Taifa letu na kuwaelimisha wenzetu wachache waliobaki na mawazo mgando kutoendelea kushabikia ujinga huu.

Dr. Slaa alisema wakati wa kampeni zake kuwa ni hatari na janga kubwa kuendelea kuliacha Taifa hili mikononi mwa huyu mkwere na CCM ulaji yake! CCM ya Nyerere haikuwa hii tunayoiona leo, na wala haitakuwa tena. Hiki ni chama kinachosubiri kifo chake mwaka 2015, maana wengi waliomo humo ni viongozi maslahi, kikipoteza madaraka wataikimbia hata nchi na ndio maana wanajilimbikizia mali wakijua kuwa wako mguu mmoja ndani, na mguu mmoja nje.

Mungu tusamehe watanzania kwa ujinga huu, endelea kulikumbuka Taifa ulilolipenda sana, tujalie nguvu ya kulirudisha Taifa lako mikononi mwa wazarendo kabla au ifikapo mwaka 2015.
 
Hao Ndio # wani bana... Wamesubiri uchaguzi uishe waongeze umeme na mgao kutuadhibu kwa kutunyenyekea miezi m3 ya kampeni!!
Na bado wnatulipisha deni la Dowans!!
 
Nahisi MUNKALI kunipanda baada ya kusoma post 64 zilizotangulia. Hili ni swala dogo kwa kimo lakini ni kubwa kimaudhui kutokana na mazingira yanahusiswa na huyo mtu na hizo preferential treatments. Kama hii taarifa ni ya kweli basi sina la kusema.
 
...Kishongo, hekima ya jibu inasema 'if you say that is not X then say it is Y' sasa tuambie ukweli ulivyo. Otherwise, karibu supu ya pweza hapa Tanga Resort Beach!
 
Duuuh, mimi nilikuwepo kwenye dhifa hii. Kwa kweli niliona kuna sports car kali nyekundu imepaki ndadi ya Ikulu tena nikajiuliza na mwenzangu ule mchuma wa Ridhiwani nini mbona umepaki ndani ya Ikulu wakati wote tumeambiwa tuache magari nje. Kumbe ilikuwa ni FERRARRI ya Tannil Somaiya? Toba!
 
Nachukia kuona Rais anakenuakenua meno kama mbayuwayu

Mhh...watu wana hasira. Nadhani lets us convince all eligible people to vote in 2015. I believe if only 70% of elligible people votes then mabadiliko ya kweli yatakuwepo.
 
Mbona tittle na habari haviendani? Nini maana ya kufuru? Au wewe hujui kiswahili? Kweli wewe ni zezeta.
 
Ilikuwa ni siku ya Desemba 9, 2010. Tanzania ilikuwa inasherehekea miaka 49 ya Uhuru wa taifa. Baada ya kukagua gwaride Uwanja wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete alifanya dhifa ya kitaifa Ikulu na kualika viongozi wa serikali, mabalozi, viongozi wa dini na wafanyabiashara wakuu.

Waalikwa wote, walikuwa wanaingia Ikulu kupitia mlango wa nyuma ulio karibu na bahari upande wa ferry. Lango kuu la kuingia Ikulu lilikuwa halitumiki kwa wageni siku hiyo na lilitumiwa na Rais na viongozi wengine wakuu. Magari yote, ikiwemo ya mawaziri na mabalozi yalipaki nje ya Ikulu kwenye uwanja mkubwa ulio karibu na ferry na wageni waalikwa waliingia kwa mguu kwenye viwanja vya Ikulu.

Mmoja wa wageni waalikwa mashuhuri wa Kikwete alikuwa ni Tanil Somaiya, mmiliki wa Shivacom Group of Companies.

Wakati mawaziri na mabalozi waliambiwa na maafisa usalama Ikulu watumie mlango wa nyuma wa kuingia Ikulu na kutembea mpaka kwenye gardens ambako sherehe ilifanyika, Tanil alipewa heshima ya kipekee na kuruhusiwa kutumia main entrance gate.

Tanil aliingia Ikulu na gari la kifahari jekundu (a red FERRARI) na kuipaki gari hiyo kwenye mlango mkuu wa kuingia IKULU ambako huwa gari la Rais ndipo linapaki.

Aliiacha FERRARI hiyo hapo kwenye lango la kuingia Ikulu kwa zaidi ya masaa mawili huku akijimwaga kwenye dhifa.

Mawaziri, mabalozi na vigogo wengine walibaki wamepigwa na butwaa iwaje wageni wote waambiwe waingie Ikulu kupitia mlango wa nyuma kwa mguu na kuacha magari yao nje halafu mfanyabiashara huyu apite main gate na kuweka gari lake kwenye main entrance ya lango kuu la kuingia Ikulu.

Tanil ni rafiki wa karibu na business partner wa Shailesh Vithlani, mfanyabiashara ambaye amekimbia nchi kutokana na kashfa ya rada.

Tanil, ambaye ametajwa kwenye WikiLeaks kuhusu rada, amehusishwa pamoja na Vithlani kwenye kashfa ya rada, military trucks, military choppers, Gulfstream presidential jet na scandal nyingine.

Inaeleweka kuwa Tanil alimchangia pesa nyingi sana Kikwete kwenye uchaguzi wa Rais uliopita na pia alitoa helikopta zake zitumike kwenye kampeni ya CCM, lakini hii ndivyo Ikulu ya Mwalimu Julius Nyerere inavyodharauliwa siku hizi?

Kwa kutumia main entrance na kupaki gari lake mbele ya lango kuu la Ikulu, Tanil alikuwa anataka kuwaonesha wageni wote kuwa yeye yuko karibu sana na Rais wa nchi na Ikulu ni kama nyumbani kwake.

Mbaya zaidi, kufuru hii ilifanywa siku ambayo Tanzania inaadhimisha uhuru wake. Kuna uhuru kamili kweli kama watuhumiwa wakubwa wa ufisadi wanafanya kufuru namna hii mpaka IKULU?

Unatarajia kweli Edward Hoseah wa PCCB anaweza kuondokana na uoga wa kumkamata Tanil kwa ufisadi wa rada wakati Rais wa nchi ni besti wake na Ikulu ni kama playground yake?

Hadi mwaka 2015 tutakuwa tumechoka na hizi habari.
 
Kishongo ukitaka tukuamini lazima utuambie hao walinzi ulikutana nao lini? Na kwa shughuli gani? Na vile vile ulijuaje ya kuwa ni walinzi waliokuwa kwenye zamu siku husika?

Ili nini? Maana hapa siyo mahakamani kama hutaki kuamini kaa kimya endelea na mambo mengine! Vinginevyo kwa lugha nzuri ntasema Umetumwa wewe kawaambie waliokutuma kuwa umemkuta hayupo
 
tanzania ni nchi pekee duniani ambayo licha ya kutokuwa na kiongozi wa nchi (rais) wananchi wake wanaishi kwa amani.
 
hakuna hata mmoja aliye corroborate hii hadithi?

Nakubaliana na wewe, jee hakuna wengine waliokuwa hapo kwenye sherehe?

Hii story hata na mimi nina imani ni ya kutungwa labda kama kuna evidence ya picha.

Kwanza yeye kuruhusiwa kuingia na gari maafisa usalama pamoja na walinzi wa Ikulu walikuwa wapi? Halafu hapo tulipoelezwa amepark hiyo gari yake, ina maana hao maafisa wote walisinzia tu?
 
Hata wakati wa Mwinyi mambo yalikuwa similar na tunavyoona sasa.................... Nchi hii inawataka watu kama Slaa na Pombe Magufuri then heshima ya serikali itarudi.



samahani magufuli ni wale wale hana moral authority kukemea uovu so my friend choose another one to compare with dr slaa and not magufuli!
 
Mkubwa hii ndio Tanzania yetu ya miaka 49 ya uhuru na hao ndio viongozi wetu ila wakumbuke "every begining has an end" na "What goes around comes around"
 
Back
Top Bottom