Finally: Nimeanza rasmi kilimo cha miti ya mbao Iringa

mkuu nazungumzia Miti ya kisasa kama pine na eucalyptus (milingoti) ambayo inatumia muda mfupi kukomaa sio ya asili...... kama milingoti ndani ya miaka 5 unaweza kuvuna mirunda au nguzo! so far unaweza kupanda Miti kwa garama ya sh 350,000 kwa ekari Baada ya miaka mitatu ukauza sh mil 1.5 kwa ekari... imagine ukiwa na ekari 20 una sh ngapi???
Nimekuelewa sasa mkuu ngoja tujipange na hiyo fursa
 
mkuu nazungumzia Miti ya kisasa kama pine na eucalyptus (milingoti) ambayo inatumia muda mfupi kukomaa sio ya asili...... kama milingoti ndani ya miaka 5 unaweza kuvuna mirunda au nguzo! so far unaweza kupanda Miti kwa garama ya sh 350,000 kwa ekari Baada ya miaka mitatu ukauza sh mil 1.5 kwa ekari... imagine ukiwa na ekari 20 una sh ngapi???
Mkuu nina swali kidogo
Baada ya kuvuna hiyo miti inachipua tena au itabidi kung'oa visiki na kupanda tena?
 
Mkuu nina swali kidogo
Baada ya kuvuna hiyo miti inachipua tena au itabidi kung'oa visiki na kupanda tena?
Miti ya milingoti huchepua Baada ya kukatwa so unaweza kuvuma hata miaka zaidi ya 80. pine ukidhavuna mpaka upande mingine
 
Miti ya milingoti huchepua Baada ya kukatwa so unaweza kuvuma hata miaka zaidi ya 80. pine ukidhavuna mpaka upande mingine
Nikushukuru mkuu ila naomba niendelee kuuliza hii miti ya milingoti inaanza kuvunwa baada ya mda gani? Na baada ya kuivuna wakati inachepua tena itahitaji matunzo kama ulivyoanza kuihudumia awali?
 
Naskia uvunaji wake aka 15-20 lkn wanasemaga unaweza chukua mkopo benki hata m100 hawachomoi,hongera
 
Hata angekuwa above 60, shida iko wapi? Kama mababu zetu wangekuwa na fikra kama zako tusingekuta kitu
Mi nilikuwa nampa challenge tuu kama anaweza kuvumilia na kupambana na changamoto kama kijana hasa uvumilivu kama huo...ila niko pamoja nae sana tuuu
 
Baada ya kuona fursa hii kupitia jukwaa hili nimeamua kuifanyia kazi.
Mwaka huu mwezi wa 8 nikasafiri kuja Iringa mji wa Mafinga nikafanya research na kugundua kweli kilimo hiki kinafanyika na mashamba yanapatikana!
Nikafanikiwa kupata Shamba ekari 5 maendeo ya Ifunda kwa 250,000@ garama za resekali ya kijiji ni 50,000. Kusafisha shamba ikanigharimu 150,000 maana lilikuwa na vichaka.
mwezi huu wa 12 nimefanikiwa kupanda ekari zote miche ya pine kwa gharama zifuatazo. Miche 2250 @sh 100(miche 450 kwa ekari 1) Gharama za wapandaji ni sh 60 kwa kila shimo moja. Mwakani Mungu akipenda Nina lengo la kupanda miche ya milingoti ambayo inawahi kuvunwa kabla ya pine.
Hii ni fursa nzuri kwa wale wenye malengo ya muda mrefu. karibuni
Hi ni habari njema
 
Naskia uvunaji wake aka 15-20 lkn wanasemaga unaweza chukua mkopo benki hata m100 hawachomoi,hongera
uvunaji wa miaka 15-20 ni mashamba ya serekali kama saohill ila kwa wakulima wadogo ni miaka kuanzia 10. ni biashara inayolipa sana kwa mikoa hii ya Iringa na njombe.
 
Nikushukuru mkuu ila naomba niendelee kuuliza hii miti ya milingoti inaanza kuvunwa baada ya mda gani? Na baada ya kuivuna wakati inachepua tena itahitaji matunzo kama ulivyoanza kuihudumia awali?
milingoti unaweza kuvuna kuanzia miaka 5 ambapo unabuna mirunda na miaka 7-9 unavuna nguzo na kuchana mbao. Baada ya kuchepua unaiprun tuu hivyo kuchanua na kupata mirunda au nguzo ila ni vigum kupata mbao coz inakuwa imepinda
 
kweli mkuu ubinafsi ni tatizo....boss wangu anamiaka 3 astaafu ila kapanda Miti zaidi ya ekari 140 ndani ya miaka 3! hapo ndo nazidi kujipa moyo na kusonga mbele.
komaa mkuu.....panda mingi mingi
 
mkuu nazungumzia Miti ya kisasa kama pine na eucalyptus (milingoti) ambayo inatumia muda mfupi kukomaa sio ya asili...... kama milingoti ndani ya miaka 5 unaweza kuvuna mirunda au nguzo! so far unaweza kupanda Miti kwa garama ya sh 350,000 kwa ekari Baada ya miaka mitatu ukauza sh mil 1.5 kwa ekari... imagine ukiwa na ekari 20 una sh ngapi???
Ubarikiwe, umeingiza kitu kichwani mwangu na nitakifanyia kazi.
 
Mkuu kuna mkubwa mmoja serikalini kaanzisha kiwanda cha nguzo za zege. Likatolewa ze tamko kwamba wanataka wasitishe ukataji miti ya nguzo ambayo ni uharibifu wa mazingira. Ukija upande wa pili maliasili nao wanakomalia sana kukata miti. Kuwa makini mkuu
Miti amabayo mali asili wana izungumzia ni miti ya asili kutoka kwenye misitu ya asili na misitu ya serikali. Ila pia nguzo sio lazima ziuzwe tz anaweza kuziuza hata Uganda, Kenya, Rwanda na Somali.
 
Hongera sana mkuu, Na mimi mwaka huu nitafanya huo uwekezaji. Nitanunua Ardhi na kupanda miti. Alafu watz tuache kuwa short sighted miaka 10 ni michache sana.
 
Baada ya kuona fursa hii kupitia jukwaa hili nimeamua kuifanyia kazi.
Mwaka huu mwezi wa 8 nikasafiri kuja Iringa mji wa Mafinga nikafanya research na kugundua kweli kilimo hiki kinafanyika na mashamba yanapatikana!
Nikafanikiwa kupata Shamba ekari 5 maendeo ya Ifunda kwa 250,000@ garama za resekali ya kijiji ni 50,000. Kusafisha shamba ikanigharimu 150,000 maana lilikuwa na vichaka.
mwezi huu wa 12 nimefanikiwa kupanda ekari zote miche ya pine kwa gharama zifuatazo. Miche 2250 @sh 100(miche 450 kwa ekari 1) Gharama za wapandaji ni sh 60 kwa kila shimo moja. Mwakani Mungu akipenda Nina lengo la kupanda miche ya milingoti ambayo inawahi kuvunwa kabla ya pine.
Hii ni fursa nzuri kwa wale wenye malengo ya muda mrefu. karibuni
Kaka hongera sana hii ilikua plan yangu ya mwaka 2016 ila nikashindwa Kwa sababu Fulani Fulani. Kaka naomba msaada wako plzzzzz namba yangu 0712311581 naomba nichek kaka yangu nitumie hata msg
 
yap niko tayari kuvumilia ukizingatia nikisema miaka 10 ni mingi je miaka 10 ilopita nilifanya nn cha maana jib ni hakuna! Hata ningekuwa Nina miaka zaidi 40 sio mbaya coz kuna wategemezi wangu watanufaika nayo mkuu!
Umemjibu vizuri mkuu, unajua wabongo wengi ni waoga wa kuthubutu
 
Kaka hongera sana hii ilikua plan yangu ya mwaka 2016 ila nikashindwa Kwa sababu Fulani Fulani. Kaka naomba msaada wako plzzzzz namba yangu 0712311581 naomba nichek kaka yangu nitumie hata msg
ntakuchek mkuu
 
kilichonishangaza ni huku mufindi ndani ndani kuna hadi raia wa Kenya na Rwanda wamenunua mashamba makubwa na kupanda Miti huku watanzania tunaendelea kupiga soga kuwa hakuna ajira.
naomba name nipeleke huko nifanye research na nianze kupanda miti mweee nalia na njaa wakati sehemu za uwekezaji zipo aisee
 
27 Reactions
Reply
Back
Top Bottom