SDP_TZ_Mpya
Senior Member
- Jun 21, 2013
- 166
- 77
Akihitimisha hoja ya Kamati ya Hesabu ya Fedha za Serikali Kuu (PAC), makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo mh.Deo Filikunjombe (Ludewa) aliyarudia madai ya Mh.Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini) ambaye ni Mwenyekiti wake wa kamati kuwa ni vyama vinne tu ndivyo vilivyoweza kukaguliwa na CAG. Alivitaja vyama hivyo kuwa ni CUF, CCM, NCCR na TLP. Aliendelea na kurusha 'dongo' kuwa vyama vingine vimekataa kukaguliwa. Pia, kwa njia ya kejeli iliyoonekana kuelekezwa CHADEMA, Filikunjombe aliionya CCM kuwa ingawa ni chama chake lkn wasimlaumu baadae kuwa "hukututonya" kuhusu ukaguzi ujao. Hapo alikuwa akikariri maneno ya Zitto kwa CHADEMA alipokituhumu chama hicho kumvua nyadhifa zake kwa "kutokuwatonya" viongozi wake (ingawa yeye mwenyewe Zitto alikuwa ni miongoni wa viongozi wakuu wa chama hicho na ni deputy accounting officer kichama akiwa ni naibu katibu mkuu).
Hata hivyo, baada ya kuhitimisha hoja yake alipitiwa kuomba kutoa hoja. Badala yake aliomba kuwasilisha hoja hadi alipokumbushwa na wenzake na Spika, ndipo alipohitimisha kwa kuomba kutoa hoja.
Mara baada ya hapo, Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni mh.Tundu Lissu (Singida Kaskazini) aliomba mwongozo wa Spika Makinda kuwa maelezo ya Filikunjombe kuhusu Ukaguzi wa hesabu za vyama na CAG yanakinzana na taarifa ya kamati yake. Lissu alifafanua kuwa katika ripoti ya PAC wenyewe wameandika kuwa Msajili wa Vyama vya siasa alishindwa kutoa tangazo kwenye gazeti la serikali juu ya hesabu za vyama tangu mwaka 2009. Kamati imebaini kuwa sababu ni uhaba wa fedha uliomfanya CAG kushindwa kufanya ukaguzi wa vyama vyote. Kamati inasema ni vyama vya CCM na TLP ndio vilikaguliwa. Kama haitoshi, kwenye moja ya mapendekezo ya Kamati ya PAC, Lissu akiinukuu ripoti hiyo, alisema Kamati imependekeza CAG atengewe fedha za kutosha ili kufanikisha ukaguzi wa hesabu za vyama. Hata hivyo Spika Makinda 'aliyeyusha' kwa kusema tu ni sawa mwongozo umesikika na wahusika watazingatia. Alichofanya Spika ni km naibu wake Ndugai jana 'alipoyeyusha' mwongozo wa Mh.Wenje kufuatia taarifa za uwongo zilizotolewa na Mchungaji mh.Assumpter Nshama (Nkenge CCM) juu ya CHADEMA.
Ukidadisi na ku-connect dots na hasa kwa wafuatiliaji huru wa siasa za kitanzania wanaweza kuona wazi kujiingiza kwa Filikunjombe kwenye siasa za Zitto na CHADEMA yake. Hali hii inaweza kuthibisha madai ya muda mrefu ya kuwa Filikunjombe ni mmoja wa wanaotarajiwa kuongoza chama ambacho hakijasajiliwa cha CHAUMMA ambacho kinaelezwa kuundwa na Zitto, Kafulila na Hashim Rungwe.
Hata hivyo, baada ya kuhitimisha hoja yake alipitiwa kuomba kutoa hoja. Badala yake aliomba kuwasilisha hoja hadi alipokumbushwa na wenzake na Spika, ndipo alipohitimisha kwa kuomba kutoa hoja.
Mara baada ya hapo, Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni mh.Tundu Lissu (Singida Kaskazini) aliomba mwongozo wa Spika Makinda kuwa maelezo ya Filikunjombe kuhusu Ukaguzi wa hesabu za vyama na CAG yanakinzana na taarifa ya kamati yake. Lissu alifafanua kuwa katika ripoti ya PAC wenyewe wameandika kuwa Msajili wa Vyama vya siasa alishindwa kutoa tangazo kwenye gazeti la serikali juu ya hesabu za vyama tangu mwaka 2009. Kamati imebaini kuwa sababu ni uhaba wa fedha uliomfanya CAG kushindwa kufanya ukaguzi wa vyama vyote. Kamati inasema ni vyama vya CCM na TLP ndio vilikaguliwa. Kama haitoshi, kwenye moja ya mapendekezo ya Kamati ya PAC, Lissu akiinukuu ripoti hiyo, alisema Kamati imependekeza CAG atengewe fedha za kutosha ili kufanikisha ukaguzi wa hesabu za vyama. Hata hivyo Spika Makinda 'aliyeyusha' kwa kusema tu ni sawa mwongozo umesikika na wahusika watazingatia. Alichofanya Spika ni km naibu wake Ndugai jana 'alipoyeyusha' mwongozo wa Mh.Wenje kufuatia taarifa za uwongo zilizotolewa na Mchungaji mh.Assumpter Nshama (Nkenge CCM) juu ya CHADEMA.
Ukidadisi na ku-connect dots na hasa kwa wafuatiliaji huru wa siasa za kitanzania wanaweza kuona wazi kujiingiza kwa Filikunjombe kwenye siasa za Zitto na CHADEMA yake. Hali hii inaweza kuthibisha madai ya muda mrefu ya kuwa Filikunjombe ni mmoja wa wanaotarajiwa kuongoza chama ambacho hakijasajiliwa cha CHAUMMA ambacho kinaelezwa kuundwa na Zitto, Kafulila na Hashim Rungwe.