Filikunjombe: Sikwenda Kigoma kumsafishia yeyote njia

Mbona kasha irusha clip Facebook angalieni, nasari anasikika akisema kigoma inaweza kutoa rais baada ya miaka 5,10 au 15 hajasema 2015 ivo walicho kanusha ni kweli Gonga hapa umsikie Alichokisema Mhe. Joshua Nassari-Kigoma - YouTube

Nimeisikiliza hiyo clip.

Tukitaka kuwa wakweli, sidhani kama ni sahihi kumlaumu mwandishi wa gazeti la Mwananchi na Bwana Zitto. Hapa siongelei kama Zitto anafaa kuwa Rais au hapana lakini naongelea juu ya ukweli kama Nasari alitamka au hakutamka kuwa Zitto anafaa kuwa Rais. Japo mwandishi hakunukuu neno kwa neno kama alivyotamka Nasari lakini kwa tafsiri pana inaonesha ndivyo alivyokusudia.

Kwenye hili siwezi kumlaumu mwandishi wa gazeti la mwananchi wala Zitto. Nitamlaumu Zitto kama itadhihirika kuwa Nasari alifanya hivyo kwa kuombwa afanye hivyo na Zitto lakini nayo haitaingilia akilini maana Nasari ni mtu mzima tena mbunge ambaye anaowawakilisha wanaamini ana akili, utashi na busara.

Ningekuwa Nasari, nisingehangaika kukanusha maana tofauti ya alichotamka na kilichoandikwa gazetini ni ndogo sana, hasa katika mtazamo wa kisiasa. Kunaweza kuwa na tofauti kubwa kwenye mtazamo wa kisheria.

Zitto alikuwa sahihi kutamka kuwa hawa watu walitamka ila haieleweki kwa nini wanakanusha. Kwa sababu lile lilikuwa ni tamasha, kuna wengine huenda walikwishapitia Serengeti na safari lager au baada ya kuona umati wa watu, wakatokwa na maneno ambayo baadaye baada ya kurudiwa akili hawakuweza kukumbuka kwa nini waliyasema. Tulihangaika sana kuhakikisha Nasari anaupata ubunge lakini sishawishiki sana kama kweli huyu kijana ni makini na ana hekima ya uongozi maana hata ile kauli yake ya kuasema atatangaza Arusha kuwa nchi ilitutia kinyaa. Leo tena anatamka halafu anakanusha. Tumefanikiwa kuongeza mbunge toka Arumeru Mashariki lakini siamini kama tumeongeza nguvu ya maamuzi ya busara bungeni na nje ya bunge.
 
Njia ya mwongo ni fupi! Zitto ni mnafiki na hana nia njema na CDM, Zitto yawezekana ananunua waandishi wa magazeti waaandike utoto na unafiki wake, Na Bahati nzuri wanachadema niwaelewa wanamwelewa vizuri Zitto anavyojipambanua kuwa yeye hatufai si mwenzetu huyu, ni wa kumwogopa kama ukimwi, Namimi nimekuwa nikisema Zitto kwanini anafurahia saana kuungwa mkono na ccm kwenye mambo yake mengi!
 
haya sasa, mimi binafsi bila kumung'unya maneno nilishasema na nitasema daima (mpaka siku abadilike) kuwa zitto kabwe ni mnafiki, na ni kijana hatari kwa mstakabali wa taifa letu kidemokrasia!

Sipingi wazo/ndoto yake ya kuwa rais bali njia anazotumia kuifikia ndoto hiyo ni ya kipuuzi na haikubaliki tuikemee na kuipinga, italiingiza taifa hili kwenye machafuko,

atambue kuwa yeye amebeba dhamana ya tumaini la vijana wengi tena wakware wa fikra machipuko ambao ni hatari zaidi hasa walishwapo hata uongo tu!

Propaganda zake na ccm za kuivuruga chadema zimekuwa zikimulikwa usiku na mchana na kila hatua ya unyayo wake inahesabiwa kwa umakini mkubwa!

Wenzake ndani ya chadema wapo kila kona ya tz wakikijenga chama (m4c) tena kwakujitolea wakila kwa mama ntilie, lakini yeye hata siku moja hajahudhuria mikutano ya chadema tangu alipoenda songea na mwanza kuipiga kampeni za udiwani mwezi wa pili kama si kosei! Amekuwa ni mtu wa ziara binafsi tu kila wiki yupo kwenye ndege, hana tofauti sasa na rais wetu kwa ziara zilivyo:

Hivyo arejee kwenye mikingamo huru ya chama na tafakuri sahihi za ukombozi mororo bila kutumia mbinyo wa kuligawa taifa kwa makundi ya vijana, wazee na watoto!

Tunataka taifa lisimame pamoja, liongee lugha moja na litamalaki pamoja, huku tukijisifu uwepo wa uongozi safi wa kijana mwenzetu zitto zuberi kabwe!!

umenena yericko, siasa za ubinafsi ni hatari sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom