Mkuu Zitto ni kiongozi wa juu wa CDM na ameshiriki kukijenga kipindi hicho akiwa Zitto kweli hivyo mwenendo wake sasa lazima tuhoji.sasa hivi anatumia muda mwingi kujijenga na anatumia kisingizio cha democrasia kuvuruga chama.Uwezo na umakini wa Zitto hauwezi kutusaidia kuleta mapinduzi ya kweli kama ana malengo binafsi.
Tumemwambia mara nyingi kama kijana mwenzetu abadilike lakini amejaa kiburi,majivuno yasiyo na msingi kwa Taifa hili.nafikiri huyu anafaa kupewa idara ya uchumi pale MOEF aachane na siasa au aende huko CCM (ambako wanamsifia kwa kuivuruga CDM lakini HAWAMTAKI).
Viongozi wa CDM tunawaachia hili tumeshasema hadi sauti zimekauka naamini mnachukua hatua kwa umakini ili asikigawe chama.
Kidemokrasia Zitto ni positive change Tanzania. Anahamasisha vijana kuwa huru katika kuenjoy haki zao za kikatiba. Sijaona mahali Zitto akikataza watu kuexercise their freedom. Zitto anatuma ujumbe kwa wapenda demokrasia kuwa CHADEMA haina de facto mgombea wa urais na mgombea atapatikana baada ya mchakato maalum unaoheshimu katiba ya chama. Asiyekubali hilo ndio "hatari kwa mstakabali wa taifa letu kidemokrasia!".
ili aisome hii fanya hivi Zitto njoo ujibu shutuma hizi hapaHaya sasa, mimi binafsi bila kumung'unya maneno nilishasema na nitasema daima (mpaka siku ABADILIKE) kuwa Zitto Kabwe ni MNAFIKI, na ni kijana hatari kwa mstakabali wa taifa letu kidemokrasia!
Sipingi wazo/ndoto yake ya kuwa rais bali njia anazotumia kuifikia ndoto hiyo ni ya kipuuzi na haikubaliki tuikemee na kuipinga, italiingiza taifa hili kwenye machafuko,
Atambue kuwa yeye amebeba dhamana ya tumaini la vijana wengi tena wakware wa fikra machipuko ambao ni hatari zaidi hasa walishwapo hata uongo tu!
Propaganda zake na ccm za kuivuruga chadema zimekuwa zikimulikwa usiku na mchana na kila hatua ya unyayo wake inahesabiwa kwa umakini mkubwa!
Wenzake ndani ya chadema wapo kila kona ya Tz wakikijenga chama (M4C) tena kwakujitolea wakila kwa mama ntilie, lakini yeye hata siku moja hajahudhuria mikutano ya chadema tangu alipoenda Songea na Mwanza kuipiga kampeni za udiwani mwezi wa pili kama si kosei! Amekuwa ni mtu wa ziara binafsi tu kila wiki yupo kwenye ndege, hana tofauti sasa na Rais wetu kwa ziara zilivyo:
Hivyo arejee kwenye mikingamo huru ya chama na tafakuri sahihi za ukombozi mororo bila kutumia mbinyo wa kuligawa taifa kwa makundi ya vijana, wazee na watoto!
Tunataka taifa lisimame pamoja, liongee lugha moja na litamalaki pamoja, huku tukijisifu uwepo wa uongozi safi wa kijana mwenzetu Zitto Zuberi Kabwe!!
pia pitia na hapa kiongozi Zitto hapo kwenye red jibu tuhuma eti unafanyaga haya madudu?Kwa hiyo democrasia ni kununua kurasa ya mbele ya mwananchi na kusema kuwa wambunge wanamtabiria kuwa rais?? hii democrasia ya hivi wewe umeiona wapi?? acha hizo.
Na hata wakileta video inayo"dhihirisha" kuwa jamaa walisema kuwa ZZK atakuwa kiongozi mkubwa katika taifa hili....haimaanishi ni Rais????...Jaji Mkuu,Spika,PM,Makamu wa Rais nk. ni viongozi wakubwa sana katika hii nchi ambayo ZZK hajafikia level hiyo. Kwanini Mwananchi waseme ni Urais?
Nitarudi
Bado ipo studio inafanyiwa mavocaling kuingiza sauti tuzitakazo!
ukwli ni kwamba Nassary,Fillikunjombe na Mdee,wote waliongea maneno yaliyoandikwa na gazeti la mwananchi.kwa wote tuliokuwepo pale uwanjani tulisikia,napata tabu kuamiini wanavyojikataa.Sasa naanza kuamini unafiki wa wanasiasa vijana kama akina nassari.iweje ukatae jambo ulilotamka kwa wako mdomo tena mbele ya watu wengi?
Mh. Mh. Deo Filikunjombe amestushwa sana na swala la yeye kumsafishia Zitto njia ya Urais. 'Hayo ya Zitto ni ya kupikwa, something wrong somewhere" Anashangaa kwa nini kawekewa maneno mdomoni ambayo namna au nyingine imemdhalilisha kwa wapiga kura wake na kuonekana kama kibaraka fulani?
Atazungumza na waandishi wa Habari/atatoa tamko lake hivi karibuni. Mh. Jembe Mh. Deo Filikunjombe anasema kwamba ametumwa na watu wake kuwawakilisha na siyo kuzungumzia mambo yasiyo na msingi tena ya kuropokwa.hakwenda kigoma mumsafishia yeyote njia... Stay tuned.
source mshirika wa Mheshimiwa
Atambue kuwa yeye amebeba dhamana ya tumaini la vijana wengi tena wakware wa fikra machipuko ambao ni hatari zaidi hasa walishwapo hata uongo tu!
Bado ipo studio inafanyiwa mavocaling kuingiza sauti tuzitakazo!