FikraPevu: Polisi aliyefyatua bomu lililoua mwandishi akamatwa, kushitakiwa kwa mauaji

Mkuu wangu, kama hujapata picha ni kwamba, Tume hyo inakazi maalumu kuonyesha uhusika wa CDM katika "mauaji" hayo, ili itoe mapendekezo yake na hatimaye ndoto za Tendwa na wanaomtuma zitekelezwe na baadae waje kutunga hyo sheria ya kubana shughuli za siasa katika mda usio wa uchaguzi....
Kazi za shetani hufanyakazi kwa uwazi sana huku wao wakidhani ni siri mno.

Haya mabadiliko kwenye nchi yanasimamiwa na Mungu mwenyewe, watapanga mambo yao sirini lakini yatawekwa hadharani! Wataendelea kunasa kwenye mitego walio tega wao, Mungu hadhhakiwi! Uwezo wao wa kudanganya tume u outsmart!
 
ckujua kama itachukua muda hivi,nilijua baada ya mazishi tu tutakutana court na ushahidi wa picha nyingi ukutani,sasa tume inafanya nini c kazi imeisha au ndo mpaka per dm ikate
 
Hakuna ushahidi wa kutosha jamaa atashinda kesi, ataachiwa huru na kudai fidia! KODI zetu tutamlipa Tshs. 1Bil kama fidia
 
Kama wauaji au muuaji ameshapatikana na hamna CHADEMA inakuwaje CHADEMA ikahusishwa na mauaji. Nape aseme sasa kwamba CHADEMA imehusika toka Morogoro hadi Iringa ila hakuna kiongozi wa CDM aliyekamatwa, hii ni kuchafuana. Ifike mahali CHADEMA wachukue hatua za kisheria pale wanaposingiziwa wameua ili kukomesha CCM kuichafulia CDM.
nape anajua kila kitu toka mwanzo,walishapanga na wakakabizi kazi kwa polis.maana taarifa yake kwa vyombo vya habari alitabiri haya kwani toka lini akawa nabii????na kama polis wangekuwa hawafanyi kazi kwa kupendelea chama tawala,nape alipaswa awe mhojiwa wa kwanza wa mauaji ya morogoro,lakini hakuna kitu kama hicho.tendwa aache upuuzi,asimamie haki na wala sio kutishia kufuta chama.ukweli anaujua wote na anafanya kazi kwa kuongozwa na magamba.whatever they do,hawawezi kushindana na uma.
mungu awarehem wote waliouwawa na polisccm.na ninamuomba damu zao ziwe juu ya wote wadhalimu na wauaji hawa.
 
Askari alikuwa na bomu kwa ajili ya shughuli za kufungua tawi!!?? Askari aliiba bomu hilo wapi??? Na aliyesahinisha hilo bomu ali akatekeleze amri ya wakubwa ni nani!! Ilikuwa alitumie kwa kiongozi gani ambaye ni adui wa CCM na serikali kwa ujumla???

Hapo ndo utaona wazi askari huyo anatolewa kama mbuzi wa kafara tu
 
Kuanzia kesho utaanza kusikia "Suala hilo liko mahakamani msilijadili".. Tanzania inaongozwa kama movie ya Kihindi.

Huu upumbavu uko Tanzania tu! Nikikumbuka ile kesi maarufu ya mauaji iliyomkabili O.J. Simpson huko Marekani na jinsi ilivyojadiliwa duniani kote wakati huo huo ikiwa Mahakama Kuu na hatimaye Mahakama ya Rufaa sina hamu. Naiona nchi yetu kama kuzimu fulani hivi.
 
Sasa kama askari aliyetekeleza mauaji anafahamika na wanajiandaa kumfikisha mahakamani, huo msururu wa tume za uchunguzi wa kazi gani? Hata hivyo natarajia kuona washitakiwa katika kesi hii ya mauaji ni pamoja na RPC wa Iringa.
Au tume zinalazimika kuwa nyingi ili kufanya cover up ya wahusika wakuu waliotoa amri ya kuzuia mikutano ya Chadema na kuua raia asiyekuwa na hatia.
Asante mkuu umeanza kuandika nilicho taka nami nikihoji sasa hizo tume zivunjwe tu zisiendelee kumaliza pesa za walipa kodi na mh Tundu lisu kasema zimeundwa kinyume cha sheria yani wameishiwa mpaka wana fanya maamuzi mabovu na ya hovyo kabisa pia mh.Mnyika aliwashauri tume ya nini wakati ushahidi upo? kamateni mhusika weka ndani
 
POLISI ambaye alifyatua bomu kwa karibu na kusababisha kifo cha Mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi, anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote, Fikra Pevu limefahamishwa.
alikuwa chini ya amr ya IGP na RPC.

Taarifa za kutoka Iringa zimeeleza kwamba kushitakiwa kwa askari huyo, kunafuatia kukamilika kwa uchunguzi wa awali ambao unathibitisha pasi shaka kwamba bomu alilofyatua ndilo lililosababisha kifo cha mwandishi huyo wa habari.

Imethibitishwa kwamba kilichousambaza mwili wa mwandishi huyo ni bomu maalumu linalorushwa kwa kutumia bunduki kwa nia ya kusambaza watu waliokusanyika kwa nia ya kutenda uhalifu na lilirushwa kwa karibu mno kinyume cha masharti na kanuni za matumizi yake.

Bomu hilo hutakiwa kurushwa kutoka umbali wa mita kati ya60 na 80, wakati askari huyo alilirusha kwa karibu mno na akimlenga mwandishi Mwangosi.

Katika tukio hilo, bomu hilo liliusambaratisha mwili wa Mwangosi na kumjeruhi ofisa mmoja wa polisi ambaye anaelezwa kutaka kumsaidia mwandishi huyo ambaye alikua akipigwa na polisi wenzake.
Marehemu Mwangosi aliuawa Jumapili iliyopita katika kijijini cha Nyololo, wilayani Mufindi, mkoani Iringa katika tukio ambalo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) walikuwa wakifungua tawi la chama chao, huku Polisi wakitumia nguvu kubwa kuzuia uzinduzi wa tawi hilo.

Source: Fikra Pevu | Kisima cha busara!

Na alikuwa anafanya kazi chni ya amri wanayoita halali ya polisi,that means IGP na RPC hawasalimiki, hapo kwenye red kama huyo afande alifanya hivyo anapaswa kutambiliwa kwa kuonesha nia yake hyo njema, atambuliwe hii itawafanya polisi wengine waadilifu kutiwa moyo, na sometime kuwa against amri dhalimu za wakuu wao,,,,,,,,,,samahani naomba nulize kitu kwani hii inchi ina rahisi madarakani? Mbona hasemi kitu, my goodness nw anaogopa hadi kivuli chake
 
Bomu la machozi linatakiwa kurushwa mita 60 au 80 ili kutawanya waandamanaji, ndiyo kosa lake watatuambia, sasa yeye alifyatua at close range, nia yake kuwatawanya polisi wenzake walomzunguka marehemu au kumtawanya marehemu.

Maajabu bomu lisianze kuwabamiza polisi wenzake migongoni walomzunguka marehemu lipenye mpaka katikati kutua tumboni kwa marehemu.

Nilikuwa nasikia FFU kabla ya kwenda kazini huwa wanavuta majani, nashawishika kuamini sasa
 

Huu upumbavu uko Tanzania tu! Nikikumbuka ile kesi maarufu ya mauaji iliyomkabili O.J. Simpson huko Marekani na jinsi ilivyojadiliwa duniani kote wakati huo huo ikiwa Mahakama Kuu na hatimaye Mahakama ya Rufaa sina hamu. Naiona nchi yetu kama kuzimu fulani hivi.

Mkuu ukiiangalia Tanzania kwa jicho la tatu unaweza kuwanasa vibao watawala... Huwa nikiangalia Bunge naona kama kijiwe cha kuilinda na kuitetea serikali (Hasa spika na naibu wake)
 
Katika hili sakata na mengine mengi yalokwishatokea ndani ya nchi hii kunamaswali mengi sana yanahitaji majibu.

Kama vitendo vya dhuluma dhidi ya wananchi vitaendelea wa kasi hii kwa kweli tanzania inaelekea kupozeza heshima iliyojijengea kwa miaka mingi ya kuwa kisima cha amani barani africa.

Wakati ni sasa watawala wautumia kufikiria upya namna wanavyotuongoza hasa ukizingatia kizazi cha sasa ni kizazi kinachoutafuta ukweli kwa njia zozote na kwa gharama zozote
 
Nadhani si busara jambo hili kuendeshwa kisiasa... tutakurupuka halafu baadaye tuta'chemka'....waacheni wataalam wafanye kazi zao..ashtakiwe kwa uzembe kazini au mauaji ... haya ndio mambo ambayo wataalam watayajua...tujifunze kuwaheshimu wataalam.....mambo ya kitaalam tuwaachie wataalamu.....anyway tusiumize sana vichwa kwani hata chanzo chenyewe hakijakaa sawasawa
 
Ilipozama MV Spice islanders, watu walifikishwaq mahakamani, rais akaunda Tume, kesi ikaondolewa mahakamani. The same happened ilipozama MV Skagit.

Sasa, mwandishi ameuawa, polisi anafikishwa mahakamani wakatyin IGP ameunda tume na waziri ameunda tume. Nini kitatokea kwenye kesi hiyo iwapo matokeo ya tume hizo yatatofaitiana na ushahidi uliotumika kumshitaki polisi?

Nini kitamfanya polisi huyu asikate rufaa kama akipatikana na hatia kwa kutumia ushahidi wa tume ambayo ilifanya kazi wakati ameshashitakiwa? Akitoa hoja kuwa tume zilifanya kazi kwa maelekezo ya kutafuta ushahidi dhidi yake, nani atabisha?
Nadhani taasisi zetu zinapaswa kuwa makini katika masuala makini, Tuache kufanya kazi 'kisengelenyuma'
 
Back
Top Bottom