Fikra za Mwalimu: Hizi hapa.. mzikubali au mzipinge!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Waswahili ndio waliosema kuwa "kwanini tuandikie mate wakati wino upo" na ndio hao hao waliosema "kwanini tugonganishe mawe, wakati kibiriti kipo" (well that is my own saying). Nimekuwa nikidai mara nyingi pasipo hofu kuwa Fikra za Mwalimu zikiangaliwa upya zinaweza kutuonesha mwanga wa wapi tunataka kwenda. Mara nyingi hata hivyo kuna watu ambao wanapinga fikra hizo (hata kama hawazijui) na kutoa madai lukuki juu ya "mwalimu alisema nini".

Ni kwa sababu hiyo basi nimeona nianze pole pole kwa kuweka mawazo ya Mwalimu na nimeyatoa wapi ili wale wanaozipinga waseme mawazo hayo yana makosa gani, na kama wanakubali basi tuendelee na mawazo mengine.

Lengo ni kujaribu kuonesha kuwa mtu akichukua muda kujifunza alichosema Mwalimu basi anaweza akajikuta yeye tayari ni mfuasi wa fikra za Mwalimu. Katika kufanya hivi nitoe maangalizi ya mambo ambayo ni ya kuzingatia.

a. Katika hoja zangu zote za utetezi wa Mwalimu na fikra zake sijawahi kusema kuwa Nyerere hakuwahi kufanya makosa au hakutambua makosa. Mara zote nimeonesha na mifano kuwa yeye mwenyewe alijua baadhi ya makosa yake na alikuwa tayari kukiri hivyo.

b. Katika utetezi wangu wa Mwalimu na fikra zake nyingi nimekuwa nikionesha kuwa Nyerere kama wanadamu wengine alikuwa na mapungufu yake na nitakuwa mwongo na mzandiki nikidai kuwa Nyerere hakufanya kosa hata moja wakati wa utawala wake. Hivyo, sifuati mafundisho ya Mwalimu nikiwa kama kipofu.

c. Katika kuonesha fikra ninazokubaliana naye haina maana ninakubaliana na maamuzi yote yaliyotokana na fikra hizo au njia zote zilizotumika kutekeleza fikra hizo. Hivyo, kukubaliana na fikra fulani haina maana nakubaliana na vitendo au maamuzi yaliyofuata, ninachokubaliana ni ile principle kuwa fikra hizo zinaweza kutekelezwa kwa namna mbalimbali na zikaendelea kubakia kuwa kweli.

d. Mawazo ya Mwalimu ni mawazo ya kifalsafa zaidi na kimtazamo ingawa baadhi yao hayakutekelezeka au hayakuongoza utekelezaji wa sera fulani. Hata hivyo ninaamini kuwa fikra zake bado zinahitajika leo hii kama kweli tunataka kujenga Taifa lililoendelea kwelikweli.

e. Mwisho, na nyie leteni fikra za Mwalimu na mziseme ni zipi na mnipe changamoto kama nakubaliana nazo au la. Nawaahidi kuwa mkileta jambo ambalo lilikuwa ni mawazo au fikra ya Mwalimu na likaonekana kweli hapo Mwalimu alipotoka basi kwa pamoja tutalitupilia mbali. Lakini pia nikiwaonesha kuwa fikra au mawazo fulani ni sahihi ni jukumu lenu pia kukubali kuwa ni jambo zuri na linapaswa kuzingatiwa. Huo unaitwa uungwana.

NB: Fikra za Mwalimu - mkusanyiko wa maoni, hoja, mitazamo, mawazo, ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambayo yalitolewa tangu kuingia kwake kwenye siasa za Tanganyika (Tanzania) na za kimataifa hadi alipofariki Oktoba 14, 1999. Fikra hizo zinaweza kuonekana katika hotuba, maandishi, mahojiano, vitabu, na nyaraka mbalimbali alinukuliwa.

Katika hili nyaraka za sera ambazo zilipitishwa na mtu zaidi ya mmoja kama (Azimio la Arusha, Mwongozo wa TANU na ule wa CCM, n.k)sitovihesabu kama fikra za Mwalimu hata kama zinakubaliana na mawazo yake.

Mko tayari?
 
Mkuu heshima mbele, wewe ziweke hapa tuzichambue ukweli nitakubali, lakini ninataka kuwaonyesha wananchi kwamba hatuko hapa tumedumaa as a nation kwa bahati mbaya, na sababu nyingi za msingi zinapatikana kwenye maneno na fikra za Mwalimu,

Yes yanayotukuta sasa, mengi ni uzembe wetu wenyewe kibin-adam, as a nation, lakini kisiasa ni lazima kuwe na someone to point a fingure at,

Otherwise, mkuu ahsante kwa finally, kukubali kuwa Mwalimu alikuwa bin-adam kama sisi, alikuwa na mapungufu makubwa ambayo baadhi yake ndio yametufikisha tulipo as a nation. I am more than happy kukata ishus kama utaweka maneno maneno moja baada ya lingine ya Mwalimu, hapa tuyachambue kulingana na mazuri yetu kitaifa na mabaya yetu.

Ahsante.
 
Mkjj,

sikujua kuwa kuna sehemu uliwahi kusema hapa kuwa Nyerere hakuwa binadamu kama sisi! Naona kazi kweli unayo kwenye hii mada!
 
Mkjj,

sikujua kuwa kuna sehemu uliwahi kusema hapa kuwa Nyerere hakuwa binadamu kama sisi! Naona kazi kweli unayo kwenye hii mada!

Kwa hili hata mimi Nyani nitamtetea kwa nguvu zangu zote kaka yangu Mwanakijiji. Hajawahi kusema au hata kukaribia kusema Nyerere hakuwa binadamu!!
 
Kwa hili hata mimi Nyani nitamtetea kwa nguvu zangu zote kaka yangu Mwanakijiji. Hajawahi kusema au hata kukaribia kusema Nyerere hakuwa binadamu!!

Ngabu,

Hili ni tatizo la perception hapa kuwa ukijaribu kutetea mambo aliyofanya nyerere basi inaonekana kuwa nawewe unataka Nyerere apewe usaint.

Unajua mimi nina kila sababu ya kumpondea Nyerere kwa sababu naamini kuwa alichangia Mrema kutopigiwa kura za kutosha na watu wa vijijini pale alipompigia kampeni Mkapa.

Ingawa mimi ni mpenzi mkubwa wa Mrema ambaye namwona kama ni my hero kwa alivyopigania haki za wanawake na wanyonge kwenye jamii na namna Mkapa alivyomnyanyasa kwa FFU na usalama wa taifa mara baada ya Mkapa kutwaa kiti cha enzi, lakini bado huwa nakiri kuwa sina sababu yoyote ya kumchukia mtu ambaye amekufa kuanzia 1999.

yaliyobaki mengi ni historia na ninaamini kuwa nchi yetu kama ilikuwa ya kubadilika ingeweza kubadilika kwa miaka hii yote ambayo Nyerere amekuwa hayupo madarakani au hapa duniani. For this one, sina sababu ya kuandika historia upya ili nitafute sababu ya kile ambacho ninashindwa kufanya sasa hivi!.

No wonder every time nina-side na Mwanakijiji katika mijadala ya kumpondea au kumsifia Nyerere.
 
Ngabu,

Hili ni tatizo la perception hapa kuwa ukijaribu kutetea mambo aliyofanya nyerere basi inaonekana kuwa nawewe unataka Nyerere apewe usaint.

Unajua mimi nina kila sababu ya kumpondea Nyerere kwa sababu naamini kuwa alichangia Mrema kutopigiwa kura za kutosha na watu wa vijijini pale alipompigia kampeni Mkapa.

Ingawa mimi ni mpenzi mkubwa wa Mrema ambaye namwona kama ni my hero kwa alivyopigania haki za wanawake na wanyonge kwenye jamii na namna Mkapa alivyomnyanyasa kwa FFU na usalama wa taifa mara baada ya Mkapa kutwaa kiti cha enzi, lakini bado huwa nakiri kuwa sina sababu yoyote ya kumchukia mtu ambaye amekufa kuanzia 1999.

yaliyobaki mengi ni historia na ninaamini kuwa nchi yetu kama ilikuwa ya kubadilika ingeweza kubadilika kwa miaka hii yote ambayo Nyerere amekuwa hayupo madarakani au hapa duniani. For this one, sina sababu ya kuandika historia upya ili nitafute sababu ya kile ambacho ninashindwa kufanya sasa hivi!.

No wonder every time nina-side na Mwanakijiji katika mijadala ya kumpondea au kumsifia Nyerere.

Okay...what a revelation!

Haya..sasa wewe na Mrema...Mwanakijiji na Nyerere...FMES na Malecela.....kwikwikwiiii

Ngabu je...?
 
Okay...what a revelation!

Haya..sasa wewe na Mrema...Mwanakijiji na Nyerere...FMES na Malecela.....kwikwikwiiii

Ngabu je...?
McCain?

Hivi tutakujaga kupiga hatua kadhaa mbele bila kupoint vidole kwa fulani na fulani? Maana naona kuanzia rais hadi sisi wananchi tunapenda kulundikia wengine lawama kwa vitu tulivyoshindwa kurekebisha.
 
Okay...what a revelation!

Haya..sasa wewe na Mrema...Mwanakijiji na Nyerere...FMES na Malecela.....kwikwikwiiii

Ngabu je...?

kwi kwi kwi,

wewe mbona baada ya ile thread yako kuhusu Mkapa kukata issues kule Davos kuna watu walisema kuwa Ngabu na Mkapa.....lol

Inabidi uje to reject and denounce if this aint true!
 
McCain?

Hivi tutakujaga kupiga hatua kadhaa mbele bila kupoint vidole kwa fulani na fulani? Maana naona kuanzia rais hadi sisi wananchi tunapenda kulundikia wengine lawama kwa vitu tulivyoshindwa kurekebisha.

Ahahahahahaaaa...Icadon we muhuni kweli wewe....eti McCain...
 
..............The only certain thing is that if we forget any of our principles, even when we are ignoring or breaking them, then we shall have betrayed the purpose of our revolution and Africa will fail to make its proper contribution to the development of mankind............
Hiyo hapo juu ndio JK na kundi la wafuasi wake wanatakiwa wajifunze....maadili+Nidhamu+Uzalendo................yaani hapo ukimuweka EL, BWM na wenzao wana-fit haswaaa
 
Hiyo hapo juu ndio JK na kundi la wafuasi wake wanatakiwa wajifunze....maadili+Nidhamu+Uzalendo................yaani hapo ukimuweka EL, BWM na wenzao wana-fit haswaaa


Hiyo ni fikra nzuri yenyewe kama principle bila kuwaweka inamuathiri nani. Yenyewe kama ilivyo ina makosa gani?
 
Mwanakijiji unajiandaa kufanya nini hasaa katika siasa za Tanzania,
  • Ni kweli una lengo la kuwakumbusha Watz kuhusu fikra hizo na ihishie hapo au kuna kitu unakificha?
  • Au umeamua kuwasaidia CCM NEC katika kukusanya kumbukumbu za Mwalimu?
 
Africa must change her institutions to make feasible her new aspirations; her people must change their attitudes and practices to accord with the objectives. And these changes must be positive, they must be initiated and shaped by Africa and not simply be a reaction to events which affect Africa.

Heshima mbele mkuu, maneno yake mwenyewe yanavyopingana na matendo na maneno yake, I know for a fact kuwa idea zake za ujamaa in full alizitoa u-China, baada ya ziara yek kule na kutletea bongo, sasa hapa anasema mwenyewe kumbe kwa nini zilishindwa, ni kwa sababu idea za agent wa change ni lazima zitokane na mazingara ya yule agent, yaani idea zisiende kuchukuliwa China, na kuwa practiced Tanzania, zitashindwa miserably!
 
How do we know that Nyerere was the best thing? See the problem I have with folks who regard Nyerere highly is that we don't the alternatives, at his time, to make a logical, objective comparison. I am not even sure if we know Nyerere for who is or what he wanted Tanzanians to believe. He managed to create an aura of admiration and worship. He created an atmosphere where no one would question his ideas.

Remember the days when we couldn't read anything other than Uhuru, Mzalendo, Daily News and Sunday News before Mfanyakazi came into existence to provide some kind of an entertainment relief? You remember the days when the 8:00 PM RTD news bulletin would be followed up by a "Ujumbe wa Leo" propaganda? I have to give it up to Nyerere. He ensured that Tanzanians couldn't run or hide from his ideology. If you feed someone junk for twenty (20) years, they would believe that crap. He even went as far as insulting our intelligence by putting a hoe against himself in the election. A hoe or a hammer, can you believe that? Who elects a hoe as the president?

What ticked me off is the fact that he forced us to sing derogatory songs against Oscar Kambona. We sang this tune during our morning mchakamchaka routines in High School, "Kambona ameolewa! Wapi?! Wapi?! Uingereza!" Was Kambona really that bad? What is the historical truth?

Since I was born past the time Kambona took off, I had to dig into the history materials to find out for myself. This is what I found.

When the TANU National Executive Committee met in Arusha January 26-29 1967 it turned out to be a stormy session. At this meeting Nyerere proposed that Ujamaa become the official policy of the government. Oscar Kambona objected strongly to this policy. Twice during these sessions, the Executive Committee adjourned in order to allow their three leaders, Nyerere, Kambona and Kawawa to go into private session. Each time that they returned to the Executive Committee it was apparent that Kawawa had supported Nyerere to defeat Kambona. The result was that the Arusha Declaration was adopted.


Source: Maryknoll Africa
 
Mkulu Kibunango,

Heshima mbele, mkulu MMJ, ameamua kutuelimisha kuhusu uzito wa maandishi ya Mwalimu, ambayo CCM wameamua kule Butiama, kuwa kuliweka taifa kwenye muelekeo ulio sawa, ni lazima wachapishe maandishi hayo kwa wingi sana na kuyasambaza labda ndio itakuwa dawa ya matatizo yetu, as a nation!
 
Quote: Mwalimu(Mwanakijiji)

For a revolution has begun in Africa. It is a revolution which we hope to control and channel so that our lives are transformed. It is a revolution with a purpose, and that purpose is the extension to all African citizens of the requirements of human dignity.[/B]


He also believed that Chinese leader Mao Tse Tung had undue and profound influence on Nyerere. He attributed that to Nyerere's first visit to the People's Republic of China in 1965, contending that it was after this trip that Nyerere decided to establish a one-party state after he returned to Tanzania.

Revolution imeanzia China.
 
THE NEED TO CHANGE:​

(
In the Epilogue of his collective work "Uhuru na Umoja" Pg. 22)​

…. Throughout these speeches and writings, and through all the activities of the Governments which I have been privileged to lead and support, there is however one recurring practical theme. It is the theme of change. For Africa must change; change from an area where people (take?) out an existence and adapt themselves to their environment, to a continent which challenges the environment and adapts it to man's need.

Africa must change her institutions to make feasible her new aspirations; her people must change their attitudes and practices to accord with the objectives. And these changes must be positive, they must be initiated and shaped by Africa and not simply be a reaction to events which affect Africa.

For a revolution has begun in Africa. It is a revolution which we hope to control and channel so that our lives are transformed. It is a revolution with a purpose, and that purpose is the extension to all African citizens of the requirements of human dignity. The task before us is a big and complicate one. In the process we shall have many decisions to make which involves clashes of principle – where we have to choose, let us say, between rapid development and individual freedom, or between efficiency and equality. There is and will be no simple o universal answer to such problems; the choice will have to be made in the light of historical circumstances and the conflicting needs of present and future.

The only certain thing is that if we forget any of our principles, even when we are ignoring or breaking them, then we shall have betrayed the purpose of our revolution and Africa will fail to make its proper contribution to the development of mankind.

But the opportunity is before us provided we have to courage to sieve it. For the choice is not between change or no change; the choice for Africa is between changing or being changed – changing our lives under own direction, or being changed by impact of forces outside our control.

In Africa there no stability in stagnation in this twentieth century; stability can only be achieved through maintaining balance during rapid change.

Tanzania has chosen to ride and try to harness the whirlwind which is sweeping through this continent. We know that some human dislocation is inevitable in this process, but we believe that much more would ultimately be involved in doing nothing. For we recognize that to try to maintain the status quo is to try to ignore the world.

We prefer to participate in the shaping of our own destiny, and we believe that we have the resolution and the ability to overcome difficulties and build the kind of society we want.
For those with courage to aspire, to believe, and to work, Tanzania is a challenging and exciting land. It is my privilege and my happiness to dedicate myself to its future.


SWALI: Je fikra hizo za Mwalimu kuhusu haja ya Africa na Tanzania kubadilika zimepitwa na wakati na tusiziangalie tena. Je hoja yake kuhusu haja ya Afrika and hence Tanzania kubadilika ina makosa gani?


Nionavyo mimi fikra za Mwalimu kuhusu kubadilika kwa Afrika bado zina nguvu kubwa.Kwakweli waafrika tukitaka maendeleo ya kweli tunahitaji kubadilika.Tubadilike na tuachane na ubinafsi.Huu ndiyo ugonjwa unaotumaliza waafrika(watanzania).Tuiache ile dhana ya kudhani kuwa uongozi ni ulaji wako wewe na mkeo,wanao na jamaa wengine wa karibu,Mali ya uma ni kufuja tu kwani una hasara nayo gani.Ubinafsi ndiyo ugonjwa wetu mkubwa sisi waafrika.Ubinafsi ndiyo umetufanya tuwe waroho wa madaraka,tuwe wadhulumaji,tuwe na chuki sisi kwa sisi na hivyo tuuane hovyohovyo,tuwe mafisadi,tuwe wazembe katika majukumu mbalimbali tuliyokabidhiwa etc etc hivyo kutufanya tuendelee kuwa masikini wa kutupwa mpaka leo hii pamoja na rasilimali zote tulizojaaliwa na mwenyezi Mungu.
Kwaleo Watanzania wenzangu wito wangu ni huo.Katika nafasi yoyote ile uliyonayo,shughuli yoyote unayojishughulisha nayo tafadhali achana na ubinafsi kuanzia sasa.Jitoe haswa kwa faida ya jamii yetu yote ya Tanzania na siyo kwa faida ya mkeo,wazazi,watoto na jamaa peke yao.
 
Back
Top Bottom