Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,581
- 46,178
Kila mtu amesikia au kuoana kwa uhalisia, taarifa au katika filamu mateso na ukatili binadamu wanaofanyiana kati yao. Tofauti katika mateso ya binadamu mmoja kwa mwingine na yale wanayofanyiana wanyama hayawani ni kwamba wanyama hutesana kwa sababu kubwa ya kugombea chakula na "survival"/ kuendelea kuishi. Kwa upande wa binadamu ni tofauti sana kwani mara nyingi binadamu mmoja humtesa binadamu mwenzake pasipo hizo sababu kuu mbili au bila sababu yoyote ya msingi katika asilimia kubwa ya visa.
Kama shetani hayupo, uchawi haupo, nguvu za giza hazipo, chanzo cha fikra asili za binadamu kuvumbua njia za mateso, kutengeneza zana za mateso na kutesana kati ya binadamu pasipo manufaa yoyote ya msingi kwa mtesaji zinatoka wapi?
Kama shetani hayupo, uchawi haupo, nguvu za giza hazipo, chanzo cha fikra asili za binadamu kuvumbua njia za mateso, kutengeneza zana za mateso na kutesana kati ya binadamu pasipo manufaa yoyote ya msingi kwa mtesaji zinatoka wapi?