WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Mahusiano yanayopelekea kupeana mimba yanaleta uchungu ama furaha kutegemeana na maelewano na makubaliano ya wahusika.Wanawake wengine hudhani kuwa njia ya kumkamata sawasawa mwanaume anayerukaruka ni kupata ujauzito.Wapo pia wanaume hufanya hivyohivyo, wakidhani ati ni kumshikisha adabu mwanamke anayeringa! Lakini wanaume wengi hawataki kusikia kwamba kitendo walichofanya kimezaa matunda na ndiyo hapo utakaposhangaa mtu anaruka futi 1000 kwamba hahusiki! Thanks God kuna kipimo cha DNA siku hizi - kwa hiyo hakuna kuruka wala kubambikiwa tena.
Maswali kadhaa hunijia akilini ninapofikiria wanawake wanaotelekezwa baada ya kupewa ujauzito:
1.Mtoto anayezaliwa bila ridhaa ya wazazi anaonekana vipi katika jamii?
2.Mwanamke anayetelekezwa baada ya kupewa ujauzito, anakuwa na mtihani gani kulea mimba na hatimaye mtoto?
3.Je kwa wale wanawake wanaojua raha ya kupata ujauzito uliopangiliwa au unaokubalika na wote ( mwanaume na mwanamke wahusika) mnaweza kusema nini kuhusu wanawake wanaoachwa wakipitia kipindi hiki kigumu cha matazamio na mashaka makubwa na hatimaye kuja kubeba mzigo wote unaoendana na malezi?
Hebu tuangalie takwimu kuhusu watoto wanaozaliwa na mzazi peke ( single parent)Kufuatana na Wade Horn and Andrew Bush, "Fathers, Marriage, and Welfare Reform," Hudson Institute Executive Briefing, 1997, Hudson Institute,
Maswali kadhaa hunijia akilini ninapofikiria wanawake wanaotelekezwa baada ya kupewa ujauzito:
1.Mtoto anayezaliwa bila ridhaa ya wazazi anaonekana vipi katika jamii?
2.Mwanamke anayetelekezwa baada ya kupewa ujauzito, anakuwa na mtihani gani kulea mimba na hatimaye mtoto?
3.Je kwa wale wanawake wanaojua raha ya kupata ujauzito uliopangiliwa au unaokubalika na wote ( mwanaume na mwanamke wahusika) mnaweza kusema nini kuhusu wanawake wanaoachwa wakipitia kipindi hiki kigumu cha matazamio na mashaka makubwa na hatimaye kuja kubeba mzigo wote unaoendana na malezi?
Hebu tuangalie takwimu kuhusu watoto wanaozaliwa na mzazi peke ( single parent)Kufuatana na Wade Horn and Andrew Bush, "Fathers, Marriage, and Welfare Reform," Hudson Institute Executive Briefing, 1997, Hudson Institute,
- Kwa wafungwa wa muda mrefu ,asilimia 70 ni watoto waliozaliwa bila kuwepo na baba kwa maana mama tu ndiyo alilea mtoto
- Asilimia 60 ya wabakaji na asilimia 75 ya vijana wadogo walioshtakiwa na mauaji wamekuwa bila kuwa na baba nyumbani.
- Watoto wasiokuwa na baba wanafeli mara tatu zaidi masomo kuliko wanaolelewa na baba na mama.
- Vilevile watoto hawa, wana uwezekano wa karibia asilimia 40% zaidi ya wenzao kunyanyasika kuliko wale walio na baba zao.