Girland
JF-Expert Member
- Jan 24, 2016
- 1,824
- 2,841
Je Wewe utaoa /kuolewa au utaoana na mwenza wako wa maisha? Maisha yamebadilika Sana zamani ungesikia, mwanamke akisema "huyu ni mume wangu, nimeolewa miaka mitano iliyopita ".Sasahivi utasikia "kuanzia tuoane 🤔ni mwaka sasa "!Je wewe ni muumini wa mrengo upi?
Mfumo wa haki sawa (feminism) unalenga kuleta usawa Kati ya mwanamke na mwanaume. Mfumo huu unapingana na ule halisia (ambao wanauita mfumo dume)!.
Lakini mfumo huu umeishia kuvunja ndoa nyingi na kuzalisha idadi kubwa ya "Single mothers ",kwa sababu ndoa ni ndoa pale ambapo mwanamke atakubali kuolewa!
Sasa "feminisiti "mje hapa mtuambie kwenye ndoa mnataka haki zipi? Kwanini hamkubali kuolewa na mnataka kuoana na waume zenu?
Upande wa pili sifa tele ziwaendee wanawake wanaojielewa (wife material), Hawa hawajikwezi na hawana makuu, ndoa zao zinadumu niamini mimi ni mwanamke ndiye anasababisha ndoa kuendelea au kuvunjika.
Mfumo wa haki sawa (feminism) unalenga kuleta usawa Kati ya mwanamke na mwanaume. Mfumo huu unapingana na ule halisia (ambao wanauita mfumo dume)!.
Lakini mfumo huu umeishia kuvunja ndoa nyingi na kuzalisha idadi kubwa ya "Single mothers ",kwa sababu ndoa ni ndoa pale ambapo mwanamke atakubali kuolewa!
Sasa "feminisiti "mje hapa mtuambie kwenye ndoa mnataka haki zipi? Kwanini hamkubali kuolewa na mnataka kuoana na waume zenu?
Upande wa pili sifa tele ziwaendee wanawake wanaojielewa (wife material), Hawa hawajikwezi na hawana makuu, ndoa zao zinadumu niamini mimi ni mwanamke ndiye anasababisha ndoa kuendelea au kuvunjika.