Utu Kwa Mali......watu wengi nowadays wanaangalia pesa tu....hii ni hatareKwa kumalizia,walivyofika ukweni yeye peke yake ndio hakuwa na ndinga,hivyo akaona aibu kurudi tena!
Duu. Pole sana Mkuu...enhe, ikawaje? Ulikomaa hadi ukaweka ndani au ulisepa mazima?Pole kaka wengi kuangalia unanini nakumbuka nilikaribishwa kwa mchumba angu mala ya kwanza Sweden aliumwa dada ake mchumba angu nilivyoenda odini kumdalimia ndugu nilitolewa balu utadhani mimi ndo mtoa roho pole sana kaka.
Hata heshima kwako binafsi ni muhimu sana mkuumkuu utu ni muhimu sana
aiseee nilikua sijui mkuuMkono mtupu haulambwi!
nashukuru sana mkuupole sana mkuu
wanajukwaa
leo hii mpaka naandika ujumbe huu nina huzuni na kitu kinachoma kama mkuki moyoni mwangu,
Hapa nilipo nipo kwenye msibwa takribani siku ya tano upande wa mke wangu yaani ukweni
Hapa nyumbani mke wangu ni mkubwa ana wadogo zake wawili mmoja ameolewa na mmoja anasoma chuo
Sasa balaa ni ile siku ya msiba tulipanda gari kuelekea msibani mimi na mke wangu kwakua kipato si kizuri niliona sina budi kuwahi mapema
Nilipofika pale msibani kama dakika tano yule mdogo wake na mke wangu wakaingia yeye na mume wake na gari nzuri ya kisasa dah mapokezi yao kama wafalme kiasi kulikuwa na mzee alimpisha kwenye kiti yule bwana ili hali mimi nilichukua mwenyewe mkeka
Baada ya pale mwenzangu alianza kuitwa kila kona chemba,niliwasikia wazee wakimuta baba njoo tupange mipango,baada ya hapo niliambiwa nichukue toroli nikakodi majamvi na maturubai na shemeji zangu
baada ya hapo shughuli zimeendelea leo ndio nimemalizwa kuambiwa nikafuate kuni nisaidiane na wapishi,
Yule bwana mdogo yupo na amezunguukwa na wazee na watoto wa mwenzangu wapo mapajani kwa bibi nahisi mke wangu pia amehisi kitu
Kila nikivuta picha kuna siku mama mkwe alikuja kumwangalia mke wangu alikua amejifungua akajamba mbele yangu nikaondoka kwa kujua ni kibinadamu ushuzi ulimponnyoka tu
Lakini leo nimeprove ule ushuzi ulikuwa na maana gani
kumbe leo nimeamini si lolote si chochote mimi ni ushuzi tu
uamuzi niliofikia nisikanyage tena pale ukweni kwa fedheha iliyonikuta aibu
ushauri wenye kujenga la kakini dah kama nimepigwa mkuki moyoni
assanteni