Fedha zilizoibwa BOT,kurejeshwa

Shukurani

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
251
11
Tunasubiri kuona utekelezaji wa hiliJK: Fedha zote zilizoibwa BoT zitarejeshwa

2008-02-01 08:50:57
Na Joseph Mwendapole


Rais Jakaya Kikwete, amewahakikishia Watanzania kuwa, fedha zote zilizoibwa (BoT) kupitia Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), zitarejeshwa serikalini na amewaomba wananchi kuwa na subira.

Aliyasema hayo katika hotuba yake ya kila mwezi kabla ya kwenda Addis Ababa kuhudhuria kikao cha Wakuu wa Nchi za Afrika.

``Napenda kuwahakikishia kuwa, Serikali inayo dhamira ya dhati ya kulifuatilia suala hili mpaka mwisho wake ujulikane. Mwisho ambao utakuwa na maslahi kwa taifa letu,`` alisema.

Alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, wameanza kuchukua hatua.

Aidha, alisema amewaagiza watoe taarifa kwa wananchi mara kwa mara kadri inavyowezekana pamoja na haja ya kuwa waangalifu kutokutoa mengi yahusuyo uchunguzi wanaoufanya ili ushahidi usiharibike.

Alisema anaamini kuwa, kazi hiyo itakamilika ndani ya kipindi cha miezi sita waliyopewa na aliwataka wananchi wenye taarifa zitakazosaidia katika uchunguzi na hatua katika suala hilo waisaidie kamati hiyo.

Rais Kikwete aliwapongeza wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young kwa kazi nzuri waliyoifanya na kutoa taarifa ya kina kuhusu matatizo yahusuyo matumizi ya fedha za Akaunti hiyo.

Kuhusu suala la mafuta, Rais Kikwete alisema bado bei ya nishati hiyo iko juu sana na kuathiri uchumi wa nchi zote duniani tajiri na maskini ingawa nchi maskini zinaathirika zaidi.

``Hili si jambo geni kwetu…Napenda kurudia kauli zangu za siku za nyuma kwamba, hatuna uwezo mkubwa wa kujikinga na athari za bei za mafuta tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu na hasa wabanifu katika matumizi ya mafuta na tuepuke matumizi yasiyo ya lazima,`` alisema.

Alisema wakati huo huo serikali itaendelea na juhudi za kuzalisha nishati mbadala kutokana na mimea hususan miwa, mawese na mbono-kaburi (jatropha) na kwamba juhudi hizo zikifanikiwa zitasaidia kupunguza mzigo wa mafuta yanayoagizwa kutoka nje.

Alisema ana furahi kuona juhudi hizo zina mwelekeo mzuri na katika miaka michache ijayo Tanzania itaanza kunufaika na matunda yake.

Akizungumzia ujio wa Rais George Busha wa Marekani, Rais Kikwete aliwaomba watanzania wampokee mgeni huyo kwa mujibu wa mazoea na desturi za ukarimu wa Kitanzania.

``Huu ni ugeni mkubwa na wa heshima kubwa kwa nchi yetu. Rais George Bush ameipa heshima kubwa nchi yetu kwa kuamua kutumia sehemu kubwa ya ziara yake ya Bara la Afrika hapa kwetu. Ameonyesha upendo mkubwa kwetu nasi tumuonyeshe hivyo hivyo,`` alisema.

Aliomba pia Watanzania wajitokeze kwa wingi siku hiyo kumpokea mgeni huyo mashuhuri.

SOURCE: Nipashe
 
N zilizoenda kwenye kampeni za CCM zitarudishwa?

zile za deep green zitarudishwa?na zitztoka wapi , za kagoda nazo watarudisha chama tawala ama watatuambia tuu kuwa tayari zimerudishwa na huo utakuwa mwisho wa picha?

Tutawezaje sisi wananchi kujua kuwa ni kweli zimerudi jikoni na sio mazingaumbwe ya kuambiwa zimerudi na zikaandikwa kwa maandishi kisha tukafungwa goli la kisigino....
 
N zilizoenda kwenye kampeni za CCM zitarudishwa?

zile za deep green zitarudishwa?na zitztoka wapi , za kagoda nazo watarudisha chama tawala ama watatuambia tuu kuwa tayari zimerudishwa na huo utakuwa mwisho wa picha?

Tutawezaje sisi wananchi kujua kuwa ni kweli zimerudi jikoni na sio mazingaumbwe ya kuambiwa zimerudi na zikaandikwa kwa maandishi kisha tukafungwa goli la kisigino....
Kuna kiini macho hapo kwanza ninadhani kwamba kutakuwa na udanganyifu usio wa kawaida kwani hawawezi kuzirejesha zimenunulia fulana za kampeni hapo ni danganya toto tu.
 
Mpaka kieleweke, maswali ni mengi kuliko majibu ambayo yanaweza kukupa ufumbuzi wa hili suala. Ushahidi wa kuona ni muhimu kuliko ushahidi wa kusikia. Jk inabidi atupe njia ambayo itatufanya tuamini kuwa zimerudi> labda tutahitaji kamera za vyombo vya habari kutuletea matukio ya mabunda ya noti yakiingia kwenye acount za BOT. hizo zilizoenda chama tawala, mimi sijui zitarudi vipi? Muulize Makamba,japo kakana CCM hausikii
 
Naanza kuhisi kuwa kuna harakati zinafanyika ili hizi pesa ziwe 'write-offs' pia.

Si mmeona hapa: http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9406

Writeoff imetumika kifanisi kama silver bullet ya kusimamia mapungufu yaliyopo na yaliyosababisha upoteaji wa pesa hizo.


Nina mashaka kwa haya mabilioni, lililotendeka kwa hizo nyingine ni rahisi sana kutendeka kwa hizo za EPA. Uongozi wa kutenda hivo upo na unaonekana uko mstari wa mbele katika hilo. Tusishangae kusikia wizi huo umekuwa offset na masalio ya misaada ya budget ya kujengea twin towers, au yamekuwa offset na misaada iliyobakia katika mradi wa ukimwi au malaria au maji kutokana na serikali kufanyia usimamizi vizuri kazi zake hivyo kuwa na ziada.... kwa jinsi nilivo ona mpaka sasa, mengi yapo ambayo yanaweza kuhalalisha offset ya pesa hizo zote!!

SteveD.
 
hat zikirejeshwa mtajulishwa??changa la macho tu..mie nawasikitikia wana wa watanzania ambao bado mnafikiri kutatokea madabiliko kamaa CCM ikiwz madaraakni.nilijishikiza serikalini kwa muda na bado nipo,nimejaribu kujenga mazingira mazuriu ya maendeleo ila wafanyakzi wenzangu njaa zinawauma hawataki.

tatizo sio watu,tatizo ni fikra za watu amabao wanahisi CCM ikong'oka basi na ulaji kwao ni mwisho.na tatizo kubwa nililloliona ni kwamba.hawana Elimu ya kutosha.

Cha kufanya ni kuamasha ari ya Vijana wasomi walioko huko Vyuoni waje tuenmdeleze mapambano na kumkoma Nyani Giladi.

Invisible tumemiss miziki mikali,Tunaomba uniwekeee japo hata wa zamani niburudike.
 
Yangu macho ila ni muhimu tusiruhusu kukata tamaa hapa kwani kila jambo lina mwanzo na mwisho wake hivyo tuwepo hadi kuuona mwisho wa jambo hilo.
 
Gembe wazo lako ni zuri,hata miye nilifanya kazi serikalini mara baada ya kugraduate toka university,just within 3 month nikashindwa kufanya kazi kabisa,maana unafanya kazi na generations yenye 45 to 55 yrs old, hakuna jipya na hawataki mabadiliko,nikaamua kujiuzulu hiyo kazi ndani ya masaa 24. Ni kazi ngumu ila ushindi lazima
 
``Napenda kuwahakikishia kuwa, Serikali inayo dhamira ya dhati ya kulifuatilia suala hili mpaka mwisho wake ujulikane. Mwisho ambao utakuwa na maslahi kwa taifa letu,`` alisema.

Unaweza kupata kihindihindi kwa maneno kama hayo. Dhamira ya dhati ingeaza kwa kuiweka wazi riport yenyewe.Balali angesharejeshwa nchini kujibu/kutoa ushahidi au utetezi.

hakuna dhamira ya dhati wala nini, zote zuga,danganya toto.
 
N zilizoenda kwenye kampeni za CCM zitarudishwa?

zile za deep green zitarudishwa?na zitztoka wapi , za kagoda nazo watarudisha chama tawala ama watatuambia tuu kuwa tayari zimerudishwa na huo utakuwa mwisho wa picha?

Tutawezaje sisi wananchi kujua kuwa ni kweli zimerudi jikoni na sio mazingaumbwe ya kuambiwa zimerudi na zikaandikwa kwa maandishi kisha tukafungwa goli la kisigino....


Una uhakika gani kuwa zilikwenda huko? Sisi tunakipenda chama chetu, tumejitolea kwa hali na mali. Ulikuwa wapi wakati wa harambee za kuchangisha pesa za uchaguzi? Vyama vingine vilikaa bweteteeee kungoja ruzuku na misaada kutoka nje. CCM tulianzisha harambee. Leo mnatuita wezi. Wameiba waajiriwa wa sirikali na siyo chama.
 
Kwani walijikopesha mpaka kusema kwamba wataziresjesha, au ndio njia ya ku-pre-empt watu kuchukuliwa hatua za kinidhamu, kama kufungwa baada ya kuzirejesha?
 
Una uhakika gani kuwa zilikwenda huko? Sisi tunakipenda chama chetu, tumejitolea kwa hali na mali. Ulikuwa wapi wakati wa harambee za kuchangisha pesa za uchaguzi? Vyama vingine vilikaa bweteteeee kungoja ruzuku na misaada kutoka nje. CCM tulianzisha harambee. Leo mnatuita wezi. Wameiba waajiriwa wa sirikali na siyo chama.

Acha kuchekesha watu wewe.
Eti unakipenda chama?
Hata mamam mzazi wa Kibka mashuri kule Manzese ana mpenda mwanae kwa upendo wake wote lakini upendo huo hauzuii kijana wake kuwa na kuitwa kibaka.
Unakipenda kwa sababu kimekupa kula haramu, SISIEMU hamli mkashiba mpaka mlize wenzenu.

Kwamba wameiba waajiriwa wa sirikali siyo chama ni kauri ionyeshayo ufinyu wa Siasa na Utendaji katika shguli nzima za uchumi.

Siasa ya chama chochote kilichoko madarakani ikitafsiriwa inambana na kumpa mwongozo kila mtu ndani ya serikali na nchi.

Kwamba kundi la watu katika serikali linaweza kuiba fedha zinazo zidi zile viongozi wa chama chenu wanavaa suti na kwenda na mabakuli kuomba kwa wafadhiri, ni dalili kwamba chama chenu ni mkusanyiko wa wazee walo jaa mvi za uhuni kuliko busara.

Iweje wizi wa $133Billion ukatokea cham kisijue na pale kikiambiwa kuna wizi kikabisha kwa makelele mazito huku kimekunja ndita na ngumi tayari kuanzisha ugomvi? Mwishoni kama kichekesho na kujifedhehesha Kiongozi mkuu wa SISIEMU anasimama wima na kuhutubia wananchi akidai fedha zitarudishwa.
Usanii.

Mnajikanyanga kwa maneno huku midomo ikicheza cheza kama mmekula kaa la moto wa kuokea chips!

Ohh! BOT mambo swanu kabisa, ni njama za Wapinzani tu wanatuonea gele kwamba tumeiba sisi na sio wao.
Ohh Fedha zitarudishwa japo zile tulizo tumia kwnye kampeni itakua haiwzekani kwani ni ninyi wenyewe wananchi mmefaidi kupitia Rushwa!

Mmepita kukanusha nchi nzima kwamba hakuna wizi leo mnatuambia fedha zitarudishwa ya kweli hayo?

Toka lini wanachama wa SISIEMU mkakaa mkao wa kuchangishana kwa ajili ya uchaguzi?
Hiyo mikutano mnakutana usiku kama misukule au wanga?
Wapi huko mkutanako? Bagamoyo?

Hebu tupe makabrasha au barua mlizo andikiana kualikana na wapi mlikutana kuchangishana hivyo visenti.

Wewe sema ninyi ni mabingwa wa kuchanga pesa pale tu mlipo na uwezo wa kupeleka midomo,matumbo na makalio yenu.
Michango kama ya Kitchen Party au Bachelors Party hiyo mnaiweza kuliko hata walioanzisha huo utamaduni.

SISIEMU mchangishane fedha wakati utamaduni wenu ni wizi,unyanganyi na unyanyasaji???

SISIEMU haioperate mafichoni, ninyi wezi wakubwa, msio stahili hata kupewa dhamana ya kuongoza familia zenu.

Ndiyo maana wakati ule wa kampeni mlivumisha kwamba Rostam Azizi amepewa fedha na wazazi wake waishio Iran ili kukisaidia chama cha SISIEMU, kumbe ilikuwa ni janja yenu ya kumbariki Rostamu kwa Roho chafu ya Ibilis ili kutukata maboya juu ya wizi kupitia Kampuni zenu Feki,na yeye akionekana anagawa fedha ionekane ni milionea wa kutupwa.

Eti wazazi wa Rosatmu ni Mabilionea huko Iran! Mnawazimu kweli ninyi nyamafu hayawani mnaowaza zaidi kwa msuri kuliko ubongo.
Milionea yeyote yule haondoki kwao labda awe na so, yeye Rostamu kama kwao wana ngawira za kumwaga anatafuta nini huko Igunga?
Si aende kwao Iran naye akafunge kilemba kama wenzie?
Janja yenu imejulikana sasa mnatafunana ndimi na mikia yeni kama vibwengo walozinguliwa nguvu ya hirizi zao.

Mkavie akili zenu na kujiunga kwenye Bench la KANU na UNIP. Huko mkaoze,mkanuke na kutoleana harufu mbaya ya maovu yenu.
 
Acha kuchekesha watu wewe.

Mnajikanyanga kwa maneno kama mmekula kaa la moto wa kuokea chips!
Ohh! BOT mambo sawnu ni njama za Wapinzani tu.
Ohh Fedha zitarudishwa!
Mmepita kukanusha nchi nzima kwamba hakuna wizi leo mnatuambia fedha zitarudishwa ya kweli hayo?

Toka lini wanachama wa SISIEMU mkakaa mkao wa kuchangishana kwa ajili ya uchaguzi?

Hebu tupe makabrasha au barua mlizo andikiana kualikana na wapi mlikutana kuchangishana hivyo visenti.

Wewe sema ninyi ni mabingwa wa kuchanga pesa pale tu mtakapo kuwa na uwezo wa kupeleka midomo,matumbo na makalio yenu.
Michango kama ya Kitchen Party au Bachelors Party hiyo mnaiweza kuliko hata walioanzisha huo utamaduni.

SISIEMU mchangishane wakati utamaduni wenu ni wizi,unyanganyi na unyanyasaji???

SISIEMU haioperate mafichoni, ninyi wezi wakubwa, msio stahili kupewa hata dhamana ya kuongoza familia zenu.

Ndiyo maana wakati ule wa kampeni mlivumisha kwamba Rostam Azizi amepewa fedha na wazazi wake waishio Iran ili kukisaidia chama cha SISIEMU, kumbe ilikuwa ni janja yenu ya kumbariki Rostamu kwa Roho chafu ya Ibilis ili kutukata maboya juu ya wizi kupitia Kampuni zenu Feki.
Eti wazazi wa Rosatmu ni Mabilionea huko Iran! Mnawazimu kweli ninyi nyamafu hayawani mnaowaza zaidi kwa msuri kuliko ubongo.

Janja yenu imejulikana sasa mnatafunana ndimi na mikia kama vibwengo walozinguliwa nguvu ya hirizi zao.

Mkavie akili zenu na kujiunga kwenye Bench la KANU na UNIP. Huko mkaoze,mkanuke na kutoleana harufu mbaya ya maovu yenu.

Madilu wa Madela
easy easy Mzee .Sikuwahi kukujua kwamba una hasira namna hii . Lakini najua si hasira bali ni uzalendo ulionao kwa Nchi yetu . Huyu Mamkwe mwache aendelee kukaa na wakwe zake .
 
Lunyungu unajua hawa Mahabithi wa SISIEMU wanatulazimisha kuingia kwenye kundi lao la ujinga kwa maneno yao ya kujikanyaga.

Kweli kuwafinya hatuwezi, na kuwapakia tunashindwa?

Nikipata wasaa ni lazima niwape vipande vyao.
 
Kwanza atueleze zile za RADA kabla hajaleta porojo zake.
 
MADILU:::BIG UP BR TUNAWAITAJI WATU KAMA NYIE KWENYE NCHI HII,,,,,,MAMAMKWE HUYU MSAMEHENI MSHAON""MA.....WAT NEXT??MSIJIBISHANE NA HUUYU MTU MUNGU ASIJE WAWEKA PEPONI KABLA MKIWA NA PUMZI ZENU....Teeehtehehhe
 
Back
Top Bottom