Fedha zilimwagwa kumng'oa Askofu Malasusa KKKT...

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,468
911,172
Fedha zilimwagwa kumng'oa Askofu Malasusa KKKT
Wednesday, 08 December 2010 20:21 0diggsdigg

Mwandishi Wetu
MBINU chafu za kutumia fedha kurubuni wajumbe ili wafanye mapinduzi zimeelezwa kuwa zilitumika bila mafanikio kwenye mkutano mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP)ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ili kumng'oa Askofu Alex Malasusa.

Fedha hizo zinadaiwa kutolewa na wanasiasa wenye fedha ambao mipango yao ni kujenga mitandao kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2015.

Hata hivyo, Askofu Malasusa, ambaye pia ni mkuu wa KKKT nchini, alifanikiwa kuendelea kuongoza dayosisi hiyo baada ya kushinda kwa kishindo kwenye kura ya maoni iliyopigwa mwanzoni mwa mkutano huo wa DMP.
Viongozi wa DMP hawakutaka jana kuzungumzia suala hilo wala tofauti zilizoibuka kwenye mkutano huo unaomalizika leo mjini Bagamoyo, lakini Katibu Mkuu wa dayosisi hiyo anayeshughulikia utawala na utumishi, Ernest William alisema kikundi kidogo cha watu kilitaka kuvuruga dayosisi hiyo na ndio maana kilitoa habari hizo wakati wa kuelekea mkutano mkuu.

Lakini akabainisha kuwa idadi kubwa ya kura iliyotaka Askofu Malasusa aendelea kuiongoza DMP ni uthibitisho tosha kuwa kiongozi huyo amefanya kazi kubwa na inayokubalika.
“Mtu ukisemwa vibaya ujue ndio unafanya vizuri. Kwanza maneno haya yameibuka wakati tunaelekea katika uchaguzi, hii inaonyesha wazi kuwa ni uvumi tu ulioibuliwa na watu fulani,” alisema mchungaji William.

Baadhi ya watu walio kwenye mkutano huo waliiambia Mwananchi kuwa kuna fedha nyingi zilimwagwa kwa ajili ya kufanya mapinduzi hayo, lakini njama hizo ziligundulika mapema ndipo wajumbe walipolazimisha kufanyika kwa mabadiliko ya ratiba ili ajenda ya kupiga kura ya imani kwa Askofu Malasusa iendeshwe mwanzoni.

Awali hoja hiyo ilipingwa na ikatakiwa mkutano uendeshwe kama ulivyopangwa hadi mjumbe mmoja alipoibuka na hoja kuwa kupiga kura ni muhimu ili kuondoa wasiwasi kwa mwenyekiti, ambaye ni Askofu Malasusa na wajumbe baada ya barua kusambazwa kwenye sharika zote kumsafisha kiongozi huyo Jumapili iliyopita.

"Hali ilikuwa ngumu na kama uchaguzi ungefanyika mwishoni, watu wangeweza kubadilishwa kabisa msimamo," alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo.
Habari zinadai kuwa baada ya kuafikiana kupiga kura ya maoni mwanzoni mwa mkutano juzi, karatasi za kura zilianza kuandaliwa lakini mjumbe mwingine akaibuka na kutoa hoja kwamba upigaji kura usiwe wa siri.

"Sisi ni Wakristo na mambo yetu tunaendesha kwenye nuru, kwa hiyo hakuna sababu ya kupiga kura za siri," mjumbe huyo alimnukuu mtoaji hoja ambaye alishangiliwa na kupitishwa uamuzi huo uliomfanya Askofu Malasusa athibitishwe kwa asilimia 96.6 ya kura kuendelea kuiongoza dayosisi hiyo hadi atakapostaafu utumishi wa kanisa.

Habari za kufukuta kwa mgogoro huo ziliwekwa bayana wakati msaidizi wa askofu wa DMP, Mchungaji George Fupe alipowaeleza waandishi Novemba 23 kuwa kuna kikundi cha watu wanaojiita waumini wa kanisa hilo ambao alidai kuwa walikuwa wakifanya njama za kuhujumu mkutano huo kwa kutumia magazeti.
Mchungaji Fupe alieleza, hata hivyo, kuwa kanisa halijatikiswa na njama hizo na kwamba litaendelea na mkutano wake kama ulivyopangwa.
 
Yaani mpaka kwa kanisa wanaanza kutumia rushwa kheri RC ambao jina linatoka ROME
 
Sitashangaa kama Jina la Mluteri Edward L halijajitokeza katika sakata hili.
Tamaa ya pesa na madaraka inapompofua mtu hata uwezo wa Mungu hauoni.
 
Sitashangaa kama Jina la Mluteri Edward L halijajitokeza katika sakata hili.
Tamaa ya pesa na madaraka inapompofua mtu hata uwezo wa Mungu hauoni.



ni kwamba shetani yuko kila mahali na anataka kuitawala dunia ole wenu mtakaomruhusu awatumie katika tamaa zenu
 
Inawezekana Lowassa na kundi lake hawafurahi Askofu Malasusa anapokemea ufisadi nchini; ndio maana wameanza kuja na mbinu za kutaka kuyachafua madhehebu yenye ushawishi mkubwa katika jamii!!
 
inawezekana lowassa na kundi lake hawafurahi askofu malasusa anapokemea ufisadi nchini; ndio maana wameanza kuja na mbinu za kutaka kuyachafua madhehebu yenye ushawishi mkubwa katika jamii!!

mtasema sana mungu mkubwa malasusa na lowasa ni marafki wakubwa ata mbnu za kumhujumu aliyezizuia ni mtandao wa lowasa
 
Huyu jamaa Lowasa yupo kila angle duu,kama mchezaji wa mpira ni midfied kisheti, lakini watanzania hatudanganyiki.
 
Hilo tukio mbona ni la muda mrefu. Na kwanini kila jambo baya anahusishwa lowasa ! Itafikia mahali hata mtu akinyimwa unyumba na mke wake atasema kuna mkono wa lowasa!
 
Fedha zilimwagwa kumng'oa Askofu Malasusa KKKT
Wednesday, 08 December 2010 20:21 0diggsdigg

Mwandishi Wetu
MBINU chafu za kutumia fedha kurubuni wajumbe ili wafanye mapinduzi zimeelezwa kuwa zilitumika bila mafanikio kwenye mkutano mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP)ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ili kumng'oa Askofu Alex Malasusa.

Fedha hizo zinadaiwa kutolewa na wanasiasa wenye fedha ambao mipango yao ni kujenga mitandao kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2015.

Hata hivyo, Askofu Malasusa, ambaye pia ni mkuu wa KKKT nchini, alifanikiwa kuendelea kuongoza dayosisi hiyo baada ya kushinda kwa kishindo kwenye kura ya maoni iliyopigwa mwanzoni mwa mkutano huo wa DMP.
Viongozi wa DMP hawakutaka jana kuzungumzia suala hilo wala tofauti zilizoibuka kwenye mkutano huo unaomalizika leo mjini Bagamoyo, lakini Katibu Mkuu wa dayosisi hiyo anayeshughulikia utawala na utumishi, Ernest William alisema kikundi kidogo cha watu kilitaka kuvuruga dayosisi hiyo na ndio maana kilitoa habari hizo wakati wa kuelekea mkutano mkuu.

Lakini akabainisha kuwa idadi kubwa ya kura iliyotaka Askofu Malasusa aendelea kuiongoza DMP ni uthibitisho tosha kuwa kiongozi huyo amefanya kazi kubwa na inayokubalika.
“Mtu ukisemwa vibaya ujue ndio unafanya vizuri. Kwanza maneno haya yameibuka wakati tunaelekea katika uchaguzi, hii inaonyesha wazi kuwa ni uvumi tu ulioibuliwa na watu fulani,” alisema mchungaji William.

Baadhi ya watu walio kwenye mkutano huo waliiambia Mwananchi kuwa kuna fedha nyingi zilimwagwa kwa ajili ya kufanya mapinduzi hayo, lakini njama hizo ziligundulika mapema ndipo wajumbe walipolazimisha kufanyika kwa mabadiliko ya ratiba ili ajenda ya kupiga kura ya imani kwa Askofu Malasusa iendeshwe mwanzoni.

Awali hoja hiyo ilipingwa na ikatakiwa mkutano uendeshwe kama ulivyopangwa hadi mjumbe mmoja alipoibuka na hoja kuwa kupiga kura ni muhimu ili kuondoa wasiwasi kwa mwenyekiti, ambaye ni Askofu Malasusa na wajumbe baada ya barua kusambazwa kwenye sharika zote kumsafisha kiongozi huyo Jumapili iliyopita.

"Hali ilikuwa ngumu na kama uchaguzi ungefanyika mwishoni, watu wangeweza kubadilishwa kabisa msimamo," alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo.
Habari zinadai kuwa baada ya kuafikiana kupiga kura ya maoni mwanzoni mwa mkutano juzi, karatasi za kura zilianza kuandaliwa lakini mjumbe mwingine akaibuka na kutoa hoja kwamba upigaji kura usiwe wa siri.

"Sisi ni Wakristo na mambo yetu tunaendesha kwenye nuru, kwa hiyo hakuna sababu ya kupiga kura za siri," mjumbe huyo alimnukuu mtoaji hoja ambaye alishangiliwa na kupitishwa uamuzi huo uliomfanya Askofu Malasusa athibitishwe kwa asilimia 96.6 ya kura kuendelea kuiongoza dayosisi hiyo hadi atakapostaafu utumishi wa kanisa.

Habari za kufukuta kwa mgogoro huo ziliwekwa bayana wakati msaidizi wa askofu wa DMP, Mchungaji George Fupe alipowaeleza waandishi Novemba 23 kuwa kuna kikundi cha watu wanaojiita waumini wa kanisa hilo ambao alidai kuwa walikuwa wakifanya njama za kuhujumu mkutano huo kwa kutumia magazeti.
Mchungaji Fupe alieleza, hata hivyo, kuwa kanisa halijatikiswa na njama hizo na kwamba litaendelea na mkutano wake kama ulivyopangwa.
Hizi figisu akina EL na genge lake likiongozwa na "show" wamezianza zamani sana!! Halafu nyumbu wanadakia juujuu!
 
Back
Top Bottom