Fedha za wafadhili zasababisha umeme kutopitishwa chini ya ardhi

Andindile

JF-Expert Member
Mar 18, 2009
304
16
Hatimaye waziri Ngereja amefafanua kuwa kitu kilichowazuia kupitisha umeme chini ya ardhi ni kwa sababu fedha wanazotumia ni za ufadhiri kutoka Shirika la maendeleo la Japani (JICA). Kwa kauli hii inaonyesha kuwa watoa fedha walikuwa na ajenda yao ambayo hawakuiweka wazi. Ajenda yenyewe ilikuwa kuhakikisha yale manguzo makubwa ya aluminium yananunulika la sivyo watu wangekosa kazi labda na kiwanda chao kufungwa kwa kukosa soko la kuuza hizo nguzo. Mahali ambapo kunakuwa na ajenda ya siri nyuma yake hata taarifa za tafiti za athari ya kimazingira na afya ya binadamu wanazosema kuwa zilifanywa na serikali na kuthibitisha kuwa umeme huo hauna madhara ukipitishwa karibu na makazi ya watu nazitilia shaka kwa sababu taarifa hizo zililenga kuhakikisha kuwa mradi unatekelezwa kwa udi na uvumba. Jamani tusubiri baada ya miaka michache tutakuja kusikia wakazi wote waliokaribu na njia ya umeme wa msongo mkuwba along Sam Nujoma Road wakatakiwa kuhama ili kuwaepusha na madhara ya umeme huo.

Habari zaidi soma mwananchi la J.Tatu 08/03/2010

Ni mtazamo wangu tu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom